Thursday, March 15, 2018

Katibu Mkuu wa Mambo ya Nje atembelea Ofisi za Kamisheni ya Kiswahili ya EAC Zanzibar

Katibu Mkuu wa Wizara ya Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki, Prof. Adolf Mkenda (katikati upande wa kulia), akizungumza na Prof. Kenneth Simala (kushoto), Katibu Mtendaji wa Kamisheni ya Kiswahili ya Afrika Mashariki.  Pamoja na mambo mengine Prof. Simala alimkabidhi Prof. Mkenda Mpango Mkakati wa Kamisheni hiyo wa mwaka 2017/2022. Kamisheni hiyo ina lengo la kukuza na kutangaza Lugha ya Kiswahili kwa nchi za Afrika Mashariki. Prof. Mkenda alitembelea Ofisi za Kamisheni hiyo zilizopo Zanzibar wakati wa ziara yake ya kujitambulisha kwenye Serikali ya Mapinduzi Zanzibar kufuatia kuteuliwa kwake kuwa Katibu Mkuu wa Wizara ya Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki ambayo ni Wizara ya Muungano. Wakati wa ziara


Prof. Mkenda (katikati) akiwa ameshikilia  Mpango Mkakati wa Kamisheni hiyo huku akisikiliza maelezo kutoka kwa Prof. Simala (kulia). Kushoto ni Mkurugenzi wa Idara ya Mambo ya Nje Zanzibar, Balozi Mohammed Hamza
Prof. Mkenda (kushoto) akiwa ameongozana na Prof. Simala (wa pili kushoto), Balozi Hamza (mwenye suti) na Maafisa wengine mara baada ya kutembelea Ofisi za Kamisheni ya Kiswahili ya Afrika Mashariki.

No comments:

Post a Comment

Note: Only a member of this blog may post a comment.