Monday, July 11, 2022

BALOZI MULAMULA AKUTANA NA WANAFUNZI-DIASPORA WA MAREKANI.

Waziri wa Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki, Balozi Liberata Mulamula amekutana na walimu na wanafunzi wenye asili ya Afrika na Marekani wanaofundisha na kusoma vyuo mbalimbali vya Marekani ambao wapo nchini kwa ziara ya kikazi hadi tarehe 17 Julai 2022.

Ziara hiyo iliyoratibiwa na Mtanzania-Diaspora, Bi Zawadi Sakapala ambaye ni mmiliki wa kituo cha “Community Centre” kilichopo Kijichi jijini Dar Es Salaam inalenga pamoja na mambo mngine, kutoa fursa kwa wanafunzi hao kujifunza masuala ya utamaduni wa Tanzania na kubadilishana ujuzi na uzoefu katika masomo ya sayansi, ufundi, ufundishaji na Usimamizi wa watoto wadogo (daycare).

Katika kikao hicho, Bi Zawadi alimfahamisha Mhe. Balozi Mulamula kuwa kituo chake kimekuwa kikishirikiana na vyuo vikuu mbalimbali nchini Marekani kuratibu ziara za walimu na wanafunzi wenye asili ya Afrika na Marekani kutembelea nchi za Afrika kwa ajili ya kubadilishana uzoefu katika sekta ya elimu.

Hivyo, ili kuimarisha sekta ya elimu katika nchi za Afrika, kikao hicho kiliazimia kuongeza jitihada za kuhamasisha Waafrika wengi zaidi kujiunga na vyuo vya Marekani, kuunganisha vyuo vya Afrika na Marekani, wanafunzi-Watanzania wanaopata fursa ya kusoma Marekani, watumike kufundisha lugha ya Kiswahili ikiwa ni moja ya njia ya kueneza lugha hiyo duniani pamoja na kwahimiza watu wenye asili ya Afrika kutumia elimu, ujuzi na maarifa waliyopata wakiwa ughaibuni kuinua jamii za nchi za Afrika.

Wakati huo huo, Balozi Mulamula amekutana na Ujumbe wa Shirika la Umoja wa Mataifa la Programu ya Maendeleo (UNDP) ambao upo nchini kwa ajili ya kufanya mazungumzo na wadau wa siasa ili kubainisha maeneo ambayo, shirika hilo linaweza kusaidia katika uendeshaji wa uchaguzi mkuu ujao.

Ujumbe huo unaongozwa na Afisa Uchaguzi Mkuu katika Idara ya Siasa na Masuala ya Amani ya Umoja wa Mataifa, Bw. Akinyemi Adegbola umefanikiwa kufanya vikao na wadau mbalimbali ikiwa ni pamoja na Tume ya Taifa ya Uchaguzi, wawakilishi wa vyama vya siasa na asasi za kiraia, umepokea maoni ya wadau hao ya maoneo yanayohitaji msaada na umeahidi utayafanyia kazi kikamilifu. Maeneo hayo ni pamoja na uelimishaji wa wapiga kura, msaada wa kiufundi katika upigaji na uandikishwaji wa wapiga kura na teknolojia ya mawasiliano wakati zoezi la uchaguzi.

Kwa upande wake, Balozi Mulamula aliueleza ujumbe huo kuwa Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Mhe. Samia Suluhu Hassan katika kipindi kifupi cha uongozi wake ameonesha dhamira ya dhati ya kuboresha mazingira ya kisiasa nchini, kwa kuhamasisha majadiliano ya kisiasa, ushirikishwaji wa wadau wote, umoja na mshikamano wa kitaifa. Hivyo, aliuhakikishia ujumbe huo kuwa uchaguzi ujao utaendelea kuwa huru, haki na amani kama ilivyo desturi ya Tanzania.

Waziri wa Mambo ya Nje na Ushiikiano wa Afrika Mashariki, Balozi Liberata Mulamula akiongea na walimu na wanafunzi wenye asili ya Afrika na Marekani (hawapo pichani) wanaosoma na kufundisha vyuo mbalimbali vya Marekani ambao wapo nchini kwa ziara maalum hadi tarehe 17 Julai 2022.


Waziri wa Mambo ya Nje na Ushiikiano wa Afrika Mashariki, Balozi Liberata Mulamula akimsikiliza mmoja wa mwanafunzi anayesoma katika vyuo vikuu vya Marekani kuhusu mikakati ya kusaidia vijana wa Afrika kupata elimu bora itakayoweza kukabili mazingira ya dunia ya sasa.

Mhitimu wa Shahada ya Uzamivu kutoka Chuo Kikuu cha Howard cha nchini Marekani ambaye pia ni Kiongozi wa Taasisi ya 3GC Inc. akieleza shughuli za taasisi hiyo zinazolenga kuwasaidia vijana wa Afrika 
Mkurugenzi wa Kitengo cha Diaspora katika Wizara ya Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki, Balozi James Bwana na Mkurugenzi wa Kitengo cha Mawasiliano ya Serikali, Balozi Mindi Kasiga wakifuatilia mazungumzo baina ya Waziri wa Mambo ya Nje na Ushiikiano wa Afrika Mashariki, Balozi Liberata Mulamula na walimu na wanafunzi wenye asili ya Afrika na Marekani wanaosoma na kufundisha vyuo mbalimbali vya Marekani


Waziri wa Mambo ya Nje na Ushiikiano wa Afrika Mashariki, Balozi Liberata Mulamula akimvisha scurf ya bendera ya Tanzania, mmiliki wa kituo cha “Community Centre” kilichopo Kijichi jijini Dar Es Salaam, Bi. Zawadi Sakapala

Waziri wa Mambo ya Nje na Ushiikiano wa Afrika Mashariki, Balozi Liberata Mulamula akiwa katika picha ya pamoja na walimu na wanafunzi wenye asili ya Afrika na Marekani wanaosoma na kufundisha vyuo mbalimbali vya Marekani



BALOZI MULAMULA AKUTANA NA  AFISA UCHAGUZI MKUU WA UN


Waziri wa Mambo ya Nje na Ushiikiano wa Afrika Mashariki, Balozi Liberata Mulamula akiwa katika mazungumzo na Afisa Uchaguzi Mkuu katika Idara ya Siasa na Masuala ya Amani ya Umoja wa Mataifa, Bw. Akinyemi Adegbola yaliyofanyika jijini Dar Es Salaam

Baadhi ya ujumbe uliongozana na Afisa Uchaguzi Mkuu katika Idara ya Siasa na Masuala ya Amani ya Umoja wa Mataifa, Bw. Akinyemi Adegbola kwenye mazungumzo ya Waziri wa Mambo ya Nje na Ushiikiano wa Afrika Mashariki, Balozi Liberata Mulamula na Afisa huyo.

Ujumbe wa Waziri wa Mambo ya Nje na Ushiikiano wa Afrika Mashariki, Balozi Liberata Mulamula ukifuatilia mazungumzo yake na Afisa Uchaguzi Mkuu katika Idara ya Siasa na Masuala ya Amani ya Umoja wa Mataifa

Waziri wa Mambo ya Nje na Ushiikiano wa Afrika Mashariki, Balozi Liberata Mulamula akiagana na ujumbe wa UNDP ambao upo nchini kwa ajili ya kuzungumza na wadau wa siasa kuhusu uchaguzi.

Waziri wa Mambo ya Nje na Ushiikiano wa Afrika Mashariki, Balozi Liberata Mulamula akiwa katika picha ya pamoja na ujumbe wa UNDP ambao upo nchini kwa ajili ya kuzungumza na wadau wa siasa kuhusu uchaguzi.


BALOZI MULAMULA AKUTANA NA MWAKILISHI MKAZI WA UN WOMEN

Waziri wa Mambo ya Nje na Ushiikiano wa Afrika Mashariki, Balozi Liberata Mulamula akiwa katika mazungumzo na Mwakilishi Mkazi wa  UN Women, Bi.  Hodan Addou kwenye Hoteli ya Seana jinini Dar Es Salaam.


BALOZI MULAMULA AKUTANA NA  BALOZI MTEULE LT. JEN. MATHEW EDWARD MKINGULE 

Waziri wa Mambo ya Nje na Ushiikiano wa Afrika Mashariki, Balozi Liberata Mulamula akiwa katika mazungumzo na Balozi Mteule Lt. Jen. Mathew Edward Mkingule yaliyofanyika jijini Dar Es Salaam


Waziri wa Mambo ya Nje na Ushiikiano wa Afrika Mashariki, Balozi Liberata Mulamula akiwa na Balozi Mteule Lt. Jen. Mathew Edward Mkingule baada ya mazungumzo yao yaliyofanyika jijini Dar Es Salaam


 

VACANCY ANNOUNCEMENT


 

Saturday, July 9, 2022

WAZIRI MULAMULA: WAFANYABIASHARA CHANGAMKIENI FURSA ZA MASOKO KATIKA JUMUIYA ZA KIKANDA


Waziri wa Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki Mhe. Balozi Liberata Mulamula ametoa rai kwa Wafanyabiashara wa Tanzania kuchangamkia fursa za masoko zinazopatikana katika Jumuiya za Kikanda ambazo Tanzania ni mwanachama kama vile Jumuiya ya Afrika Mashariki (EAC), Jumuiya ya Maendeleo Kusini mwa Afrika (SADC) na fursa zitokanazao na Eneo Huru la Biashara Afrika (AfCFTA)

Waziri Mulamula ametoa rai hiyo wakati akizungumza na wafanyanyabisha kwenye maadhimisho ya kilele cha Maonesho ya Bukoba “Bukoba Expo" yaliyofanyika katika Viwanja ya CCM mjini Bukoba. Maonesho hayo yaliyobebwa na kauli mbiu isemayo “Biashara, viwanda na utalii ni fursa ya uwekezaji Mkoani Kagera”.

Akizungumza na wafanyabiashara wakati wa akifunga maonesho hayo Waziri Mulamula alieleza kuwa Serikali ya Jamhuri ya Muungano wa Tanzania inayoongozwa na Mheshimiwa Rais Samia Suluhu Hassan inayo dhamira ya dhati ya kukuza uchumi wa nchi kupitia biashara na uwekezaji kwa kudumisha ushirikiano na nchi jirani na kutafuta fursa za masoko kwa bidhaa zinazozalishwa nchini. Aliongeza kusema wakati Serikali inafanya hayo ni vyema sekta binafsi ikaunga mkono juhudi hizo za Serikali kwa kuchangamkia fursa za masoko zinazopatikana katika Jumuiya za Kikanda ili kujiongezea tija zaidi katika shughuli zao. 

"Mtakumbuka kuwa Tanzania pamoja na kuwa mwanachama wa Jumuiya ya Afrika Mashariki pia ni mwanachama wa SADC na hivi karibuni tumeridhia mkataba wa Eneo Huru la Biashara la Bara la Afrika (Africa Continental Free Trade Area-AfCFTA). Eneo Huru la Biashara la Afrika ni soko kubwa kuliko masoko yote yaliyoanzishwa ulimwenguni kwa kuwa na uwingi wa nchi wanachama zinazofikia 55. Soko hili linakadiriwa kuwa na idadi ya watu wapatao Bilioni 1.3 na Pato ghafi la Taifa (GDP) lenye jumla ya Dola za Marekani trilioni 3.4 na fursa za uchumi unaokua kwa kasi". Alieza Waziri Mulamula

Akizungumzia kuhusu maonesho hayo Waziri Mulamula ameleeza kuwa ubunifu wa waandaji umeakisi maono ya Rais Samia Suluhu Hassan ya kuhakikisha Mkoa wa Kagera na wananchi wake wanapata maendeleo kwa kushiriki kikamilifu katika shughuli za uchumi, biashara na uwekezaji kwa kutumia fursa zilizopo katika Mkoa huo na nafasi ya Kijiografia ya Mkoa kwa kupakana na nchi za Rwanda, Burundi na Uganda.

Kwa upande wake mratibu na mwandaaji wa Maonesho ya Bukoba Bw. William Rutta ameeleza kuwa maonesho hayo ambayo yamewavutia washiriki zaidi ya 350 wakiwemo wajasiliamari, wafanyabiashara, Taasisi za serikali na washiriki kutoka nchi za Burundi, Uganda, na Congo yametembelewa na wateja zaidi ya 10,000.

Aidha Bw. Rutta amebainisha malengo ya amonesho hayo kuwa ni pamoja na kuweka mwendelezo wa wiki ya uwekezaji ya Kagera ya mwaka 2019, kuunganisha wafanyabiashara na wananchi wote kushiriki katika shughuli za kuzalisha, mali, kuendeleza utalii na kubadilishana teknolojia ya uzalishaji na kuhamasisha utalii kwa kuandaa safari katika mbuga za wanyama asili za Burigi, Ibanda kyerwa, Runanyika Karagawe, Hifadhi ya Rubondo, Seregeti na vivutio vya asili kama fukwe za ziwa Victoria. Lengo lingine ni uboreshaji wa mazingira kwa kuhamasishwa upandaji miti aina ya palm tree katika mji wa Bukoba.

Waziri Mulamula kwenye maadhimisho ya kilele cha maonesho hayo pamoja na wajumbe wengine aliambatana na Mkuu wa Mkoa wa Kagera Mhe. Meja Jenerali, Charles Mbuge, Mkuu wa Wilaya ya Bukoba Mhe. Moses Machali na Mwenyekiti wa CCM Mkoa wa Kagera Bi. Costansia Guhiye.
Waziri wa Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki Mhe. Balozi Liberata Mulamula akizungumza na mmoja wa washiriki wa Maonesho ya Bukoba 
Waziri wa Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki Mhe. Balozi Liberata Mulamula (aliyevalia kilemba) na Mkuu wa Mkoa wa Kagera Mhe. Meja Jenerali Charles Mbuge akiwa katika picha ya pamoja Waandaaji wa Maonesho ya Kagera na Washiriki wa maonesho hayo. 
Waziri wa Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki Mhe. Balozi Liberata Mulamula akisalimiana na Mkuu wa Wilaya ya Bukoba Mhe. Moses Machali alipowasili kwenye maadhimisho ya kilele cha Maonesho ya Bukoba yaliyofanyika katika viwanja vya CCM Bukoba mjini
Waziri wa Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki Mhe. Balozi Liberata Mulamula akifuatilia matukio mbalimbali yaliyokuwa yakiendelea kwenye maadhimisho ya kilele cha Maonesho ya Bukoba
Waziri wa Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki Mhe. Balozi Liberata Mulamula akimkabidhi cheti cha kufanyavizuri mmoja wa washiriki wa Maonesho Bukoba kutoka nchini Burundi
Waziri wa Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki Mhe. Balozi Liberata Mulamula akizungumza hadhira iliyojitokeza kwenye maadhimisho ya kilele cha Maonesho ya Bukoba
Waziri wa Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki Mhe. Balozi Liberata Mulamula akiwa katika picha na mmoja wa washiriki wa Bukoba Expo mzalishaji wa bidhaa za mafuta ya asili ya ngozi
Waziri wa Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki Mhe. Balozi Liberata Mulamula akipokelewa katika viwanja vya CCM mjini Bukoba alipowasili kwenye maadhimisho ya kilele cha Maonesho ya Bukoba “Bukoba Expo”.
Meza kuu wakifuatilia matukio mbalimbali yaliyokuwa yakiendelea kwenye madhimisho ya kilele cha Maonesho ya Bukoba
Waziri wa Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki Mhe. Balozi Liberata Mulamula akiwasili kwenye maadhimisho ya kilele cha Maonesho ya Bukoba “Bukoba Expo” yaliyofanyika katika viwanja vya CCM Bukoba mjini.
Waziri wa Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki Mhe. Balozi Liberata Mulamula akizungumza na mmoja wa washiriki wa Maonesho ya Bukoba
Waziri wa Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki Mhe. Balozi Liberata Mulamula akiangalia bidhaa za mmoja wa washiriki wa Bukoba Expo 
Waziri wa Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki Mhe. Balozi Liberata Mulamula akimsikiliza Mkurugenzi wa Masoko wa Kampuni ya Mati Super Brands Ltd Bw. Living Munishi kwenye maadhimisho ya kilele cha Maonesho ya Bukoba
Waziri wa Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki Mhe. Balozi Liberata Mulamula akifurahia jambo baada zoezi la upandaji mti kwenye madhimisho ya kilele cha Maonesho ya Bukoba

WIZARA YA MAMBO YA NJE NA NSSF ZAJADILI FURSA ZA UWEKEZAJI NJE YA NCHI

Katibu Mkuu Wizara ya Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki, Balozi Joseph Sokoine amefanya mazungumzo na Mkurugenzi Mkuu wa Mfuko wa Taifa wa Hifadhi ya Jamii - NSSF, Bw. Masha Mshomba tarehe 8 Julai 2022 katika ofisi ndogo za Wizara jijini Dar es Salaam.


Viongozi hao wamejadili juu ya umuhimu wa kukuza na kuimarisha ushirikiano baina ya Wizara na mfuko huo wa NSSF.  


Pamoja na mambo mengine viongozi hao wamezungumzia kuhusu uwekezaji kwenye viwanja vya Serikali nje ya nchi ili kuona namna ambavyo Wizara na NSSF wanaweza kushirikiana katika miradi ya ujenzi wa ofisi na vitega uchumi.


Aidha, Balozi Sokoine akaeleza kuwa Serikali ina miliki viwanja zaidi ya 40 kwenye maeneo ya uwakilishi nje ya nchi, hivyo akatoa rai kwa taasisi hiyo kushirikiana na Wizara katika kuviendeleza kwa kujenga majengo ya Ofisi za Balozi pamoja na vitega uchumi ili kuipunguzia Serikali gharama ya kupanga lakini zaidi  kupata faida kutokana na vitega uchumi hivyo.


Naye Bw. Mshomba aliafiki wazo hilo la uwekezaji na kueleza kuwa  NSSF imeshakuwa na mipango ya miradi ya uwekezaji nje ya nchi hivyo, wazo hilo limekuja wakati mwafaka na kwamba NSSF inaunga mkono juhudi za Serikali ya Awamu ya Sita za kufungua mipaka hususan katika sekta ya biashara na uwekezaji.


Aidha, Kikao hicho kiliridhia kuundwa kwa timu ya Wataalamu kutoka katika pande zote mbili ili kuruhusu kufanyika kwa tathmini ya kina juu ya uwekezaji huo na faida zake ili kuweza kuwa na miradi ya pamoja na Wizara wenye tija kwa Taifa.


======================================


Katibu Mkuu Wizara ya Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki, Mhe. Balozi Joseph Sokoine (kulia) amefanya mazungumzo na Mkurugenzi Mkuu wa Mfuko wa Taifa wa Hifadhi ya Jamii - NSSF, Bw. Masha Mshomba tarehe 8 Julai 2022 katika ofisi ndogo za Wizara jijini Dar es Salaam.

Mkurugenzi Mkuu wa Mfuko wa Taifa wa Hifadhi ya Jamii - NSSF, Bw. Masha Mshomba (wa pili kulia) akiwa katika mazungumzo na Balozi Joseph Sokoine (hayupo pichani) katika Ofisi Ndogo za Wizara jijini Dar es Salaam.
 Kulia ni Mkurugenzi wa Mipango na Utawala - NSSF, Bw. Gabriel Silayo na wa tatu kutoka kulia ni Meneja Uhusiano na Elimu kwa Umma - NSSF, Bi. Lulu Mengele.

Kaimu Mkurugenzi Idara ya Sera na Mipango, Bw. Justin Kisoka akifafanua juu ya uwekezaji wa miradi ya pamoja na namna Wizara na NSSF zinavyoweza kushirikiana katika kutathmini uwekezaji kwenye maeneo ya miradi.

Kushoto ni Mkurugenzi wa Idara ya Diaspora katika Wizara ya Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki, Balozi James Bwana na kulia ni Mkurugenzi wa Kitengo cha Sheria katika Wizara hiyo wakifuatilia mazungumzo.

Picha ya pamoja

 


Friday, July 8, 2022

WIZARA YAAHIDI KUALIKA WASHIRIKI WENGI ZAIDI WA NJE KATIKA MAONESHO YA SABASABA

Naibu Waziri wa Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki, Balozi Mbarouk N. Mbarouk amesema kuwa Wizara pamoja na balozi zake, itaendelea kuhamasisha nchi marafiki na mashirika ya kimataifa kushiriki maonesho ya Kimataifa ya Biashara (Sabasaba) ambayo amesema yanazidi kuimarika ukilinganisha na miaka ya nyuma.

Kauli hiyo ameitoa leo tarehe 08 Julai 2022 alipotembelea maonesho hayo yanayofanyika kwenye viwanja vya Julius Nyerere, barabara ya Kilwa jijini Dar Es Salaam.

Balozi Mbarouk amesema kuwa kushiriki kwa wageni wengi kutoka nje ya nchi, kuna faida kubwa kwa wafanyabiashara wa hapa nyumbani, kwa kuwa kuna wapa fursa ya kujifunza teknolojia mpya, kupata masoko ya bidhaa wanazozizalisha na wabia wa kushirikiana nao katika biashara na uwekezaji.

Akiwa kwenye viwanja hivyo, Mhe. Naibu Waziri alitembelea mabanda mbalimbali ya washiriki wa maonesho hayo, hususan wale wa kutoka nje ya nchi ili kujionea bidhaa, huduma na teknolojia walizokuja nazo. Katika maongezi na washiriki hao alisisitiza umuhimu wa kubadilishana teknolojia na uzoefu na wafanyabiashara wa hapa nchini ili kujenga uwezo wa kuzalisha bidhaa bora zitakazokuwa na uwezo wa kukabili ushindani wa soko la dunia.

Katibu Mkuu wa Wizara hiyo, Balozi Joseph Sokoine aliahidi kuwa Wizara yake itashirikiana na wadau wengine kama Mamlaka ya Maendeleo ya Biashara (TANTRADE) na Wizara ya Uwekezaji, Viwanda na Biashara kuhakikisha kuwa wafanyabiashara wengi zaidi kutoka nje ya nchi wanashiriki maonesho hayo. “Wizara yetu ni mdau mkubwa katika utekelezaji wa Diplomasia ya Uchumi na maonesho ni jukwaa muhimu katika diplomasia ya uchumi, hivyo tutaongeza nguvu zaidi kushajihisha kampuni nyingi zaidi kutoka nje, zishiriki maonesho haya mwakani na miaka mingine”, Alisema Balozi Sokoine.

Maonesho ya Biashara ya Kimataifa ya mwaka 2022 yalianza tarehe 28 Juni na yanatarajiwa kuhitimishwa tarehe 13 Julai 2022 ambapo nchi 20 zinashiriki kwa kuoenesha bidhaa, huduma na teknolojia mbalimbali.

Naibu Waziri wa Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki, Balozi Mbarouk Nassor Mbarouk akisaini Kitabu cha Wageni baada ya kuwasili katika Bnada la Wizara ya Mambo ya Nje lilipo katika Maonesho ya Kimataifa ya Biashara (Sabasaba). Aliyesimama ni Mkurugenzi wa Kitengo cha Mawasiliano ya Serikali, Balozi Mindi Kasiga.
Naibu Waziri wa Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki, Balozi Mbarouk Nassor Mbarouk akipewa maelezo kuhusu ushiriki wa Wizara katika Maonesho ya Kimataifa ya Biashara (Sabasaba) na Mkurugenzi wa Kitengo cha Mawasiliano ya Serikali, Balozi Mindi Kasiga.

Naibu Waziri wa Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki, Balozi Mbarouk Nassor Mbarouk akiwa katika moja ya banda yaliyopo kwenye Maonesho ya Kimataifa ya Biashara (Sabasaba)
Naibu Waziri wa Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki, Balozi Mbarouk Nassor Mbarouk akisikiliza maelezo ya mshiriki wa Maonesho ya Kimataifa ya Biashara (Sabasaba) kutoka nje ya nchi
Naibu Waziri wa Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki, Balozi Mbarouk Nassor Mbarouk akiwa katika picha ya pamoja na watumishi wa Wizara ya Mambo ya Nje wanaoshiriki Maonesho ya Kimataifa ya Biashara (Sabasaba)


KATIBU MKUU KATIKA MAONESHO YA SABASABA

Katibu Mkuu wa Wizara ya Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki, Balozi Joseph Sokoine akiwa kwenye viwanja vya Maonesho ya Kimataifa ya Biashara (Sabasaba) kwa ajili ya kutembelea mabanda mbalimbali kujionea bidhaa, huduma na teknolojia..

Katibu Mkuu wa Wizara ya Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki, Balozi Joseph Sokoine akisaini Kitabu cha Wageni baada ya kuwasili katika Bnada la Wizara ya Mambo ya Nje lilipo katika Maonesho ya Kimataifa ya Biashara (Sabasaba).

Katibu Mkuu wa Wizara ya Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki, Balozi Joseph Sokoine akipewa maelezo kuhusu ushiriki wa Wizara katika Maonesho ya Kimataifa ya Biashara (Sabasaba) na Mkurugenzi wa Kitengo cha Mawasiliano ya Serikali, Balozi Mindi Kasiga.

Katibu Mkuu wa Wizara ya Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki, Balozi Joseph Sokoine akisalimiana na Balozi wa Marekani hapa nchini ambaye alifika kutembelea 

Bnada la Wizara ya Mambo ya Nje lilipo katika Maonesho ya Kimataifa ya Biashara (Sabasaba).

Katibu Mkuu wa Wizara ya Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki, Balozi Joseph Sokoine akiwa katika picha ya pamoja na watumishi wa Wizara ya Mambo ya Nje wanaoshiriki Maonesho ya Kimataifa ya Biashara (Sabasaba

 

Thursday, July 7, 2022

UONGOZI WA CCM MKOANI KAGERA WAPONGEZA UTENDAJI WA WAZIRI MULAMULA

Uongozi wa Chama cha Mapinduzi (CCM) Mkoa wa Kagera wamempongeza Waziri wa Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki Mhe. Balozi Liberata Mulamula kwa kazi nzuri anayoendelea kuifanya ya kuimarisha Uhusiano wa Kidiplomasia baina ya Tanzania na Mataifa mengine ulimwenguni sambamba na kutekeleza vyema diplomasia ya uchumi. 

Haya yamesemwa na Mwenyekiti wa CCM Mkoa wa Kagera Bi. Costansia Guhiye wakati wa mazungumzo yaliyofanyika baina ya Viongozi wa Chama wa Mkoa huo na Waziri Mulamula alipotembelea Ofisi Kuu ya Chama Mkoa wa Kagera mjini Bukoba.

Katika mazungumzo hayo Waziri Mulamula alitoa rai kwa viongozi hao kuendelea kuwahamasisha na kuwahimiza wananchi wa Mkoa wa Kagera kuchangamkia fursa zinazopatika katika Nchi Wanachama wa Jumuiya ya Afrika Mashariki kama vile biashara na fursa za kufundisha Kiswahili zinazopatikana katika Nchi wanachama wa Jumuiya. 

Sambamba na hayo Waziri Mulamula amepongeza jitihada zinazofanywa na viongozi hao katika kulea na kukuza Chama, kuhamasisha amani, maendeleo, umoja na mshikamano kwa wananchi wa Mkoa huo. Aidha amewatakia maandalizi mema ya uchaguzi wa Chama unaotarajiwa kufanyika katika siku za usoni. 

Waziri Mulamula amewasili Mkoani Kagera leo tarehe 7 Julai 2022 ambapo anatarijiwa kuwa mgeni rasmi kwenye maadhimisho ya kilekile cha Monesho ya Bukoba “Bukoba Expo” tarehe 8 Julai 2022 yanayofanyika katika viwanja vya CCM mjini humo. 
Waziri wa Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki Mhe. Balozi Liberata Mulamula akizungumza na Uongozi wa Chama cha Mapinduzi (CCM) Mkoa wa Kagera 
Kuotaka kushoto, Mwenyekiti wa CCM Mkoa wa Kagera Bi. Costansia Guhiye, Waziri wa Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki Mhe. Balozi Liberata Mulamula na Katibu wa CCM Mkoa wa Kagera Ndugu Christopher Paranjo wakifurahia jambo.
Waziri wa Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki Mhe. Balozi Liberata Mulamula akiwa katika picha ya pamoja na Viongozi wa CCM Mkoa wa Kagera.
Waziri wa Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki Mhe. Balozi Liberata Mulamula akisisitiza jambo wakati wa mazungumzo na Uongozi wa Chama cha Mapinduzi (CCM) Mkoa wa Kagera 
Mwenyekiti wa CCM Mkoa wa Kagera Bi. Costansia Guhiye akisisitiza jambo wakati wa mazungumzo baina ya Uongozi wa Chama cha Mapinduzi Mkoa wa Kagera na Waziri Mulamula
Waziri wa Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki Mhe. Balozi Liberata Mulamula (kulia) akisaini kitabu cha wageni alipotembelea Ofisi Kuu ya Chama Mkoa wa Kagera mjini Bukoba
Katibu wa CCM Mkoa wa Kagera Ndugu Christopher Paranjo akielezea jambo wakati wa mazungumzo baina ya Uongozi wa Chama cha Mapinduzi wa Mkoa huo na Waziri Mulamula