Thursday, March 20, 2014

Binti Mfalme wa Sweden awasili nchini kwa ziara ya kikazi

Waziri wa Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Kimataifa, Mhe. Bernard K. Membe (Mb.) akimpokea Binti Mfalme wa Sweden, Mtukufu Victoria Lugrid Alice Desiree mara baada ya kuwasili kwenye Uwanja wa Ndege wa Kimataifa wa Julius Kambarage Nyerere, nchini Tanzania kwa ziara ya kikazi ya siku tatu kuanzia Tarehe 19 hadi 21 Machi, 2014. 
Mhe. Membe akiwa katika mazungumzo na Binti Mfalme wa Sweden, Mtukufu Victoria Lugrid Alice Desiree mara baada ya kuwasili nchini.
Mkurugenzi wa Idara ya Ulaya na Amerika katika Wizara ya Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Kimataifa, Balozi Dora Msechu kwa pamoja na wajumbe walioambatana na Binti Mfalme Victoria Ludrid Alice Desiree nchini wakifuatilia kwa karibu mazungumzo kati ya Mhe. Membe na Binti Mfalme wa Sweden, Mtukufu Victoria (hawapo Pichani).
Mkurugenzi Msaidizi wa Idara ya Ulaya na Amerika katika Wizara ya Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Kimataifa, Bi. Victoria Mwakasege pamoja na Afisa Mambo ya Nje Bi. Tunsume Mwangolombe wakati wa mazungumzo kati ya Waziri Membe na Binti Mfalme Victoria Ludrid Alice Desiree (hawapo pichani) 

Picha na Reginald Philip.

Monday, March 17, 2014

PRESS RELEASE




H.E. Jakaya Mrisho Kikwete, President of the United Republic of Tanzania has sent a congratulatory message to H.E Michael D. Higgins, President of Ireland on the occasion of the National Day of Ireland on 17th March 2014.

The message reads as follows.

“His Excellency Michael D. Higgins,

  The President of Ireland,

  Dublin, IRELAND.

Your Excellency and Dear colleague,

It is once again my pleasure and privilege to extend to you and through you to the Government and people of Ireland my heartfelt congratulations on the occasion of your country’s National Day.

Tanzania cherishes the good relations and co-operation that happily exist between our two countries. On this historic day, I take the opportunity to reaffirm my country’s commitment and desire to continue working with you and your Government in strengthening further the existing ties of friendship and co-operation for the mutual benefit of our two countries and peoples.


Please accept, Your Excellency, my best wishes for your continued good health and prosperity for the people of Ireland”.


ISSUED BY: THE MINISTRY OF FOREIGN AFFAIRS AND INTERNATIONAL CO-OPERATION, DAR ES SALAAM

17TH MARCH, 2014

Saturday, March 15, 2014

WAZIRI MEMBE AKUTANA NA MABALOZI WA NCHI ZA KIAFRIKA WANACHAMA WA JUMUIYA YA MADOLA


Mhe. Bernard Membe, Waziri wa Mambo ya Nje wa Tanzania kwenye mazungumzo na Mabalozi wa Nchi za Kiafrika Wanachama wa Jumuiya ya Madola Jijini London, Uingereza. 



Balozi wa Tanzania nchini Uingereza Mhe. Peter Kallaghe akimkaribisha Waziri wa Mambo ya Nje wa Tanzania na Mwenyekiti wa Kikosi Kazi cha Mawaziri wa Nchi Wanachama wa Jumuiya ya Madola Mhe.Bernard Membe kwenye mazungumzo mjini London, Uingereza.


Mhe. Bernard Membe (Mb.), Waziri wa Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Kimataifa ametoa wito kwa Nchi za Kiafrika Wanachama wa Jumuiya ya Madola kuunganisha nguvu na kuwa na sauti moja itakayotetea maslahi ya nchi za kiafrika kwenye jumuiya hiyo.

Mhe. Membe aliyasema hayo alipokutana na Mabalozi wa Nchi 12 za Kiafrika wanaowakilisha nchi zao kwenye Jumuiya ya Madola pembezoni mwa Mkutano wa Kikosi Kazi cha Mawaziri cha jumuiya hiyo kilichofanyika Jijini London Uingereza tarehe 13-14 Machi 2014.

Kwenye mazungumzo yao Mhe. Membe aliwakumbusha Mabalozi hao chimbuko la jumuiya hiyo na ushiriki wa nchi za kiafrika ili kutetea maslahi ya Waafrika na hatimaye kuvuna matunda ya ushiriki wa Waafrika kwenye Jumuiya ya Madola.

“Kama wanachama kutoka Bara la Afrika, ni wajibu wetu kushikamana na hata pale mwanachama mmoja anapotolewa au anapowekewa vikwazo vya ushiriki, tuungane na kuhakikisha mwanachama huyo anaondolewa vikwazo na hatimaye kurudi kwenye jumuiya. Tusipofanya hivyo hata sisi tutakuwa na tatizo” alisema Mhe. Membe.

Aliwaasa kuwa na sauti moja katika kutetea haki za ushiriki wa nchi za Kiafrika ndani ya jumuiya hiyo. Alisema namba ya nchi za Afrika kwenye jumuiya hiyo ni kubwa na hivyo ushiriki wa Waafrika lazima uwe wa kushindo.

Alisisitiza kuwa na sauti moja ya Waafrika kutakemea masuala yanayokuja kama shinikizo kutoka wanachama wa Nchi za Magharibi kama vile ndoa za jinsia moja, ambayo yanagusa dini, tamaduni, mila na desturi za Kiafrika. Alisema upepo wa shinikizo hilo unavuma kwa kasi kana kwamba kukubaliana na masuala hayo kutaondoa umaskini barani Afrika. Nchi za Kiafrika kwenye Jumuiya hiyo zina wajibu wa kushiriki kikamilifu kwa kusimamia agenda zitakazoleta maendeleo barani Afrika.

Ili kufanikisha wajibu huo, Mhe. Membe aliwahimiza Mabalozi hao kushiriki  kwenye chaguzi mbalimbali za jumuiya, kutoa taarifa kwa Wakuu wa Nchi na Serikali zao kutoka Makao Makuu ya Sekretarieti ya Jumuiya hiyo yaliyopo London Uingereza na mwisho kuhakikisha wanashiriki kikamilifu na kutoa sauti ya pamoja kwenye shuguli mbalimbali za Jumuiya badala ya kusubiri wengine wafanye maamuzi kwa niaba yao.

Kwa upande wao, mabalozi hao walimpongeza Mhe. Membe kwa kuchaguliwa kuwa Mwenyekiti wa Kikosi Kazi cha Mawaziri cha jumuiya hiyo kwa kipindi cha miaka miwili. Aidha walisifu jitihada za Tanzania kutetea maslahi ya nchi za Kiafrika wanachama wa jumuiya hiyo. 

Kwa upande mwingine walilalamikia uongozi wa Sekretarieti ya Jumuiya ya Madola kwa kutoshirikiana na mabalozi hao hususan kwenye maandalizi ya Vikao vya Wakuu wa Nchi na Serikali wanachama au baada ya vikao hivyo. Waliongeza kuwa kero za kiutendaji zinafanyiwa kazi juu juu tu na badala yake zinazua kero kubwa zaidi. Hivyo walimuomba Mhe. Membe kuwasaidia kwa kupitia Vikao vya Kikosi Kazi cha Mawaziri kuondoa changamoto hizo.

Ndani ya Jumuiya ya Madola kuna nchi za Kiafrika 18 ambapo 12 kati ya hizo zilizoshiriki kwenye mkutano huo ni; Mauritius, Cameroon, Seychelles, Namibia, South Africa, Uganda, Kenya, Mozambique, Ghana, Lesotho, Zambia na Tanzania. Jumuiya ya Madola ina jumla ya nchi 53.

Imetolewa na:
Kitengo cha Mawasiliano ya Serikali kwa Umma
Wizara ya Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Kimataifa


WAZIRI MEMBE AENDESHA KIKAO CHA MAWAZIRI WA NCHI ZA JUMUIYA YA MADOLA


Mhe. Bernard Membe akiendesha kikao cha 43 cha Kikosi Kazi cha Mawaziri wa Nchi Wanachama wa Jumiya ya Madola Jijini London Uingereza. 

Mawaziri wa Kikosi Kazi cha Nchi Wanachama wa Jumuiya ya Madola wakiwa kwenye mazungumzo na Waandishi wa Habari mara baada ya kumaliza Kikao cha 43 cha chombo hicho.




Kikao cha arobaini na tatu cha Kikosi Kazi cha Mawaziri wa Jumuiya ya Madola kimeipunguzia adhabu nchi ya Fiji na hivyo kuiruhusu kushiriki kwenye baadhi ya matukio ikiwemo michezo ya Jumuiya ya Madola ya mwaka 2014.

Kikao hicho kilichofanyika Jijini London Uingereza chini ya uenyekiti wa  Mhe. Bernard Membe (Mb.), Waziri wa Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Kimataifa wa Tanzania kilifikia uamuzi huo baada ya kupitia na kuridhishwa na hatua mbalimbali zilizochukuliwa na Fiji katika kujiandaa na uchaguzi mkuu ujao ikiwa ni jitihada za kutetea uanachama wake ndani ya jumuiya hiyo.

Akiongoza mjadala huo, Mhe. Membe alisifu hatua za makusudi zilizochukuliwa na nchi hiyo kama vile kushugulikia masuala ya haki za binadamu na utawala bora, kuanzisha daftari la kudumu la wapiga kura, kuandaa mazingira ya uwazi kwa ajili ya uchaguzi mkuu wa Septemba 2014 ikiwemo kuandaa mazungumzo na wadau mbalimbali wa siasa na aliyekuwa Waziri Mkuu aliyeingia kijeshi kujiuzulu na kugombea kama raia.

Akiendesha kikao hicho cha kwanza kama mwenyekiti wa chombo hicho muhimu, Mhe. Membe alisisitiza umuhimu wa kikosi kazi hicho kutekeleza majukumu yake bila urasimu na ubaguzi bali kwa kutoa fursa sawa za ushiriki wa nchi wanachama na kuzingatia misingi ya haki kwa manufaa ya wanachama wote.

Mhe. Membe pia aliwasisitizia mawaziri wenzake wanaotumikia chombo hicho kuwa makini na kuheshimu mila na desturi za nchi wanachama hususan zile za Kiafrika na kuepuka kushinikiza ajenda ambazo zinagusa dini, tamaduni na mila za nchi nyingi za kiafrika, kama vile ndoa za jinsia moja. Alisema kwa kufanya hivyo Jumuiya ya Madola itahatarisha muungano na mshikamano uliopo sasa ndani ya jumuiya hiyo.

Aidha Mhe. Membe alisema hazina kubwa ya Jumuiya ni wingi wa nchi wanachama na tamaduni na desturi mbalimbali zinazowakilishwa na wanajumuiya. Hivyo kuheshimu tamaduni zote ndio kutajenga heshima ya Jumuiya ya Madola kimataifa.

Akiwashukuru wajumbe wa kikosi kazi kama mwenyekiti, Mhe. Membe alisema jukumu la uenyekiti wa chombo hicho si dogo, lakini wajumbe wa chombo hicho wakiungana kwa pamoja na kwa msaada wa Sekretarieti ya Jumuiya ya Madola anahakika ndani ya miaka miwili ya uenyekiti wake Jumuiya hiyo itaendelea kusimamia misingi muhimu ya jumuiya hiyo bila kutetereka.

Mhe. Membe amewakilisha Tanzania kama Waziri mwenye dhamana kuanzia mwaka 2011 akiwa kama mjumbe, na mwaka 2013 Jijini Kolombo Sri Lanka alichaguliwa bila kupingwa kuwa mwenyekiti kwa miaka miwili. Waziri wa Mambo ya Nje wa New Zealand Mhe. Murray McCully alichaguliwa kuwa makamu mwenyekiti.

Ukiacha Tanzania na New Zealand, wajumbe wengine ni mawaziri wa Mambo ya Nje kutoka nchi saba ambazo ni Cyprus, Guyana, India, Pakistan, Sierra Leone, Visiwa vya Solomon na Sri Lanka ambao wanaingia kwa nafasi yao ya uenyekiti wa Mkutano wa Wakuu wa Nchi na Serikali za Jumuiya ya Madola.

Imetolewa na:
Kitengo cha Mawasiliano ya Serikali kwa Umma

Wizara ya Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Kimataifa

Wednesday, March 12, 2014

Katibu Mkuu amkabidhi Hati za kazi Mwakilishi wa Heshima wa Mauritius hapa nchini

Katibu Mkuu wa Wizara ya Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Kimataifa, Bw. John M. Haule kwa niaba ya Waziri wa Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Kimataifa, mhe. Bernard K. Membe (Mb.) akimkabidhi  Bw. Syed Nazre Abbas Rizvi Hati zinazomwezesha kufanya kazi kama Mwakilishi wa Heshima wa Mauritius nchini Tanzania. Makabidhiano hayo yalifanyika Ofisini kwa Katibu Mkuu tarehe 12 Machi, 2014. 
Bw. Syed Nazre Abbas Rizvi akisaini Kitabu cha Wageni mara baada ya kupokea kibali cha kuwa Mwakilishi wa Heshima wa Mauritius hapa nchini
Katibu Mkuu,  Bw.  Haule akizungumza na  Bw. Syed Nazre Abbas Rizvi.
Katibu Mkuu wa Wizara ya Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Kimataifa Bw. John Haule akiagana na Bw. Syed Nazre Abbas Rizvi mara baada ya kumaliza mazungumzo yao.



Picha na Reginald Philip

Tuesday, March 11, 2014

Mkutano wa Baraza la Mawaziri wa SADC waendelea nchini Malawi



Waziri wa Mambo ya Nje wa Malawi ambaye pia ni Mwenyekiti wa Baraza la Mawaziri wa SADC, Mhe. Ephraim Chiume (kushoto) akitoa hotuba ya ufunguzi wa Mkutano wa Baraza la Mawaziri wa SADC ulioanza jana tarehe 10 Machi, 2014 jijini Lilongwe, Malawi.

Mhe. Chiume akiendelea na hotuba ya ufunguzi, kushoto ni Katibu Mtendaji wa SADC, Mhe. Stergomena Tax

Waziri wa Fedha, Mhe. Saada Salum (Mb) mwenye ushungi. Waziri wa Nchi wa Serikali ya Zanzibar anayeshughulikia masuala ya Utawala Bora, Mhe. Mwinyi Haji Makame (kushoto) na Mhe. Janeth Mbene (Mb), Naibu Waziri wa Viwanda na Biashara wakiwa katika chumba cha mkutano.
Wajumbe wa mkutano.

Picha ya Pamoja ya Baraza la Mawazri  wa SADC. Waliokaa wa kwanza kutoka kushoto ni Waziri wa Fedha, Mhe. Saada Salum

Mhe Tax Aainisha mafanikio ya SADC katika kipindi cha mwaka 2013/2014

Na Ally Kondo, Lilongwe

Katibu Mtendaji wa Jumuiya ya Maendeleo ya Nchi za Kusini mwa Afrika (SADC), Mhe. Stergomena Tax aeleza mafanikio ya SADC katika kipindi cha utekelezaji wa bajeti na Mpango Kazi wa Jumuiya hiyo kwa mwaka 2013/2014. Mhe. Tax alitoa maelezo hayo mbele ya Mkutano wa Baraza la Mawaziri wa SADC ambao ni wa kwanza kushiriki tangu alipochaguliwa kushika wadhifa huo.  Mkutano wa Baraza la Mawaziri wa SADC unafanyika Lilongwe, Malawi na unatarajiwa kukamilika tarehe 11 Machi, 2014.

Mhe. Tax ambaye ni Mtanzania alisema kuwa SADC ilitekeleza kikamilifu na kwa mafanikio makubwa mpango kazi wa kusuluhisha mgogoro wa Madagascar. Hivyo alitumia fursa hiyo kuipongeza Madagascar, kurejeshewa uanachama wa SADC baada ya kufanya uchaguzi wa amani  kati ya mwezi Oktoba na Desemba, 2013 ambao umerejesha utawala wa Katiba katika nchi hiyo.
SADC pia katika kipindi hicho, ilituma timu za waangalizi wa uchaguzi katika chaguzi za Madagascar, Swaziland na Zimbabwe. Katika nchi zote hizo, waangalizi wa uchaguzi hao walikamilisha majukumu yao kwa ufanisi mkubwa.

Sanjari na hayo, SADC imeendelea kujadiliana na COMESA na EAC kuhusu ushirikiano wa kuanzisha Soko Huru la Pamoja baina ya nchi za jumuiya hizo. Awamu ya kwanza ya majadiliano hayo yanatarajiwa kukamilika mwaka 2015.

Aidha, SADC inajivunia kuanza kwa utekelezaji wa Itifaki ya Jinsia na Maendeleo katika nchi wanachama. Itifaki hiyo imeanza kutekelezwa baada ya theluthi mbili ya nchi za SADC kuidhinisha Itifaki hiyo.
SADC pia inakamilisha Rasimu ya Itifaki kuhusu kuanzisha upya Mahakama ya SADC.  

Katika orodha hiyo ya mafanikio, SADC pia imeweza kuwa na chombo cha kuandaa miradi ya maendeleo, chombo ambacho kitasaidia kubuni miradi makini itakayoweza kupata fedha kutoka taasisi za fedha. Sambamba na hili, SADC imeandaa Mpango Mkuu wa miradi ya miundombinu.

Katika mkutano huo, Mhe. Tax alitaja pia maeneo yatakayopewa kipaumbele katika Mwaka wa Fedha 2014/2015. Maeneo hayo ni pamoja na: kuimarisha soko huru katika nchi za SADC; majadiliano ya utatu wa kuanzisha Soko huru la pamoja la nchi za EAC, COMESA na SADC;  maendeleo ya viwanda na maendeleo ya miundombinu katika ushirikiano wa utatu (EAC,SADC, COMESA) na utekelezaji wa Mpango Mkuu wa Kikanda wa Maendeleo ya Miundombinu.

Vipaumbele vingine ni: utekelezaji wa mikakati ya kikanda ili kuboresha upatikanaji wa uhakika wa chakula (food security); kuhamasisha na kujenga amani pamoja na kuimarisha demokrasia na utawala bora katika Kanda ya SADC; na kutekeleza mikakati ya pamoja ya kukabiliana na ugonjwa wa UKIMWI.