Wednesday, September 10, 2014

Rais Kikwete amwapisha Balozi mpya wa Tanzania nchini Rwanda

Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Mhe. Jakaya Mrisho Kikwete akimwapisha Balozi mpya wa Tanzania nchini Rwanda, Mhe. Ali Siwa. Hafla hiyo ilifanyika, Ikulu, Dar es Salaam tarehe 09 Septemba, 2014.
Katibu Mkuu wa Wizara ya Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Kimataifa, Bw. John Haule (wa kwanza mstari wa mbele) pamoja na wageni waalikwa  wakifuatilia tukio la kuapishwa kwa Balozi mpya wa Tanzania nchini Rwanda.
Balozi Siwa akisaini Hati ya Kiapo mbele ya Mhe. Rais Kikwete
 Mhe. Rais Kikwete akimkabidhi vitendea kazi, Balozi Siwa.
Mhe. Rais Kikwete akimpongeza Balozi Siwa mara baada ya kiapo.
Mhe. Rais Kikwete katika picha ya pamoja na Balozi Siwa. 
Mhe. Rais Kikwete na Balozi Siwa katika picha ya pamoja na Makamu wa Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Mhe. Dkt. Mohammed Gharib Bilal, Waziri  wa Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Kimataifa, Mhe. Bernard K. Membe (Mb.) na Katibu Mkuu Kiongozi, Balozi Ombeni Sefue.
Mhe. Rais Kikwete  katika picha ya pamoja na Familia ya Balozi Siwa.

No comments:

Post a Comment

Note: Only a member of this blog may post a comment.