Monday, March 5, 2018

Serikali ya Tanzania na Palestina zasaini Hati ya Makubaliano kuhusu masuala ya Afya.



 Waziri wa Afya, Maendeleo ya Jamii, Jinsia,Wazee na watoto, Mhe. Ummy Mwalimu na Balozi wa Palestina nchini Mhe. Balozi Hazem Shabat  wakisaini Hati ya Makubaliano (MOU)  katika eneo la afya. 
Makubaliano hayo yana lengo la kuboresha mahusiano kati ya Tanzania na Palestina, katika Makubaliano hayo nchi ya Palestina wamekubali kuisaidia Tanzania  katika masuala ya afya hasa katika maeneo ya kuimarisha mifumo ya afya, matibabu ya kibingwa ya moyo, mifupa ya fahamu na saratani, kubadilishana wataalam katika matibabu ya kibingwa na uboreshaji wa mifumo ya TEHAMA.  Makubaliano hayo  yamesainiwa tarehe 05 Machi,2018, katika ukumbi wa Wizara ya Afya, Dar es Salaam
                                    
   Mheshimiwa Waziri Ummy na Mhe. Balozi Shabat wakiendelea kusaini Hati  hiyo ya Makubaliano, wanaoshuhudia  kulia ni Wataalam kutoka Wizara ya Mambo ya Nje na Wizara ya Afya na kushoto ni Naibu Balozi kutoka Ubalozi wa Palestine nchini Bw. Derar Ghannam
                                          
Mhe. Waziri Ummy na Mhe. Balozi Shabat wakibadilishana Mikataba ya Makubaliano hayo baada ya kusaini, wanaoshuhudia ni waandishi wa Habari pamoja na Wataalam kutoka Wizara ya Mambo ya Nje na Wizara ya Afya.

Mheshimiwa Waziri Ummy Mwalimu akiongea baada ya kusaini Hati ya Makubaliano.


 
                                   





No comments:

Post a Comment

Note: Only a member of this blog may post a comment.