Friday, March 9, 2018

Katibu Mkuu akutana na Mabalozi wa Afrika waliopo nchini

Katibu Mkuu wa Wizara ya Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki, Prof. Adolf Mkenda akihutubia kwenye hafla iliyoandaliwa na Umoja wa Mabalozi wa nchi za Afrika nchini Tanzania. Katika hotuba yake Prof. Mkenda aliwashukuru Mabalozi hao kwa kumwalika kwenye hafla hiyo na kuwaahidi kushirikiana nao kwenye shughuli zao za uwakilishi wa mataifa yao hapa nchini.
Balozi wa Misri nchini Mhe. Yasser Ahmed Al Eldin Elshawaf
Balozi wa Algeria nchini, Mhe. Saad Belabeb (kushoto), pamoja na Balozi wa Msumbiji nchini, Mhe. Monica Patricio Clemente wakisikiliza hotuba ya Prof. Mkenda.

Mkurugenzi wa Idara ya Itifaki, Balozi Grace Martin pamoja na Balozi wa Jamhuri ya Kidemokrasia ya Congo hapa nchini, Mhe. Jean Mutamba wakimsikiliza kwa makini Prof. Mkenda hayupo pichani.
Sehemu nyingine ya wageni waalikwa wakifuatilia kwa makini hotuba.

Prof. Mkenda akiendelea kuhutubia kwenye hafla hiyo.
Balozi wa Afrika Kusini akizungumza kama mshereheshaji katika hafla iliyoandaliwa na Umoja wa Mabalozi hao wa Afrika.
Sehemu ya Maafisa kutoka Ofisi mbalimbali za Balozi za Afrika zilizopo nchini.

 


No comments:

Post a Comment

Note: Only a member of this blog may post a comment.