Thursday, December 7, 2023

MABALOZI WAPONGEZA JUHUDI ZA SERIKALI UOKOAJI HANANG, WAAHIDI MISAADA ZAIDI YA KIBINADAMU

 

Waziri wa Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki, Mhe. January Makamba (Mb.) akizungumza katika kikao kati yake na Mabalozi na Wawakilishi wa Mashirika wa Kimataifa Jijini Dar es Salaam alipokutana nao na kuwaelezea kilichotokea Hanang mkoani Manyara na hatua zilizochukuliwa na Serikali katika kukabiliana na janga hilo

Waziri wa Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki, Mhe. January Makamba (Mb.) akizungumza na Mabalozi na Wawakilishi wa Mashirika wa Kimataifa (hawapo pichani) alipokutana nao Jijini Dar es Salaam na kuwaelezea kilichotokea Hanang mkoani Manyara na hatua zilizochukuliwa na Serikali katika kukabiliana na janga hilo

 

Waziri wa Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki, Mhe. January Makamba (Mb.) akiongoza Mabalozi na Wawakilishi wa Mashirika wa Kimataifa kusimama kwa dakika moja kwa ajili ya kuwaombea wananchi waliopoteza maisha kutokana na maafa yaliyotokea Hanang mkoani Manyara alipokutana nao Jijini Dar es Salaam na kuwaelezea kilichotokea Hanang mkoani Manyara na hatua zilizochukuliwa na Serikali katika kukabiliana na janga hilo



Mwakilishi Mkazi wa Umoja wa Mataifa nchini Bw. Zlatan Milišić akichangia jambo wakati wa kikao cha Waziri wa Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki na Mabalozi na Wawakilishi wa Mashirika wa Kimataifa Jijini Dar es Salaam ambapo Waziri Makamba aliwaelezea kilichotokea Hanang mkoani Manyara na hatua zilizochukuliwa na Serikali katika kukabiliana na janga hilo

 

Baadhi ya Mabalozi na Wawakilishi wa Mashirika wa Kimataifa nchini wakimsikiliza Waziri wa Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki Mhe. January Makamba alipokutana nao Jijini Dar es Salaam kuwaelezea kilichotokea Hanang mkoani Manyara na hatua zilizochukuliwa na Serikali katika kukabiliana na janga hilo

 



Balozi wa Somalia nchini, Mhe. Zahra Ali Hassan akichangia jambo wakati wa kikao cha Waziri wa Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki na Mabalozi na Wawakilishi wa Mashirika wa Kimataifa Jijini Dar es Salaam ambapo Waziri Makamba aliwaelezea kilichotokea Hanang mkoani Manyara na hatua zilizochukuliwa na Serikali katika kukabiliana na janga hilo



Baadhi ya Mabalozi na Wawakilishi wa Mashirika wa Kimataifa nchini wakimsikiliza Waziri wa Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki alipokutana nao Jijini Dar es Salaam kuwaelezea kilichotokea Hanang mkoani Manyara na hatua zilizochukuliwa na Serikali katika kukabiliana na janga hilo

 


Waziri wa Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki Mhe. January Makamba akizungumza na Balozi wa Italia nnchini Mhe. Marco Lombardi alipokutana na Mabalozi na Wawakilishi wa Mashirika wa Kimataifa nchini Jijini Dar es Salaam kuwaelezea kilichotokea Hanang mkoani Manyara na hatua zilizochukuliwa na Serikali katika kukabiliana na janga hilo

 





Katibu Mkuu Wizara ya Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki Balozi Dkt. Samwel Shelukindo (kushoto) na Katibu Mkuu Wizara ya Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki Balozi Stephen Mbundi (katikati) wakizungumza na mmoja wa washiriki wa kikao kati ya Waziri wa Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki alipokutana na Mabalozi na Wawakilishi wa Mashirika ya Kimataifa jijini Dar es Salam kuelezea yaliyotokea mkoani Manyara na jinsi Serikali ilivyokabiliana na janga hilo.

Waziri wa Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki Mhe. January Makamba akizungumza na Balozi wa Marekani nchini Mhe. Michael Battle alipokutana na Mabalozi na Wawakilishi wa Mashirika wa Kimataifa nchini Jijini Dar es Salaam kuwaelezea kilichotokea Hanang mkoani Manyara na hatua zilizochukuliwa na Serikali katika kukabiliana na janga hilo

 





NaibuWaziri wa Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki Balozi Mbarouk Nassor Mbarouk akizungumza na Balozi wa Kenya nchini Mhe. Isack Njenga wakati wa Kikao kati ya Waziri wa Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki  Mhe. January Makamba na Mabalozi na Wawakilishi wa Mashirika wa Kimataifa nchini Jijini Dar es Salaam kuwaelezea kilichotokea Hanang mkoani Manyara na hatua zilizochukuliwa na Serikali katika kukabiliana na janga hilo

 

Mkurugenzi wa Mawasiliano Wizara ya Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki Balozi Mindi Kasiga akizungumza kuwakaribisha Mabalozi na Wawakilishi wa Mashirika wa Kimataifa nchini Jijini Dar es Salaam kuzungumza na Waziri wa Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki Mhe. Januari Makamba

 


 

 

Mabalozi na Wawakilishi wa Mashirika ya Kimataifa nchini wamepongeza jitihada zinazochukuliwa na Serikali katika zoezi la uokoaji Hanang, kutokana na maporomoko ya tope kutoka katika mlima Hanang kufuatia mvua kubwa iliyonyesha Mkoani Manyara tarehe 02 Disemba, 2023.

 

Mabalozi na Wawakilishi wa Mashirika hayo wametoa pongezi hizo Jijini Dar es Salaam walipokutana na Waziri wa Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki, Mhe. January Makamba (Mb.) aliyewaita kuwaelezea kilichotokea Hanang mkoani Manyara na hatua zilizochukuliwa na Serikali katika kukabiliana na janga hilo.

 

Akizungumza katika kikao hicho Mhe. Waziri Makamba amesema maporomoko hayo ya tope yamesababisha vifo vya watu 72, kujeruhi watu 117, kuharibu mali za watu, makazi na miundombinu ya barabara, maji na umeme.

 

“Serikali ya Tanzania inaishukuru Jumuiya ya Kimataifa nchini kwa jinsi ilivyoikimbilia na kusaidia wahanga wa maporomoko hayo hasa katika kusaidia urejeshaji wa huduma za muhimu za kibinadamu kwa wananchi wa Katesh” alisema.

 

Amesema katika kukabiliana na janga hilo, Serikali iliunda Kamati ya Kitaifa ya Maafa iliyo chini ya Ofisi ya Waziri Mkuu inayoshirikiana na mamlaka ya Mkoa wa Manyara na kufungua akaunti Maalum ya maafa kwa ajili ya kuratibu na upokeaji misaada mbalimbali ili kusaidia wahanga wa maporomoko hayo na kuwezesha maisha ya watu kuendelea kama kawaida.

 

“Wahanga bado wanahitaji misaada ya kibinadamu ya hali na mali, wengi wamepoteza makazi yao na kupoteza wapendwa wao pamoja na kuharibika kwa miundombinu ya barabara, maji na umeme na kusababisha maisha kusimama katika eneo hilo” alisema.

 

Amesema Serikali imeandaa maeneo maalum kwa ajili ya kuwahifadhi na kuwahudumia wahanga kwa kuwapatia huduma muhimu za kibinadamu, kuwatibu majeruhi, na kuwaokoa na kuwaondoa watu katika maeneo yaliyoathiriwa.

 

Amesema Serikali inaendelea na zoezi la kutafuta miili ya watu katika matope, kuhudumia shughuli za mazishi ya watu waliofariki na kuwafariji watu waliopoteza wapendwa wao kutokana na maporomoko hayo ili waweze kurejea katika hali zao za kawaida.

 

Naye Mwakilishi Mkazi wa Umoja wa Mataifa nchini Mhe. Zlatan Milisick amepongeza hatua za haraka zilizochukuliwa na Serikali katika zoezi la uokoaji wa wananchi na mali zao huko Hanang na kuongeza kuwa Ofisi ya Umoja wa Mataifa Tanzania itaendelea kushirikiana na Serikali na kwamba Mashirika ya Umoja wa Mataifa nchini yameungana na kuchanga misaada ya yao ya kibinadamu kwa ajili ya kusaidia wahanga hao ambayo wataikabidhi kwa Serikali.

 

Balozi wa Kenya amesema Kenya kama nchi jirani iko pamoja na Watanzania katika sala na maombi kuwaombea marehemu na kutoa pole kwa familia za marehemu.

 

Akizungumza katika kikao hicho Balozi wa Somalia nchini Mhe. Zahra Ali Hassan amesema Umoja wa Mabalozi wa Afrika kwa umoja wao wameungana na kuwaingiza katika maombi wahanga wa maporomoko hayo na kuchanga misaada ya kibinadamu ambayo wataikabidhi kwa Serikali na kutoa pole kwa Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania na Watanzania wote kwa maafa hayo makubwa yaliyotokea nchini.

 

Balozi wa Msumbiji Mhe.  Ricardo Mtumbuida amesema Msumbiji inaungana na Tanzania na kutoa pole kwa Mhe. Rais, Watanzania na wahanga wote na kuwaombea marehemu wapumzike kwa amani.


 


No comments:

Post a Comment

Note: Only a member of this blog may post a comment.