Monday, August 24, 2015

Katibu Mkuu akutana na Mwakilishi Maalum wa Marekani Eneo la Maziwa Makuu

Katibu Mkuu wa Wizara ya Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Kimataifa, Balozi Libarata Mulamula akizungumza na Mwakilishi Maalum wa Marekani katika eneo la Nchi za Maziwa Makuu (ICGLR), Mhe. Thomas Perriello alipofika Wizarani kwa ajili ya  mazungumzo kuhusu masuala mbalimbali katika eneo hilo.  
Ujumbe ulioambatana na Mhe. Perriello wakifuatilia mazungumzo kati ya Balozi Mulamula na Mhe. Pirriello (hawapo pichani) akiwemo Balozi wa Marekani nchini, Mhe. Mark Childress (kulia). 
Mhe. Perriello akizungumza huku Balozi Mulamula akimsikiliza
Mkurugenzi wa Idara ya Ulaya na Amerika katika Wizara ya Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Kimataifa, Balozi Joseph Sokoine (wa pili kulia) kwa pamoja na Kaimu Mkurugenzi wa Idara ya Ushirikiano wa Kikanda, Bw. Innocent Shiyo (kushoto)  wakifuatilia mazungumzo kati ya Balozi Mulamula na Mhe. Perriello (hawapo pichani). Wengine katika picha ni Bi. Grace Martin (wa pili kushoto), Afisa Mambo ya Nje Mwandamizi na Bi. Shamim Khalfan (kulia), Afisa Mambo ya Nje. 
Mazungumzo yakiendelea
Maafisa Mambo ya Nje wakifuatilia mazungumzo yaliyokuwa yakiendelea kati ya Mhe. Perriello na Balozi Mulamula (hawapo pichani). Kutoka kushoto ni Bi. Redemptor Tibaigana, Bw. Suleiman Saleh na Afisa aliyeambatana na Mhe. Perrielo
Balozi wa Marekani nchinui, Mhe. Childress (wa kwanza kushoto) akimtambulisha Mhe. Perriello (Katikati) kwa Katibu Mkuu wa Wizara ya Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Kimataifa,  Balozi Liberata Mulamula (kulia)
 Balozi Mulamula akiwa  akiwa katika picha ya pamoja na Mhe. Perriello mara baada ya kukamilisha mazungumzo yao.


Picha na Reginald Philip.

Friday, August 21, 2015

Rais Kikwete amuapisha Balozi mpya wa Tanzania Nchini Zimbabwe.

Rais Jakaya Mrisho Kikwete, akimuapisha Balozi mpya wa Tanzania nchini Zimbabwe, Mhe. Luteni Jenerali Charles Lawrence Makakala katika hafla iliyofanyika tarehe 21-08-2015 Ikulu Jijini Dar es Salaam. Kabla ya Uteuzi huo, Luteni Jenerali Makakala, alikua Mkuu wa Chuo cha Ulinzi cha Taifa cha Jeshi la Wananchi wa Tanzania (JWTZ) Kunduchi Jijini Dar es Salaam.
 Baadhi ya viongozi waandamizi wa Jeshi la Ulinzi la Wananchi wa Tanzania (JWTZ), Mabalozi na Maofisa kutoka Wizara ya Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Kimataifa pamoja na familia ya Balozi Mteule Makakala wakishuhudia kiapo.
 Rais Kikwete akimkabizi Balozi Makakala nyaraka na vitendea kazi mbalimbali kama muongozo wa kazi yake mpya ya Ubalozi.
 Familia ya Balozi mpya wa Tanzania nchini Zimbabwe, Mhe. Luteni Jenerali Charles Lawrence Makakala  wakishuhudia uapisho huo.

 Mheshimiwa Balozi Makakala akisaini kiapo hicho mbele ya Mheshimiwa Rais, Ikulu Jijini Dar es Salaam.

Rais Kikwete akiwa katika picha ya pamoja na viongozi waandamizi wa Jeshi la Wananchi wa Tanzania (JWTZ) pamoja na Balozi mpya wa Tanzania nchini Zimbabwe, Mhe. Luteni Jenerali Charles Lawrence Makakala, muda mfupi baada ya kula kiapo Ikulu Jijini Dar es Salaam.

Rais Kikwete akiwa katika picha ya pamoja na Naibu Waziri wa Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Kimataifa Mhe. Dkt. Mahadhi Juma Maalim (Mb), Mabalozi na Maofisa kutoka Wizara hiyo, pamoja na Balozi mpya wa Tanzania nchini Zimbabwe, Mhe.  Luteni Jenerali Charles Lawrence Makakala, baada ya kiapo katika hafla iliyofanyika Ikulu jijini Dar es Salaam Tarehe 21-08-2015.

Rais Kikwete akiwa katika picha ya pamoja na familia ya Balozi mpya wa Tanzania nchini Zimbabwe, Mhe. Luteni Jenerali Charles Lawrence Makakala.
Rais Kikwete akibadilishana mawazo na Balozi Mteule Makakala (kushoto kwa Rais) na Naibu Waziri wa Mambo ya Nje, Mhe. Dkt. Mahadhi Juma Maalim (Mb.) na Katibu Mkuu Kiongozi Balozi Ombeni Sefue.
 Rais Kikwete akibadilishana mawazo na Balozi mpya wa Tanzania nchini Zimbabwe, Mhe. Luteni Jenerali Charles Lawrence Makakala, muda mfupi baada ya kumuapisha kuwa Balozi.
 Rais Kikwete akibadilishana mawazo na Viongozi waandamizi wa Jeshi la Wananchi wa Tanzania (JWTZ) na Balozi mpya wa Tanzania nchini Zimbabwe, Mhe. Luteni Jenerali Charles Lawrence Makakala, Ikulu jijini Dar es Salaam.
 Mabalozi na Maofisa kutoka Wizara ya Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Kimataifa, nao wakibadilishana mawazo mara baada ya hafla hiyo, Ikulu jijini Dar es Salaam.
Mkurugenzi wa Idara ya Asia na Australia wa Wizara ya Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Kimataifa, Balozi Mbelwa Kairuki (Kulia) na Mkuu wa Kitengo cha Mawasiliano Serikalini na msemaji wa Wizara Bi Mindi Kasiga wakimpongeza Balozi Mpya wa Tanzania nchini Zimbabwe, Mhe. Luteni Jenerali Charles Lawrence Makakala, mara baada ya kuapishwa Ikulu jijini Dar es Salaam.
=========================
PICHA NA REUBEN MCHOME.

Rais Kikwete apokea Hati za Utambulisho za Mabalozi wa India na Denmark

Mhe. Jakaya Mrisho Kikwete, Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania akipokea Hati za Utambulisho kutoka kwa Balozi wa Denmark nchini Mhe. Einar Hebogard Jensen, Ikulu jijini Dar es Salaam leo Tarehe 21-08-2015.

Balozi mpya wa Denmark hapa nchini Mhe. Einar Hebogard Jensen, akiwasili Ikulu jijini Dar es Salaam na kupokelewa na Mnikulu Bw. George Bwando, anayeshuhudia (kushoto) ni Mkuu wa Itifaki Balozi Mohamed Juma Maharage.

Mhe. Einar Hebogard akipokea heshima kutoka kwa Bendi ya Jeshi la Polisi (hawapo pichani), kwa kuimbiwa nyimbo za Taifa za Denmark na Tanzania.

Mhe. Balozi Hebogard akiweka saini kitabu cha wageni Ikulu Jijini Dar es Salaam, muda mfupi kabla ya kuwasilisha hati zake za utambulisho kwa Rais Kikwete.
Rais Kikwete akimpokea Balozi Hebogard baada ya kukabidhi hati zake za utambulisho.

Naibu Waziri wa Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Kimataifa Mhe. Dkt. Mahadhi Juma Maalim (Mb.), akisalimiana na Balozi mpya wa Denmark hapa Nchini.

Mkurugenzi wa Idara ya Ulaya na Amerika Wizara ya Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Kimataifa, Balozi Joseph Sokoine, akisalimiana na Balozi Hebogard.

Rais Kikwete akizungumza na Balozi Hebogard mara baada ya kuwasilisha hati zake za utambulisho.

Picha ya Pamoja.
========
Balozi wa India

Msafara wa Balozi mpya wa India ukiingia katika viwanja vya Ikulu jijini Dar es Salaam, tayari kwa kuwasilisha hati za utambulisho kwa Mhe. Jakaya Mrisho Kikwete, Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania.
 Balozi mpya wa India Nchini, Mhe. Sandeep Arya, akipokea heshima kutoka kwa Bendi ya Jeshi la Polisi, kwa kuimbiwa Nyimbo za Taifa za India na Tanzania.
 Mhe. Sandeep Arya, akiweka saini kitabu cha wageni Ikulu Jijini Dar es Salaam, muda mfupi kabla ya kuwasilisha hati zake za utambulisho kwa Rais Kikwete.
 Rais Kikwete akipokea Hati za Utambulisho za Mheshimiwa Balozi Sandeep Arya.
 Naibu Waziri wa Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Kimataifa Mhe. Dkt. Mahadhi Juma Maalim (Mb.), akisalimiana na Balozi mpya wa India hapa Nchini.
Mkurugenzi wa Idara ya Asia na Australia wa Wizara ya Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Kimataifa, Balozi Mbelwa Kairuki, akisalimiana na Balozi mpya wa India hapa Nchini Mhe. Sandeep Arya.
Mhe. Sandeep Arya, akiagana na Mnikulu tayari kwa kuondoka viwanja vya Ikulu, mara baada ya kuwasilisha hati zake za utambulisho kwa Rais Kikwete.

Thursday, August 20, 2015

Matukio mbalimbali yaendelea kuelekea maadhimisho ya miaka 70 ya Umoja wa Mataifa

Mkurugenzi Idara ya Ushirikiano wa Kimataifa, Balozi Celestine Mushy (kushoto) kwa pamoja na  Mratibu Mkazi wa Mashirika ya Umoja wa Mataifa na Mwakilishi wa Shirika la Maendeleo la Umoja wa Mataifa (UNDP) nchini, Alvaro Rodriguez wakichanganya saruji, kokoto na mchanga ili kupata zege kwa ajili ya kuweka Jiwe la  Msingi ikiwa ni uzinduzi wa kuanza kwa ujenzi wa vyoo 22 kwenye Shule ya Msingi Kiboriloni, Mkoani Kilimanjaro. Uzinduzi huo ni tukio mojawapo kuelekea maadhimisho ya miaka 70 ya kuanzishwa kwa Umoja wa Mataifa  Ujenzi huo umedhaminiwa na UNDP. 
Bw. Alvaro akiweka jiwe la msingi  kuzindua kuanza kwa ujenzi wa  Vyoo hivyo
Balozi Mushy naye akiweka tofali katika msingi huo 
Mwakilishi wa UNFPA Dkt. Nathalia Kanem naye akimpatia fundi tofali la ujenzi wa vyoo hive
Mkurugenzi wa Idara ya Ushirikiano wa Kimataifa, Balozi Celestine Mushy (wa kwanza mbele) na Mratibu Mkazi wa Mashirika ya Umoja wa Mataifa na Mwakilishi wa Shirika la Maendeleo la Umoja wa Mataifa (UNDP) nchini, Alvaro Rodriguez,kwa pamoja wakimimina zege kwenye msingi wa Vyoo vinavyojengwa katika Shule ya Msingi ya Kiboriloni
Mratibu Mkazi wa Mashirika ya Umoja wa Mataifa na Mwakilishi wa Shirika la Maendeleo la Umoja wa Mataifa (UNDP) nchini, Alvaro Rodriguez, akizungumza katika uzinduzi wa Ujenzi wa vyoo 22 vinavyojengwa katika shule ya msingi ya Kiboriloni
Juu na Chini ni Balozi Mushy akizungumza na wanafunzi wakati wa Uzinduzi wa Ujenzi wa vyoo 22 katika Shule hiyo
Wanafunzi wa Shule hiyo wakionekana kuwa na furaha na matumaini baada ya uzinduzi wa Vyoo hivyo vya Shule yao.
Sehemu ya Uongozi wa Shule ya Msingi ya Kiboriloni
Wananchini na waalimu wa shule hiyo wakisikiliza kwa makini 
Dkt. Kanem akizungumza kwenye uzinduzi wa Ujenzi wa vyoo 22 vya shule ya Msingi Kiboriloni
Mwakilishi wa UNFPA Dkt. Nathalia Kanem (kulia) akifurahia jambo na Balozi Mushy (katikati), pamoja na Bw. Alvarp
Balozi Mushy akimtambulisha Bwa. Alvaro kwa waalimu wa shule ya msingi ya kiboriloni waliojipang kumpokea  
Balozi Celestine Mushy akiwa katika picha ya pamoja na Bw. Alvaro
Bwa. Alvaro (wa nne kutoka kulia) na Balozi Celestine Mushy wakiwa katika picha ya pamoja na Uongozi na waalimu wa Shule ya Msingi ya Kiboriloni
Mkurugenzi wa Idara ya Ushirikiano wa Kimataifa, Balozi Celestine Mushy akiwa na Mratibu Mkazi wa Mashirika ya Umoja wa Mataifa na Mwakilishi wa Shirika la Maendeleo la Umoja wa Mataifa (UNDP) nchini, Alvaro Rodriguez, wakiwa katika picha ya pamoja na wanafunzi wa Shule ya Msingi ya Kiboriloni

Picha na Reginald Philip