Thursday, March 8, 2018

Makamu wa Rais Mhe. Samia Suluhu Hassan afanya mazungumzo na Mkurugenzi Mkuu wa UNIDO.

Makamu wa Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Mhe. Samia Suluhu Hassan amekutana na kufanya mazungumzo na Mkurugenzi Mkuu wa Shirika la Umoja wa Mataifa linaloshughulikia Maendeleo ya Viwanda (UNIDO), Mh. Li Yong, ambaye yupo nchini kwa ziara ya siku tatu. 
Mazungumzo hayo yamehudhuriwa na Waziri wa Mambo ya Nje na Ushikiano wa Afrika Mashariki, Mhe.Dkt. Augustine Mahiga (Mb.), Waziri wa Viwanda, Biashara na Uwekezaji, Mhe. Charles Mwijage (Mb.)na Waziri wa Fedha na Mipango, Mhe. Dkt. Philip Mpango (Mb.). Mazungumzo hayo yamefanyika katika kituo cha Mikutano cha Kimataifa cha Julius Nyerere, Jijini Dar es salaam, tarehe 08 Machi,2018.
Mhe. Samia Suluhu akimsikiliza Mhe. Yong wakati wa mazungumzo hayo.
Mazungumzo yakiendelea kati ya Mhe. Suluhu na Mhe. Yong, wa kwanza kulia ni Waziri wa Viwanda, Biashara na Uwekezaji, Mhe. Mwijage akifuatilia mazungumzo hayo.
Waziri wa Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki Mhe. Dkt. Augustine Mahiga (wa kwanza kushoto), Waziri wa Fedha  na Mipango, Mhe. Philip Mpango (katikati) na  Naibu Katibu Mkuu Wizara ya Viwanda, Biashara na Uwekaji, Bw. Ludovick J. Nduhiye nao wakifuatilia mazungumzo 
Mwakilishi wa UNIDO nchini  Bw. Stephen Kargbo akifuatilia mazungumzo hayo.
Sehemu ya watumishi wa Serikali wakifuatilia mazungumzo hayo.
Mhe. Samia Suluhu akishuhudia kusainiwa kwa makubaliano ya Mpango shirikishi baina ya nchi, UNIDO na  Washirika wengine wa Maendeleo, wanaosaini Mpango huo kushoto ni Mhe. Waziri  Mwijage na Mkurugenzi Mkuu wa UNIDO Bw. Li Young. Mpango huo umesainiwa katika ukumbi wa Mikutano wa Julius Nyerere, tarehe 08 Machi,2018.
Mhe. Waziri Mwijage na Mkurugenzi Mkuu wa UNIDO Bw. Li Yong wakibadilishana Makubaliano hayo baada ya kusainiwa.
Mhe. Samia Suluhu na Mhe. Li Yong katika picha ya pamoja na Viongozi kutoka Serikalini pamoja na uongozi kutoka UNIDO.








No comments:

Post a Comment

Note: Only a member of this blog may post a comment.