Wednesday, December 6, 2023

TANZANIA , UTURUKI KUIMARISHA USHIRIKIANO SEKTA YA ELIMU

 


Naibu Waziri Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki Mhe. Balozi Mbarouk Nassor Mbarouk (kulia) akizungumza na Rais wa Taasisi ya Presidency For Turks Abroad and Related Communities ya Jamhuri ya Uturuki (YTB) Bw. Abdullah Eren (kushoto) walipokutana katika Ofisi Ndogo za Wizara Jijini Dar es Salaam.

Rais wa Taasisi ya Presidency For Turks Abroad and Related Communities ya Jamhuri ya Uturuki (YTB) Bw. Abdullah Eren (kushoto) akizungumza na Naibu Waziri Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki Mhe. Balozi Mbarouk Nassor Mbarouk (kulia)

Rais wa Taasisi ya Presidency For Turks Abroad and Related Communities ya Jamhuri ya Uturuki (YTB) Bw. Abdullah Eren (katikati) akizungumza na Naibu Waziri Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki Mhe. Balozi Mbarouk Nassor Mbarouk (kulia) huku Balozi wa Uturuki nchini Mhe. Dkt. Mehmet Gulluoglu (kushoto) akifuatilia mazungumzo hayo
Naibu Waziri Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki Mhe. Balozi Mbarouk Nassor Mbarouk katika picha ya pamoja na Rais wa Taasisi ya Presidency For Turks Abroad and Related Communities ya Jamhuri ya Uturuki (YTB) Bw. Abdullah Eren (kushoto) walipokutana katika Ofisi Ndogo za Wizara Jijini Dar es Salaam

 

Naibu Waziri Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki Mhe. Balozi Mbarouk Nassor Mbarouk (katikati) katika picha ya pamoja na Balozi wa Uturuki nchini Mhe. Dkt. Mehmet Gulluoglu (kulia ) Rais wa Taasisi ya Presidency For Turks Abroad and Related Communities ya Jamhuri ya Uturuki (YTB) Bw. Abdullah Eren (kushoto) katika picha ya pamoja baada ya kumalizika kwa mazungumzo yao katika ofisi ndogo za wizara jijini Dar es Salaam

 

 

 

Naibu Waziri Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki Mhe. Balozi Mbarouk Nassor Mbarouk amekutana kwa mazungumzo na Rais wa Taasisi ya Presidency For Turks Abroad and Related Communities ya Jamhuri ya Uturuki (YTB) Bw. Abdullah Eren katika Ofisi Ndogo za Wizara Jijini Dar es Salaam.

Akizungumza katika kikao hicho, Balozi Mbarouk ameiahidi Taasisi hiyo kuwa Tanzania itaendelea kushirikiana na Uturuki kuendelea kuimarisha uhusiano uliopo kwa manufaa ya pande zote mbili.

Amesema uhusiano kati ya Tanzania na Uturuki ni wa muda mrefu na unaoongoza hasa katika sekta za elimu, afya, biashara na uwekezaji na kuelezea matumaini yake kuwa uhusiano huo utaendelea kuimarika zaidi.

Naye Bw. Eren amesema YTB ni Taasisi ya Uturuki inayojihusisha na utoaji fedha za ufadhili katika ngazi ya elimu ya juu kwa wanafunzi wa mataifa mengine na kusaidia juhudi za mtangamano za Diaspora wa Uturuki wanaoishi nje ya nchi hiyo.

Mazungumzo ya viongozi hao yamelenga kuimarisha uhusiano zaidi katika sekta ya elimu kati ya Tanzania na Uturuki na Mkutano huo umewezesha kubadilishana mawazo na uzoefu katika masuala mbalimbali yenye maslahi kwa pande mbili ikiwa ni pamoja na kuona jinsi ushirikishwaji wa diaspora unavyovyoweza kuchangia maendeleo ya kisiasa, kijamii na kiutamaduni katika nchi husika.
 

No comments:

Post a Comment

Note: Only a member of this blog may post a comment.