Monday, June 24, 2019

Prof. Kabudi akutana na Waziri wa Mambo ya Nje wa China


 Waziri wa mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki Prof. Palamagamba John Kabudi (Mb) na ujumbe wake akiwa kwenye mkutano pamoja na mwenyeji wake ambaye ni Waziri wa mambo ya nje wa China na na Mjumbe wa Baraza la Taifa Mhe. Wang Yi na ujumbe wake. Mkutano huo umefanyika Beijing,China. June 24, 2019.

Waziri wa mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki, Prof. Palamagamba John Kabudi (Mb) akiteta na mwenyeji wake ambaye ni Waziri wa mambo ya nje wa China na na Mjumbe wa Baraza la Taifa Mhe. Wang Yi na ujumbe wake mara baada ya kumaliza mkutano baina yao. Mkutano huo umefanyika Beijing,China. June 24, 2019.
Waziri wa mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki Prof. Palamagamba John Kabudi  (Mb) akisaini mkataba wa msaada wa shilingi bilioni sitini bila ya masharti yeyote pembeni yake ni Makamu Mwenyekiti wa Shirika la Kimataifa la Misaada ya Maendeleo la China Bw. Zhou Liujun,akisaini kwa niaba ya serikali ya China. Zoezi hilo limefanyika Beijing,China. June 24, 2019.

Waziri wa mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki, Prof. Palamagamba John Kabudi  (Mb) akibadilishana nyaraka na Makamu Mwenyekiti wa Shirika la Kimataifa la Misaada ya Maendeleo la China Bw. Zhou Liujun, mara baada ya kusaini nyaraka hizo. Zoezi hilo limefanyika Beijing, China. June 24, 2019.


Waziri wa mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki Prof. Palamagamba John Kabudi  (Mb) akiwa katika mkutano wa mawaziri wa mambo ya nje kutoka nchi 53 za Afrika na taasisi za fedha za China.
 Sehemu ya mawaziri wa Mambo ya Nje wa Nchi za Afrika na wajumbe wao waliohudhuria katika wamkutano wa mawaziri wa mambo ya nje kutoka nchi 53 za Afrika na taasisi za fedha za China. Beijing,China. June 24, 2019.
  




No comments:

Post a Comment

Note: Only a member of this blog may post a comment.