Wednesday, March 14, 2018

Prof. Mkenda afanya ziara ya kujitambulisha Zanzibar

Katibu Mkuu wa Wizara ya Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki, Prof. Adolf Mkenda (kulia) akiagana na Katibu wa Baraza la Mapinduzi na Katibu Mkuu Kiongozi, Dkt. Abdulhamid Yahya Mzee mara baada ya kumaliza mazungumzo yao Ofisini kwa Dkt. Mzee, Zanzibar.  Prof. Mkenda alifanya ziara Zanzibar kwa lengo la  kujitambulisha kufuatia kuteuliwa kwake kuwa Katibu Mkuu wa Wizara ya Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki ambayo ni Wizara ya Muungano.
Katibu Mkuu wa Wizara ya Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki Prof. Adolf Mkenda akiwa katika picha ya pamoja na Waziri wa Biashara, Viwanda na Masoko wa Serikali ya Mapinduzi Zanzibar, Mhe. Balozi Amina Salum Ali wakati wa ziara ya Prof. Mkenda ya kujitambulisha.
Balozi Amina Salum Ali akimkabidhi Prof. Mkenda bidhaa za viungo mbalimbali vya chakula vinavyozalishwa Zanzibar
Bidhaa za viungo vya chakula zinazozalishwa Zanzibar.
Katibu Mkuu wa WIzara ya Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki Prof. Adolf Mkenda (kushoto) akiwa katika picha ya pamoja na  Katibu Mkuu, Ofisi ya Rais na Mwenyekiti wa Baraza la Mapinduzi, Mhe. Salum Maulid Salum alipo kwenda kujitambulisha Ofisini kwake Zanzibar hivi karibuni.
Katibu Mkuu wa Wizara ya Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki, Prof. Adolf Mkenda (wanne kushoto) akiwa katika picha ya pamoja na Watumishi wa Idara ya  Mambo ya Nje Zanzibar alipofika kuwatembelea wakati wa ziara yake ya kujitambulisha aliyoifanya Visiwani humo hivi karibuni.



No comments:

Post a Comment

Note: Only a member of this blog may post a comment.