Friday, December 16, 2022
Thursday, December 15, 2022
BALOZI SIRRO AWASILISHA HATI ZA UTAMBULISHO KWA RAIS WA ZIMBABWE
Balozi wa Tanzania nchini Zimbabwe, Mhe. Simon Sirro amewasilisha Hati za Utambulisho kwa Rais wa Jamhuri ya Zimbabwe, Mhe. Emmerson Mnangagwa, Ikulu Zimbabwe.
Julai 20, 2022 Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mhe. Dkt. Samia Suluhu Hassan alimteua aliyekuwa Mkuu wa Jeshi la Polisi nchini IGP Simon Sirro kuwa Balozi wa Tanzania nchini Zimbabwe.
Balozi wa Tanzania nchini Zimbabwe, Mhe. Simon Sirro akiwasilisha Hati za Utambulisho kwa Rais wa Jamhuri ya Zimbabwe, Mhe. Emmerson Mnangagwa, Ikulu Zimbabwe |
Rais wa Jamhuri ya Zimbabwe, Mhe. Emmerson Mnangagwa akisalimiana na Balozi wa Tanzania nchini Zimbabwe, Mhe. Simon Sirro Ikulu Zimbabwe baada ya kuwasilisha Hati za Utambulisho |
Picha ya pamoja |
Tuesday, December 13, 2022
AFRIKA MASHARIKI WAHIMIZWA KUTUMIA BIDHAA ZA NDANI
Balozi wa Tanzania nchini Uganda Mhe. Aziz Mlima akitoa salaam kwa wajasiriamali wakati wa maadhimisho ya SIKU YA TANZANIA kwenye maonesho ya 22 ya Juakali ya Jumuiya ya Afrika Mashariki yanayofanyika jijini Kampala, Uganda |
Wajiriamali wa Tanzania wakiwa kwenye maonesho ya mavazi yaliyofanyika kwenye maonesho ya 22 ya Juakali yanayoendelea jijini Kampala, Uganda |
Monday, December 12, 2022
UBUNIFU, UBORA WA BIDHAA ZA WAJASIRIAMALI WATIA FORA MAONESHO YA JUAKALI
Mjasiriamali wa Tanzania alikimwonjesha mvinyo mteja kwenye maonesho ya 22 ya Jumuiya ya Afrika Mashariki ya Wajasiriamali Wadogo na Wakati maarufu Juakali, yanayoendelea jijini Kampala, Uganda. |
Tanzania na Oman Zainisha Maeneo ya Kushirikiana
Tanzania
na Oman zimedhamiria kuchukua jitihada za makusudi kuimarisha ushikiano wa
kiuchumi baina ya nchi hizo zenye uhusiano madhubuti wa kihistoria.
Hayo
yamebainishwa na Mawaziri wa Mambo ya Nje wa nchi hizo, Mhe. Dkt. Stergomena L.
Tax (Mb) na mwenyeji wake, Mhe. Sayyid Badr Al Busaidi
walipokutana pembezoni mwa Mkutano wa Pili wa Tume ya Kudumu ya Pamoja ya Ushirikiano (JPC) kati ya
Tanzania na Oman uliohitimishwa jijini Muscat tarehe
11 Desemba 2022.
Katika
hotuba zao za kufunga Mkutano wa Pili wa JPC, Viongozi hao walieleza kuwa nchi
zao zimekubaliana kuanzisha Kamati ya Pamoja ya Kufuatilia Utekelezaji wa
Maazimio ya Mkutano huo ili kuwa na tija kwa pande zote mbili.
Kamati
hiyo pamoja na mambo mengine, itahakikisha kuwa rasimu zote za mikataba na makubaliano zinakamilika na kutiwa saini ili
kujenga mazingira ya kisheria ya kuimarisha uhusiano wa kindugu uliopo baina ya
Tanzania na Oman.
Maeneo
yaliyojadiliwa na ujumbe wa nchi hizo na kuwekewa mikakati ya utekelezaji ni
pamoja na kilimo, elimu, nishati, biashara, uwekezaji, mawasiliano, mifugo na
usafirishaji. Maeneo mengine ni uvuvi, utalii, michezo, utamaduni, madini,
uhamiaji, fedha na udhibiti wa majanga ya moto.
Mkutano wa JPC kati ya Tanzania na Oman ulihudhuriwa na viongozi mbalimbali wa Serikali akiwemo Waziri wa Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki, Mhe. Dkt. Stergomena L. Tax; Naibu Waziri wa Nishati, Mhe. Stephen Byabato; Katibu Mkuu, Ofisi ya Waziri Mkuu, Kazi, Ajira, Vijana na Wenye Ulemavu, Prof. Jamal Katundu; Naibu Katibu Mkuu, Wizara ya Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki, Balozi Fatma Rajab; Naibu Katibu Mkuu, Wizara ya Nishati, Ndugu Kheri Mahimbali; na Naibu Katibu Mkuu Wizara ya Elimu na Mafunzo ya Amali, Zanzibar, Ndugu Mwanahamisi Adam.
Meza Kuu wakati wa Mkutano wa Pili wa Tume ya Kudumu ya Pamoja ya Ushirikiano (JPC) kati ya Tanzania na Oman uliohitimishwa jijini Muscat tarehe 11 Desemba 2022. |
Sunday, December 11, 2022
ZAIDI YA WAJASIRIAMALI 300 WASHIRIKI MAONESHO YA JUAKALI UGANDA
Sehemu ya wajasiriamali wa Tanzania wakipanga bidhaa zao kweye maonesho 22 ya Juakali yanayoendelea katika viwanja vya Uhuru vya Kololo jijini Kampala, Uganda |
Thursday, December 8, 2022
Wednesday, December 7, 2022
MHE. DKT. TAX AWAKARIBISHA WAWEKEZAJI KUTOKA VIETNAM
Waziri wa Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki, Mhe. Dkt. Stergomena Tax amewakaribisha wawekezaji kutoka Vietnam kuja nchini kuwekeza katika sekta ya Teknolojia ya Habari na Mawasiliano pamoja na Kilimo.
Mhe. Waziri Tax ameyasema hayo alipokutana kwa mazungumzo na Waziri wa Habari na Mawasiliano wa Vietnam na Mjumbe wa Kamati Kuu ya Chama cha Kikomunisti cha nchi hiyo Mhe. Nguyen Manh Hung alipomtembelea Ofisini kwake jijini Dodoma hivi karibuni.
Mhe. Dkt Tax amesema Tanzania inathamini ushirikiano kati yake na Vietnam ambayo imepiga hatua kubwa katika maendeleo ya teknolojia ya habari na mawasiliano na kwamba kupitia ushirikiano huo Tanzania imejipanga kunufaka katika sekta hiyo na nyingine zenye manufaa kati ya nchi hizi mbili.
Ameongeza kusema nchi hiyo ambayo tayari imewekeza kwenye sekta ya Mawasiliano hapa nchini kupitia Kampuni ya Simu ya Halotel, bado inakaribishwa kuwekeza zaidi katika sekta hiyo hususan kwenye miundombinu ya kidijiti na kwamba Serikali ya Awamu ya Sita chini ya Uongozi wa Mhe. Samia Suluhu Hassan, Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania itaendelea kuboresha mazingira ya biashara na uwekezaji ili kuhakikisha wawekezaji wanafanikisha malengo yao lakini pia Taifa linanufaika kupitia uwekezaji.
“Tanzania inaendelea kujiimarisha katika Sekta ya Teknolojia ya Habari na Mawasiliano kwa kushirikiana na wadau wa ndani na nje ya nchi. Kama ulivyosema Mhe. Waziri, Vietnam ni miongoni mwa nchi 10 duniani zilizopiga hatua kubwa katika sekta hiyo, naendelea kuhimiza wawekezaji zaidi kutoka nchini kwako kuja kuwekeza kwenye sekta hiyo lakini pia na sekta nyingine kama Kilimo hususan kile cha biashara na usindikaji wa mazao ya kilimo” alisema Dkt. Tax.
Kwa upande wake, Mhe. Nguyen Manh Hung amepongeza jitihada mbalimbali zinazofanywa na Serikali ya Tanzania katika kuboresha mazingira ya biashara na uwekezaji na kwamba nchi yake itaendelea kushirikiana na Tanzania katika masuala mbalimbali yanachangia maendeleo ya wananchi.
Akizungumzia uwekezaji kupitia kampuni ya Viettel ambayo ni kampuni mama ya mtandao wa simu wa Halotel hapa nchini, amesema nchi yake imewekeza mtaji wa takribani Dola bilioni moja katika miundombinu ya mtandao huo ambao umejikita kuwahudumia zaidi wananchi wa vijijini na kwamba hadi sasa Mtandao huo umeajiri watanzania 1,000.
Sehemu ya ujumbe ulioambatana na Mhe. Mahn Hung akiwemo Balozi wa Vietnam nchini Mhe. Nguyen Nam Tien (kulia) wakifuatilia mazungumzo |
Sehemu ya ujumbe wa Tanzania ulioshiriki mazungumzo. Kushoto ni Bw. John Kambona, Kaimu Mkurugenzi wa Idara ya Asia na Australasia katika Wizara ya Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki |