Friday, June 24, 2022

UJUMBE WA JIMBO LA HAUT KATANGA WAFANYA ZIARA YA KIKAZI NCHINI


Naibu Katibu Mkuu wa Wizara ya Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki Balozi Fatma Rajab akisisitiza jambo alipokuwa akizungumza na ujumbe kutoka jimbo la Haut Katanga la Jamhuri ya Kidemokrasia ya Kongo (DRC) walipotembelea Ofisi za Wizara jijini Dodoma. Ujumbe huo wa watu tisa unaongozwa na Gavana wa jimbo hilo Mhe. Jacques Kyabula Katwe

Ujumbe kutoka jimbo la Haut Katanga la Jamhuri ya Kidemokrasia ya Kongo (DRC) umeanza zaira ya siku 4 ya kikazi nchini. Ujumbe huo wa watu tisa unaongozwa na Gavana wa jimbo hilo Mhe. Jacques Kyabula Katwe

Pamoja na masuala mengine ziara hiyo inalenga kujionea na kujifunza namna Tanzania inavyoendesha shughuli za kilimo cha mazao ya biashara na chakula. 

Ujumbe huo umeanza zaira yake nchini kwa kutembelea Taasisi mbalimbali za serikali sambamba na kuonana na kufanyamazungumzo na viongozi waandamizi wa Serikali ikiwemo Waziri wa Kilimo Mhe. Hussein Bashe, Waziri wa Madini Mhe. Dotto Biteko na Naibu katibu Mkuu wa Wizara ya Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki Balozi Fatma Rajab. Vilevile walipata fursa ya kutembelea Bunge la Jamhuri ya Muungano wa Tanzania. 

Akizungumza kwa nyakati tofauti Gavana Jacques Kyabula Katwe ameeleza kuwa ziara yake nchini imetokana na kutuvitiwa kwake na namna Tanzania ilivyopiga hatua ya maendeleo katika sekta mbalimbali hususan kilimo na usimamizi wa madini.

“Kwa muda mrefu nimekuwa nikifuatalia maendeleo ya kilomo cha Tanzania kiasi cha kuweza kujitosheleza kwa chakula na pia kubakiwa na ziada ya kuuza kwa nchi za nje zenye uhitaji, nikasema sasa niwakati muafaka wa kutembelea Tanzania ili mimi pamoja na timu yangu tuweze kujifunza na kuanzisha ushirikiano katika sekta ya kilimo”. Alisema Gavana Katwe

Balozi Fatma Rajab akizungumza na Gavana huyo pamoja na ujumbe wake walipomtembelea Ofisini kwakwe jijini Dodoma ameleeza kuwa uhusiano wa kidiplomasia baina ya Tanzania na DRC umeendelea kuimarika daima hivyo niwakati muafaka kwa pande zote mbili kuendelea kuboresha mazingira ya ufanyaji biashara. 

“Tumekuwa tukishirikiana baina yetu, lakini pia kupitia Jumuiya ya Maendeleo Kusini mwa Afrika (SADC) ambako sote ni wanachama na sasa ninayo furaha kubwa pia kona tuko wote katika Jumuiya ya Afrika Mashariki. Tuendelea kuboresha mazingira ya biashara ili watu waendeshe shughuli zao kwa urahisi na uhuru zaidi na kuweza kujiongezea kipato chao binafsi lakini pia pato la Serikali za pande zote mbili”. Amesema Balozi Fatma Rajab.

Kwa upande wake Waziri wa Kilimo Mhe. Hussein Bashe alieleza kuwa Serikali ya Tanzania kupitia Wizara yake ipo tayari kushirikiana na Jimbo la Haut Katanga katika kuendeleza kilimo. Aliongeza kusema pamoja na Tanzania kuiuzia chakula DRC bado Tanzania haiiangali nchi hiyo kama soko bali kama mbia wa maendeleo. 

“Tupo tayari kushirikiana na DRC katika kilimo, tutafanya kila litakalowezekana kuwaongezea ujuzi ili kwa pamoja tuzalishe chakula cha kutosha; naamini Tanzania na DRC tukiungana kwa dhati katika kilimo tunaweza kuzalisha chakula kwa wingi zaidi na kuweza kulisha sehemu kubwa ya Dunia” Alisema Waziri Bashe

Waziri Biteko kwa upande wake amweleza Gavana Katwe kuwa Tanzania ipotayari kuendelea kushirikiana na DRC katika biashara ya madini. Aliendelea kueleza kuwa Tanzania ipo mikono wazi muda wote kupokea fursa za biashara za madini kutoa DRC. Aidha amemhakikishia Gavana Katwe kuwa Tanzania haina urasimu katika biashara na hiyo inawakaribisha wafanyabiashara kutoka DRC kuja nchini kuuza au kuongeza dhamani ya madini kwa kuwa uwezo huo kwa sasa Tanzania tunao.

Gavana Jacques Kyabula Katwe na ujumbe wake waliwasili nchini tarehe 22 Juni 2022 na kupokelewa na Mkurugenzi wa Bodi ya Nafaka na Mazao Mchanganyiko Dkt. Anselim Mosha. Wengine waliombatana na ujumbe huo kutoka nchini DRC ni Balozi wa Tanzania nchini humo Mhe. Saidi Juma Mshana na Konseli Mkuu wa Tanzania jijini Lubumbashi Selestine Kakele. 
Waziri wa Kilimo Mhe. Hussein Bashe (kushoto) na Gavana wa jimbo la Haut Katanga la Jamhuri ya Kidemokrasia ya Kongo (DRC) Mheshimiwa Jacques Kyabula Katwe (kulia) wakisalimiana alipotembelea Ofisi ya Wizara ya Kilimo jijini Dodoma
Gavana wa jimbo la Haut Katanga la DRC Mhe. Jacques Kyabula Katwe (kulia) akisalimiana na Mkurugenzi wa Bodi ya Nafaka na Mazao Mchanganyiko Dkt. Anselim Mosha (kushoto) alipowasili katika uwanja wa ndege wa jijini Dodoma.
Waziri wa Kilimo Mhe. Hussein Bashe na Gavana wa jimbo la Haut Katanga Mheshimiwa Jacques Kyabula Katwe na ujumbe wake wakiwa katika picha ya pamoja na Watendaji mbalimbali wa Serikali kwenye Ofisi za Wizara ya Kilimo jijini Dodoma.
Gavana wa jimbo la Haut Katanga la DRC akiwa katika picha pamoja na Viongozi na Watendaji mbalimbali wa Serikali ya Tanzania Bungeni jijini Dodoma.
Waziri wa Madini Mhe. Dotto Biteko na Gavana wa jimbo la Haut Katanga Mheshimiwa Jacques Kyabula Katwe na ujumbe wake wakiwa katika picha ya pamoja na Watendaji mbalimbali wa Serikali ya Tanzania jijini Dodoma
Gavana wa jimbo la Haut Katanga la Jamhuri ya Kidemokrasia ya Kongo (DRC) Mheshimiwa Jacques Kyabula Katwe (wa kwanza kulia) akiwa katika Bunge la Jamhuri ya Muungano wa Tanzania alipotembelea Bunge hilo tarehe 23 Juni 2022. 
Waziri wa Madini Mhe. Dotto Biteko (kulia) na Gavana wa jimbo la Haut Katanga la DRC Mheshimiwa Jacques Kyabula Katwe (kushoto) wakisalimiana alipotembelea Ofisi ya Wizara ya Madini jijini Dodoma
Gavana wa jimbo la Haut Katanga la Jamhuri ya Kidemokrasia ya Kongo (DRC) Mheshimiwa Jacques Kyabula Katwe akielezea jambo wakati wa mazungumzo baina yake Viongozi na Watendaji wa Wizara ya Madini

VACANCY ANNOUNCEMENT


 

BALOZI MULAMULA ATAKA MIGOGORO KATIKA NCHI ZA JUMUIYA YA MADOLA IMALIZWE

Waziri wa Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki, Balozi Liberata Mulamula amesema kuwa, licha ya wanachama wa Jumuiya ya Madola kufanya kazi nzuri katika kuimarisha misingi ya demokrasia, amani na utawala bora katika nchi zao, bado kuna changamoto nyingi zinazohitaji kutafutiwa ufumbuzi ili misingi hiyo ya maisha iweze kufanya kazi kwa ukamilifu wake.

Ametoa kauli hiyo leo tarehe 23 Juni 2022 jijini Kigali katika kikao cha Mawaziri wa Mambo ya Nje wa Jumuiya ya Madola kilichukuwa kinajadili masuala ya demokrasia, amani na utawala bora.

Waziri Mulamula alizitaja baadhi ya changamoto hizo na kusisitiza umuhimu wa familia ya Jumuiya ya Madola kuziangalia kwa makini na kuzitafutia ufumbuzi wa kudumu, kuwa ni pamoja na migogoro isiyoisha, ukosefu wa usalama na udhaifu wa vyombo vinavyosimamia masuala ya utawala wa sheria.

Balozi Mulamula katika maelezo yake alitambua jitihada zinazofanywa na jumuiya za kikanda na kimataifa za kutumia njia za kidiplomasia kuzuia migogoro na kuzisihi nchi za jumuiya hiyo kongwe kurejea katika misingi yake ya awali, ili kuhakikisha kuwa amani na utulivu vinatawala muda wote kwenye nchi hizo.

Aidha, Waziri Mulamula alitumia mkutano huo wa Mawaziri wa Mambo ya Nje, kuzishauri nchi wanachama kuangalia uwezekano wa kutumia taratibu za kujitathmini zinazotumika kwenye jumuiya nyingine za kujipima kiutawala bora.

Alitoa mifano ya taratibu hizo kuwa ni pamoja na Mpango wa Nchi za Afrika za Kujitathmini Kiutawala Bora (APRM); mpango wa hiyari wa nchi zinazotekeleza malengo ya Maendeleo Endelevu (SDGs) wa kujipima utekelezaji wa malengo hayo; mpango wa nchi wanachama wa Baraza la Umoja wa Mataifa la Haki za Binadamu wa kujitathmini kila baada ya kipindi fulani.

Aliwafahamisha Mawaziri wenzake kuwa, Tanzania imefanyiwa tathmini hivi karibuni na Baraza la Umoja wa Mataifa la Haki za Binadamu na kupitia tathmini hiyo, Tanzania ilipata fursa ya kueleza mazuri yaliyofanyika kuhusu utawala bora na haki za binadamu. Alisema pia kuwa nchi yake ilipata fursa ya kujifunza mazuri ya nchi nyingine kuhusu utawala bora.

Balozi Mulamula alitihitimisha hotuba yake kwa kuwakumbusha Mawaziri kuhusu programu zilizobuniwa na Sekretarieti ya Jumuiya ya Madola na umuhimu wa kuzihuisha na kuzipa nguvu. Progaramu hizo ni pamoja na misaada katika uchaguzi ikiwa ni pamoja na kuhamasisha nchi wanachama kuendesha chaguzi za huru na haki, kutoa misaada ya kiufundi katika uandaaji wa sera, misaada katika programu za mabadiliko ya sheria, kuunda taasisi imara za kitaifa za kusimamia masuala ya haki za binadamu na kuzijengea nchi uwezo wa kutoa haki bila upendeleo.


Waziri wa Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki, Balozi Liberata Mulamula akiwa katika kiti cha Tanzania wakati wa Mkutano wa Wakuu wa Nchi na Serikali wa Jumuiya ya Madola unaofanyika nchini Rwanda tarehe 20 hadi 25 Juni 2022.
Waziri wa Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki, Balozi Liberata Mulamula akisalimiana na Mawaziri wenzake wanaoshiriki katika mkutano wa Wakuu wa Nchi na Serikali wa Jumuiya ya Madola unaofanyika nchini Rwanda tarehe 20 hadi 25 Juni 2022.

Waziri wa Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki, Balozi Liberata Mulamula akiwa na makabrasha ya mkutano akilekea kwenye Kiti cha Tanzania kwa ajili ya kushiiki mkutano wa Mawaziri wa sJumuiya ya Madola unaofanyika nchini Rwanda.
Waziri wa Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki, Balozi Liberata Mulamula akihojiwa na mwandishi wa Kituo cha Runimga cha Channel 10, Bw. Ezekiel Mwamboko. Aliyemshikia kipaza sauti ni Mkurugenzi wa Kitengo cha Mawasiliano ya Serikali katika Wizara ya Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki,, Balozi Mindi Kasiga.
Waziri wa Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki, Balozi Liberata Mulamula akiwa katika picha ya pamoja na Mawaziri wa Mambo ya Nje wa nchi za Jumuiya ya Madola wanaoshiriki katika Mkutano wa Wakuu wa Nchi na Serikali wa jumuiya hiyo unaofanyika nchini Rwanda tarehe 20 hadi 25 Juni 2022.


 

Thursday, June 23, 2022

DKT. MPANGO AWASILI RWANDA KUSHIRIKI CHOGM

Makamu wa Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Mhe. Dkt. Philip Mpango amewasili nchini Rwanda tarehe 22 Juni 2022 kushiriki Mkutano wa Wakuu wa Nchi na Serikali wa nchi za Jumuiya ya Madola (Commonwealth Heads of Government Meeting-CHOGM) unaofanyika katika mji mkuu wa nchi hiyo, Kigali.

Makamu wa Rais anamwakilisha Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Mhe. Samia Suluhu Hassan kwenye mkutano huo ulioanza tarehe 20 Juni na utahitimishwa tarehe 25 Juni 2022.

Mhe. Makamu wa Rais, mbali ya kushiriki kwenye mkutano huo ameombwa pia miadi ya kufanya mazungumzo na viongozi mbalimbali wakiwemo Rais wa Namibia, Mhe. Hage Geingob; Waziri Mkuu wa Mauritius; Pravind Jugnauth; Waziri Mkuu wa Canada, Mhe. Justin Trudeau na Melinda Gates.

Inaelezwa kuwa miadi hiyo ni ishara ya dhahiri ya kuendelea kuimarika kwa diplomasia ya Tanzania duniani chini ya Serikali ya awamu ya sita inayoongozwa na Rais Samia. Hivyo, Mhe. Makamu wa Rais anatarajiwa kutumia miadi hiyo kusisitiza umuhimu wa kuimarisha uhusiano na ushirikiano baina ya pande mbili na hasa ushirikiano katika eneo la uwekezaji na biashara pamoja na utoaji wa huduma za kijamii kwa wananchi.

Aidha, Waziri wa Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki, Balozi Liberata Mulamula naye yupo nchini humo kushiriki Mkutano huo katika ngazi ya Mawaziri tarehe 23 Juni 2022. Kama ilivyo kwa Makamu wa Rais, Balozi Mulamula ameombwa miadi ya kufanya mazungumzo na Mawaziri wa mambo ya nje wa nchi za India, Zambia, Botswana, Eswatini, Singapore na mke wa Waziri Mkuu wa zamani wa Uingereza, Mhe. Tony Blair, Bibi Cherie Blair ambaye ni mwanzilishi wa Cherie Foundation.

Wakati huo huo, mikutano ya utangalizi ya mkutano huo, inaendelea ambapo tarehe 20 hadi 23 Juni 2022 ilifanyika mikutano ya jukwaa la vijana, jukwaa la wanawake na jukwaa la biashara. Tanzania ilishiriki katika majukwaa yote hayo

Wakati wa mkutano wa jukwaa la biashara, washiriki pamoja na mambo mengine, walijadili namna bora ya kufanya biashara huku dunia ikiwa bado inakabiliwa na janga la ugonjwa wa Corona na athari za vita kati ya Urusi na Ukraine.

Ujumbe wa Tanzaia katika mkutano huo uliongozwa na Naibu Katibu Mkuu wa Viwanda na Biashara katika Wizara ya Uwekezaji, Viwanda na Biashara, Dkt. Hashil Abdallah ambaye alieleza hatua zinazochukuliwa na Serikali ya awamu ya sita za kuboresha mazingira ya biashara na fursa lukuki za uwekezaji zinazopatikana nchini.

Kwa upande wa mkutano wa jukwaa la vijana ambapo Tanzania iliwakilishwa na vijana saba, ulisistizwa umuhimu wa kuwaendeleza vijana. Ilielezwa kuwa endapo nchi za Jumuiya ya Madola zinahitaji kufikia maendeleo ya kweli, hazina budi kuwekeza kwa vijana kwa sababu katika nchi hizo vijana ni zaidi ya asilimia 60. 

 Kuhusu mkutano wa jukwaa la wanawake, ulisisitizwa umuhimu wa kumuendeleza mwanamke ikiwa ni pamoja na kumpatia elimu ya kumiliki, kukuza na kufanya biashara, kuweka usawa wa kijinsia na kukomesha vitendo vyote vya unyanyasaji dhidi ya wanawake.

Waziri wa Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki, Balozi Liberata Mulamula akitoa maelezo kwa  Makamu wa Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Mhe. Dkt. Philip Mpango kuhusu maandalizi ya ushiriki wa Tanzania katika  mkutano wa Wakuu wa Nchi na Serikali wa Jumuiya ya Madola unaofanyika jijini Kigali, Rwanda tarehe 20 hadi 25 Juni 2022.

Waziri wa Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki, Balozi Liberata Mulamula akifafanua jambo kwa Makamu wa Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Mhe. Dkt. Philip Mpango kuhusu ushiriki wa Tanzania katika mkutano wa Wakuu wa Nchi na Serikali wa Jumuiya ya Madola unaofanyika jijini Kigali, Rwanda tarehe 20 hadi 25 Juni 2022.

Katibu Mkuu wa Wizara ya Mambo ya Nje na Ushikiano wa Afrika Mashariki, Balozi Joseph Sokoine akitoa maelezo kwa Makamu wa Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Mhe. Dkt. Philip Mpango ambaye anamwakilisha Rais Samia Suluhu Hassan katika Mkutano wa 26 wa Wakuu wa Nchi na Serikali wa Jumuiya ya Madola unaofanyika jijini Kigali, Rwanda tarehe 20 hadi 25 Juni 2022.
Balozi wa Tanzania nchini Uingereza, Mhe.Dkt. Asha-Rose Migiro akifafanua jambo kwa Makamu wa Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Mhe. Dkt. Philip Mpango kuhusu masuala ya CHOGM


Mkurugenzi wa Ushirikiano wa Kimataifa katika Wizara ya Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki, Balozi Robert Kahendaguza akitoa utaratibu wa namna ya mikutano ya CHOGM itakavyoendeshwa kwa Makamu wa Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Mhe. Dkt. Philip Mpango.

Afisa Dawati katika Wizara ya Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki, Bi. Salma Rajab akifafanua jambo kwa Makamu wa Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Mhe. Dkt. Philip Mpango.

 Makamu wa Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Mhe. Dkt. Philip Mpango akiwa katika kikao cha maandalizi na ujumbe wake kabla ya kushiriki kwenye mkutano wa Wakuu wa Nchi na Serikali wa Jumuiya ya Madola unaofanyika jijini Kigali, Rwanda tarehe 20 hadi 25 Juni 2022.

Makamu wa Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Mhe. Dkt. Philip Mpango akiongea na Mkurugenzi wa Kitengo cha Mawasiliano ya Serikali katika Wizara ya Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki, Balozi Mindi Kasiga.

Makamu wa Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Mhe. Dkt. Philip Mpango akiongea na baadhi ya viongozi wa Serikali wanaoshiriki Mkutano wa 26 wa Wakuu wa Nchi na Serikali wa Jumuiya ya Madola unaofanyika jijini Kigali, Rwanda tarehe 20 hadi 25 Juni 2022.

 

Tuesday, June 21, 2022

SERIKALI YASISITIZA KUZINGATIA SHERIA ZA KIMATAIFA, KUHESHIMU HAKI ZA BINADAMU

Na Waandishi wetu, Dar

Serikali kupitia Wizara ya Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki imeihakikishia Jumuiya ya Kimataifa nchini kuwa inazingatia na kutekeleza sheria za kimataifa za haki za binadamu huku ikiendelea kulinda uhifadhi wa eneo la Ngorongoro.

Kauli hiyo imetolewa na Waziri wa Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki, Balozi Liberata Mulamula (Mb) leo Jijini Dar es Salaam alipozungumza na Mabalozi na Wakuu wa Mashirika ya Kimataifa wanaoziwakilisha nchi zao hapa nchini kuwaelezea mpango wa Serikali katika kulinda na kuhifadhi eneo la Ngorongoro.

“Napenda kuchukua nafasi hii kuuhakikishia umma wa Watanzania na Jumuiya ya Kimataifa kuwa Tanzania inazingatia na kutekeleza sheria za kimataifa za haki za binadamu na hakuna nanma itaendesha mipango yake kwa kukiuka sheria za haki za binadamu”, alisema Balozi Mulamula.

Balozi Mulamula ameongeza kuwa Tanzania kupitia Wizara ya Maliasili na Utalii inatekeleza mpango wa kulinda na kuhifadhi eneo la Ngorongoro nchini kwa wananchi kuridhia kuhama kwa hiari yao na kwamba hakuna aliyeondolewa katika eneo hilo kwa nguvu kama inavyoelezwa.

“Tanzania siku zote italinda watu wake, maliasili zake na mipaka yake kwa kuzingatia sheria za kimataifa,” alisema Balozi Mulamula.

Akizungumza katika kikao hicho maalum kwa ajili ya kuielezea Jumuiya ya Kimataifa iliyopo nchini, Waziri wa Katiba na Sheria Dkt. Damas Ndumbaro (Mb) amesema kinachoendelea katika eneo la Ngorongoro kwa wakati huu ni uhamaji wa hiari wa wananchi waliokuwa ndani ya eneo la Ngorongoro na sio kwamba kuna uhamishaji wa nguvu unaofanywa na Serikali.

“Serikali imekuja na mpango wa kulinda eneo la Ngorongoro, imechukua miaka 20 kuandaa na kuratibu mpango huu, ambao unatekelezwa sasa na hakuna uhamishaji wa nguvu unaofanywa kwa wanachi kama inavyodaiwa, wananchi husika wameshirikishwa vya kutosha na ndio maana wamekubali na kuamua kuhama kwa hiari wenyewe,” alisema Dkt. Ndumbaro.

Amesema Katiba ya Tanzania inasema watu wote ni sawa na kila mtu ana haki ya kuishi popote na kuongeza kuwa Serikali itaendelea kulinda na kuheshimu wananchi wake wote bila ya kujali rangi, kabila au dini zao.

Amesema wananchi wamepewa umiliki kwa miaka kadhaa na endapo itaonekana kuna haja ya kuichaukua ardhi hiyo anayeimiliki hulipwa fidia na kupewa ardhi katika eneo lingine na kuongeza kuwa wananchi wanaohama kwa hiari yao kutoka katika hifadhi ya Ngorongoro wanalipwa fidia na kupatiwa nyumba za makazi, maeneo yenye huduma za kijamii na ardhi kwa ajili ya malisho ya mifugo. 

Naye Naibu Waziri wa Maliasili na Utalii Mhe. Mary Masanja (Mb) amesema kwamba katika wilaya ya Ngorongoro kuna maeneo mawili ambayo yamekuwa yakizua mjadala ambayo ni eneo la hifadhi la Ngorongoro ambalo ni urithi wa dunia na Pori Tengefu la Loliondo.

Amesema Serikali imechukua uamuzi wa kutekeleza mpango huo kutokana na changamoto kadhaa ambazo zinatishia uhifadhi wa eneo la Ngorongoro na kuongeza kuwa uhamaji wa hiari unaofanyika katika eneo la Ngorongoro una lengo la kuendelea kuhifadhi eneo hilo kwa manufaa ya vizazi vya sasa na vizazi vijavyo.

Akizunguma katika kikao hicho Mkuu wa Mkoa wa Arusha Mhe. John Mongela amewahahakikishia wanadiplomasia nchini kuwa zoezi hilo lilihusisha wananchi wa jumuiya zote waliokuwa wakiishi katika eneo la Hifadhi ya Ngorongoro na kuahidi kuwa majadiliano bado yanaendelea ili kuhakikisha wananchi wote wanakuwa na uelewa wa pamoja katika suala hilo na hivyo kufanikisha utekelezaji wa azma ya uhifadhi wa hifadhi ya Ngorongoro.

Mkutano huo uliohusisha viongozi waandamizi wa Serikali kutoka Wizara za mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki, Maliasili na Utalii, Katiba na Sheria pamoja na Wakuu wa Mikoa ya Arusha na Tanga.

Mkutano huo ulilenga kuwafahamisha wanadiplomasia walioko nchini juu ya utekelezaji wa mpango wa Serikali wa kuhama kwa hiari kunakofanywa na wananchi waliokuwa na makazi ndani ya Hifadhi ya Ngorongoro na hivyo kuondoa sintofahamu iliyokuwepo kuwa wananchi hao wanahamishwa kwa nguvu na serikali na hivyo kukiuka haki za binadamu.

Waziri wa Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki, Balozi Liberata Mulamula akizungumza na Mabalozi na Wakuu wa Mashirika ya Kimataifa wanaoziwakilisha nchi zao hapa nchini (hawapo pichani) kuwaelezea mpango wa Serikali katika kulinda na kuhifadhi eneo la Ngorongoro

Waziri wa Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki, Balozi Liberata Mulamula akizungumza na Mabalozi na Wakuu wa Mashirika ya Kimataifa wanaoziwakilisha nchi zao hapa nchini kuwaelezea mpango wa Serikali katika kulinda na kuhifadhi eneo la Ngorongoro

Waziri wa Katiba na Sheria Dkt. Damas Ndumbaro akizungumza katika kikao na Mabalozi na Wakuu wa Mashirika ya Kimataifa wanaoziwakilisha nchi zao hapa nchini (hawapo pichani) kuwaelezea mpango wa Serikali katika kulinda na kuhifadhi eneo la Ngorongoro

Naibu Waziri wa Maliasili na Utalii Mhe. Mary Masanja akizungumza na Mabalozi na Wakuu wa Mashirika ya Kimataifa wanaoziwakilisha nchi zao hapa nchini (hawapo pichani) kuwaelezea mpango wa Serikali katika kulinda na kuhifadhi eneo la Ngorongoro

Naibu katibu Mkuu Wizara ya Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki, Balozi Fatma Rajab akimkaribisha Waziri wa mambo ya Nje kuzungumza na Mabalozi na Wakuu wa Mashirika ya Kimataifa wanaoziwakilisha nchi zao hapa nchini (hawapo pichani) kuwaelezea mpango wa Serikali katika kulinda na kuhifadhi eneo la Ngorongoro

Balozi wa Visiwa vya Comoro Nchini, Dkt. Ahmada El Badaoui Mohammed  akitoa salamu za shukrani baada ya kikao kati ya Serikali na Mabalozi na Wakuu wa Mashirika ya Kimataifa wanaoziwakilisha nchi zao hapa nchini (hawapo pichani)

Mkurugenzi wa Mawasiliano Serikalini, Wizara ya Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki, Balozi Mindi Kasiga akiwakaribisha Mabalozi na Wakuu wa Mashirika ya Kimataifa katika mkutano

Mkurugenzi wa Diaspora, Wizara ya Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki, Balozi James Bwana akifuatilia mkutano kati ya Serikali na Mabalozi na Wakuu wa Mashirika ya Kimataifa

Balozi wa Ufaransa Nchini,  Mhe. Nabil Hajlaoui akichangia katika kikao kati ya Serikali na Mabalozi na Wakuu wa Mashirika ya Kimataifa wanaoziwakilisha nchi zao hapa nchini (hawapo pichani) kuwaelezea mpango wa Serikali katika kulinda na kuhifadhi eneo la Ngorongoro

Baadhi ya Mabalozi katika picha ya pamoja na meza kuu baada ya kikao kati ya Serikali na Mabalozi na Wakuu wa Mashirika ya Kimataifa wanaoziwakilisha nchi zao hapa nchini 



Wakuu wa Nchi za Jumuiya ya Madola kukutana Rwanda

Na Mwandishi Maalum Kigali, Rwanda

Mkutano wa Wakuu wa Nchi na Serikali wa Jumuiya ya Madola hatimaye unafanyika jijini Kigali, Rwanda baada ya kuahirishwa mara mbili (2020 na 2021) kwa sababu ya ugonjwa wa Corona.

Mkutano huo unaofanyika kuanzia tarehe 20 hadi 25 Juni 2022 umegawanywa katika makundi mbalimbali kama vile ya vijana, wanawake, wafanyabiashara, Mawaziri wa Mambo ya Nje, Wakuu wa Nchi pamoja na matukio ya pembezoni ambayo kwa pamoja mijadala yake inajikita katika maeneo matano.

Maeneo hayo ni utawala bora, utawala wa sheria, haki za binadamu; vijana, afya, teknolojia na uvumbuzi; maendeleo endelevu na mapambano dhidi ya mabadiliko ya tabianchi.

Mkutano huo unaofanyika kwa kaulimbiu “Kufikia Mustakabali wa Pamoja: Kuunganisha, Kufanya uvumbuzi, Kufanya mabadiliko” (Delivering a Common Future: Connecting, Innovating, Transforming) umejipanga kujadili na kutafutia ufumbuzi wa changamoto zinazozikabili nchi wanachama wa Jumuiya ya Madola ili kufikia maendeleo ya kweli katika nyanja zote.

Tanzania inashiriki kikamilifu katika mkutano huo na kimsingi masuala yanayojadiliwa yanakwenda sanjari na vipaumbele vya Serikali ya awamu ya sita inayoongozwa na Rais Samia Suluhu Hassan.

Ikumbukwe, Rais Samia tangu aingie madarakani, Serikali yake imejipambanua katika kuheshimu haki za binadamu na kuzingatia masuala ya utawala wa sheria na demokrasia. Serikali ya awamu ya sita pia inafanya jitihada mbalimbali zenye lengo la kuyawezesha makundi maalum ya wanawake, vijana na wazee kiuchumi pamoja na kuhakikisha kuwa huduma za afya zinaboreshwa na zinapatikana kwa wananchi wote.

Aidha, mageuzi makubwa ya kiuchumi yameshuhudiwa katika Serikali ya awamu ya sita na uwekezaji mkubwa katika elimu na elimu ya ufundi unaendelea kufanyika` kwa lengo la kuchochea ubunifu bila kusahau mikakati madhubuti ya kukabiliana na madiliko ya tabianchi.


: Katibu Mkuu,Ofisi ya Rais-Ikulu, Dkt. Moses Kusiluka (katikati waliokaa), Balozi wa Tanzania nchini, Uingereza, Mhe. Dkt. Asha-Rose Migiro na Mkurugenzi wa  Idara ya Ushirikiano wa Kimataifa katika Wizara ya Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki, Balozi, Robert Kahendaguza wakiwa katika picha ya pamoja na vijana kutoka Tanzania wanaoshiriki Jukwaa la Vijana
kwenye mkutano wa Wakuu wa Nchi na Serikali wa Jumuiya ya Madola unaofanyika Kigali, Rwanda tarehe 20 hadi 25 Juni 2022.


Balozi wa Tanzania nchini Uingereza, Mhe. Dkt. Asha-Rose Migiro (mwenye kilemba) akiongea jambo wakati vijana kutoka Tanzania wanaoshiriki Jukwaa la Vijana katika Mkutano wa Wakuu wa Nchi na Serikali wa Jumuiya ya Madola walipotembelea Ofisi za Balozi wa Tanzania nchini Rwanda. kulia kwa Balozi Migiro ni Katibu Mkuu,Ofisi ya Rais-Ikulu, Dkt. Moses Kusiluka na anayefuatia     ni Mkurugenzi wa  Idara ya Ushirikiano wa Kimataifa katika Wizara ya Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki, Balozi, Robert Kahendaguza.

Balozi wa Tanzania nchini Uingereza, Mhe. Dkt. Asha-Rose Migiro akimsikiliza mmoja wa vijana kutoka Tanzania wanaoshiriki Jukwaa la Vijana katika Mkutano wa Wakuu wa Nchi na Serikali wa Jumuiya ya Madola

Katibu Mkuu wa Wizara ya Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki, Balozi Joseph Sokoine, Katibu wa Baraza la Mapinduzi na Katibu Mkuu Kiongozi wa Serikali ya Zanzibar, Mhandisi Zena Said na Balozi wa Tanzania nchini Uingereza, Mhe. Dkt. Asha-Rose Migiro wakiwa katika kikao cha maandalizi ya Mkutano wa Wakuu wa Nchi na Serikali wa Jumuiya ya Madola unaofanyika Kigali, Rwanda tarehe 20 hadi 25 Juni 2022.

Viongozi wa Tanzania wakiwa katika kikao cha maandalizi ya Mkutano wa Wakuu wa Nchi na Serikali wa Jumuiya ya Madola unaofanyika Kigali, Rwanda tarehe 20 hadi 25 Juni 2022.


Balozi wa Tanzania nchini Rwanda, Mhe. Meja Jenerari Richard Makanzo akiwa katika picha ya pamoja na vijana kutoka Tanzania wanaoshiriki Jukwaa la Vijana
kwenye mkutano wa Wakuu wa Nchi na Serikali wa Jumuiya ya Madola unaofanyika Kigali, Rwanda tarehe 20 hadi 25 Juni 2022.

 

Monday, June 20, 2022

WAZIRI MULAMULA APOKEA NAKALA ZA HATI ZA UTAMBULISHO BALOZI WA JAPAN

Na Mwandishi wetu, Dar

Waziri wa Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki Balozi Liberata Mulamula (Mb) amepokea nakala za Hati za Utambulisho kutoka kwa Balozi Mteule wa Japan nchini, Mhe. Misawa Yasushi leo katika Ofisi Ndogo za Wizara Jijini Dar es Salaam

Akipokea nakala ya hati hizo, Balozi Mulamula amemhakikishia Balozi huyo mteule ushirikiano wakati wote katika utekelezaji wa majukumu yake hapa nchini.

“Nakuhakikishia ushirikiano kutoka Serikalini wakati wote, naamini tutaendelea kushirikiana katika kukuza na kuendeleza ushirikiano baina yetu kwa masahi ya pande zote mbili kwani uhusiano wa Tanzania na Japan ni wa muda mrefu na umekuwa imara katika kipindi chote,” amesema Balozi Mulamula

Naye Balozi Mteule wa Japan nchini Mhe. Misawa Yasushi amesema atahakikisha uhusiano kati ya Tanzania na Japan unaimarika zaidi na kukua kwa ushirikiano baina ya nchi hizi kupitia nyanja za biashara na uwekezaji na hivyo kunufaisha pande zote mbili. 

“Tanzania na Japan zitaendelea kushirikiana kufanya biashara na uwekezaji kwa maslahi ya nchi zote mbili,” amesema Balozi Yasushi.

Katika tukio jingine, Balozi Mulamula amekutana kwa mazungumzo na Mkurugenzi kutoka Wizara ya Mambo ya Nje wa China anayeshughulikia masuala ya Afrika, Bw. Wu Peng katika Ofisi Ndogo za Wizara Jijini Dar es Salaam

Pamoja na mambo mengine, Waziri Mulamula na mgeni wake, walijadili namna ya kuendelea kuimarisha maeneo ya ushirikiano katika sekta za afya, elimu, bishara na uwekezaji, nishati, miundombinu na usafirishaji.

Bw. Peng ameahidi kuwa China itaendelea kushirikiana na Tanzania na kuhakikisha inafanikisha mipango yake ya maendeleo.

Waziri wa Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki Balozi Liberata Mulamula akipokea Nakala ya Hati za Utambulisho kutoka kwa Balozi Mteule wa Japan nchini Mhe. Misawa Yasushi leo katika Ofisi Ndogo za Wizara Jijini Dar es Salaam

Waziri wa Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki, Balozi Liberata Mulamula akizungumza na Balozi Mteule wa Japan nchini Mhe. Misawa Yasushi katika Ofisi Ndogo za Wizara Jijini Dar es Salaam

Mkuu wa Itifaki Wizara ya Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki, Balozi Yusuph Mdolwa (katikati), Mkurugenzi wa Idara ya Asia na Australasia Wizara ya Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki, Balozi Caesar Waitara pamoja 
Mkurugenzi wa Mawasiliano Serikalini Wizara ya Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki, Balozi Mindi Kasiga wakifuatilia uwasilishaji wa nakala za hati za utambulisho za Balozi mteule wa Japan nchini Mhe. Misawa Yasushi


Maafisa waandamizi kutoka Wizara ya Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki pamoja na Afisa kutoka Ubalozi wa Japan nchini wakifuatilia uwasilishaji wa nakala za Hati za Utambulisho za Balozi mteule wa Japan nchini Mhe. Misawa Yasushi

Waziri wa Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki Balozi Liberata Mulamula akimueleza jambo Mkurugenzi kutoka Wizara ya Mambo ya Nje wa China anayeshughulikia masuala ya Afrika, Bw. Wu Peng katika Ofisi Ndogo za Wizara Jijini Dar es Salaam

Mkurugenzi kutoka Wizara ya Mambo ya Nje wa China anayeshughulikia masuala ya Afrika, Bw. Wu Peng akizungumza na Waziri wa Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki Balozi Liberata Mulamula (hayupo pichani) katika Ofisi Ndogo za Wizara Jijini Dar es Salaam

Picha ya pamoja 



   


Saturday, June 18, 2022

WAZIRI MULAMULA AZUNGUMZA NA UONGOZI WA CHAMA CHA WAFANYABIASHARA WA NORWAY NA AFRIKA NA UONGOZI WA MFUKO WA MAENDELEO WA NORWAY


Waziri wa Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki, Mhe. Balozi Liberata Mulamula ametembelea ofisi za Makao Makuu ya Mfuko wa Maendeleo wa Norway (NORFUND) na kuzungumza na uongozi wa mfuko huo pamoja na uongozi wa Chama cha ushirikiano wa Wafanyabiashara kati ya Norway na Nchi za Afrika (NABA) tarehe 17 Juni 2022 jijini Oslo, Norway.
Katika ziara yake nchini Norway Waziri Mulamula amekutana na taasisi hizo za maendeleo ili kuona namna ya kuboresha sekta za ushirikiano zilizopo kati ya Norway na Tanzania na kuleta manufaa kiuchumi kwa pande zote mbili.



Sehemu ya uongozi wa Chama cha ushirikiano wa Wafanyabiashara kati ya Norway na Nchi za Afrika na Mfuko wa Maendeleo wa Norway wakifatilia mazungumzo ambapo waneonesha nia ya kuongeza maeneo ya ushirikiano ili kuleta tija zaidi katika soko la kimataifa na kuboresha miundombinu wenzeshi.

Mhe. Waziri Mulamula akipokelewa na viongozi wa Chama cha ushirikiano wa Wafanyabiashara kati ya Norway na Nchi za Afrika na Mfuko wa Maendeleo wa Norway.

Picha ya pamoja na viongozi wa NABA na NORFUND.

Sehemu ya Ujumbe kutoka Wizara ya Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki wakifuatilia mazungumzo, kutoka kushoto ni Bi. Tunsume Mwangolombe na wa pili kushoto ni Bw. Seif Kamtunda.

Mazungumzo yakiendelea, Kutoka kulia Mkuu wa Kitengo cha Mawasiliano Wizara ya Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki, Balozi Mindi Kasiga na Afisa Mambo ya Nje Bi. Kisa Doris Mwaseba.

Picha ya pamoja Mhe. Waziri Mulamula na Mkurugenzi wa NABA, Bw. Eivind Fjeldstad (kulia) na Mkurugenzi wa NORFUND Bw. Tellef Thorleifsson (kushoto).