Wednesday, June 19, 2019

Wizara inaendelea kuhudumia wananchi Wiki ya Utumishi wa Umma

Bw. Hassan Mnondwa,  Mtumishi katika Wizara ya Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki akitoa ufafanuzi kwa Bw. Abdullatif kuhusu majukumu ya Wizara  alipofika kwenye Dawati la Wizara wakati wa kuadhimisha Wiki ya Utumishi wa Umma. Mwingine katika picha ni Mtumishi wa Wizara, Bi. Roxana Kagero. Katika kuadhimisha Wiki ya Utumishi wa Umma ambayo ipo kwa mujibu wa Kalenda ya Umoja wa Afrika, Wizara imefungua madawati maalum kwa ajili ya kutoa huduma mbalimbali kwa wananchi ikiwemo kusikiliza na kujibu hoja zao kuhusu Wizara pamoja na kueleza majukumu yanayotekelezwa na Wizara.
Mtumishi wa Wizara akimhudumia mgeni, Bi.Eunice Mmari kutoka Ofisi ya Kamishna wa Kazi aliyefika kwenye Dawati la Wizara katika Ofisi za Wizara zilizopo Chuo Kikuu cha Dodoma ikiwa ni maadhimisho ya Wiki ya Utumishi wa Umma yaliyoanza tarehe 16 hadi 23 Juni 2019.
Watumishi wa Wizara ya Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki, Bw. Macha na Deogratius wakiwa tayari kuwapokea na kuwahudumia wadau mbalimbali wakati wa maadhimisho ya Wiki ya Utumishi wa Umma
Mtumishi wa Wizara ya Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki, Bi. Jenipher akiwa kwenye dawati lililopo Ofisi za Wizara za Mtumba tayari kwa ajili ya kutoa huduma kwa wananchi wakati wa maadhimisho ya Wiki ya Utumishi wa Umma yanayofanyika kuanzia tarehe 16 hadi 23 Juni 2019
Mtumishi wa Wizara akiwa tayari kwenye dawati lilopo Ofisi ya Mambo ya Nje Zanzibar kwa ajili ya kuwahudumia wananchi katika kuadhimisha Wiki ya Utumishi wa Umma

No comments:

Post a Comment

Note: Only a member of this blog may post a comment.