Wednesday, January 11, 2017

Balozi wa Cuba nchini Tanzania aagwa baada ya kumaliza muda wake



Waziri wa Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki Mhe. Balozi Dkt. Augustine Mahiga akisoma hotuba wakati wa hafla fupi ya kumuaga Balozi wa Cuba Nchini Tanzani Mhe. Jorge Luis Lopes Tormo iliyofanyika katika Hoteli ya Southern Sun Jijini Dar Salaam

Mkuu wa Kitengo cha Mawasiliano ya Serikali na Msemaji wa Wizara Bi. Mindi Kasiga akiongea katika hafla hiyo

Toka kulia ni; Katibu Mkuu wa Chama cha Mapinduzi (CCM) Comrade Abdulahaman Kinana, Waziri wa Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki Mhe. Balozi Dkt. Augustine Mahiga, Balozi wa Cuba Nchini anayemaliza muda wake Mhe. Jorge Luis Lopes Tormo, Mkurugenzi wa Idara ya Marekani na Ulaya Balozi Joseph Sokoine, na Mkurugenzi wa Shirika la Maendeleo la Taifa Bw.Mlingi E. Mkucha wakifurahia jambo katika hafla hiyo
Mkuu wa Kitengo cha Mawasiliano ya Serikali na Msemaji wa Wizara Bi. Mindi Kasiga akifuatilia jambo




Balozi wa Cuba Nchini anayemaliza muda wake Mhe. Jorge Luis Lopes Tormo akiongea katika hafla hiyo

Picha ya pamoja

Tuesday, January 10, 2017

Waziri Mahiga amuaga Waziri wa Mambo ya Nje wa China Mhe. Wang

Waziri wa Mambo ya Nje na Ushrikiano wa Afrika Mashariki, Mhe.Balozi Dkt. Augustine Mahiga akijadili jambo na mgeni wake Waziri wa Mambo ya Nje wa China, Mhe. Wang Yi katika Uwanja wa Ndege wa Kimataifa wa Nyerere Jijini Dar es Salaam, wakati akijiandaa kuondoka baada ya kumaliza ziara yake ya kikazi nchini. Wa kwanza kulia ni Balozi wa China nchini Tanzania Mhe. Lu Younqing 
Waziri Mahiga akimsikiliza Waziri wa Mambo ya Nje wa China Mhe. Wang Yi


Waziri Mahiga na Waziri Wang Yi wakifurahia jambo wakati wa mazungumzo

Waziri wa Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki Mhe.Balozi Dkt. Augustine Mahiga akiagana na Waziri wa Mambo ya Nje wa China Mhe.Wang Yi katika Uwanja wa Ndege wa Kimataifa wa Nyerere wakati akiondoka nchini mara baada ya kumaliza ziara yake ya kikazi 

Waziri Mhe. Balozi Dkt. Mahiga Mkurugenzi wa Idara ya Asia na Australasia Balozi Mbelwa Kairuki (katikati kulia) na Makuu wa Kitengo cha Mawasiliano ya Serikali na Msemaji wa Wizara Bi. Mindi Kasiga wakipunga mikono kumuaga Warizi Mhe. Wang wa China. 

Monday, January 9, 2017

Waziri wa Mambo ya Nje wa China awasili nchini kwa ziara ya kikazi

Waziri wa Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki, Dkt. Augustine Mahiga akimpokea Waziri wa Mambo ya Nje wa Jamhuri ya Watu wa China, Mhe. Wang Yi (wa kwanza kulia) mara baada ya kuwasili katika Uwanja wa Ndege wa Kimataifa wa Juliusi Nyerere. Waziri Wang Yi yupo nchini kwa ziara ya siku moja.
Waziri Mahiga pamoja na Balozi Mbelwa Kairuki, Mkurugenzi wa Idara ya Asia na Australasia wakimtazama Waziri Wang Yi wakati akiteremka kwenye ndege aliyowasili nayo.
Waziri Mahiga akizungumza na mgeni wake Waziri Wang Yi mara baada ya kuwasili Uwanja wa Ndege wa Kiamataifa wa Julius Nyerere
Balozi Kairuki (katikati), Balozi wa China nchini Tanzania Lu Younqing (wa kwanza kushoto), pamoja na Afisa Mambo ya Nje, Bw. Humphrey Shangarai (wa kwanza kulia) nao wakiwa katika mazungumzo hayo
Sehemu ya ujumbe alioambatana nao Mhe. Waziri Wang Yi

Friday, January 6, 2017

Waziri Mahiga akutana kwa mazungumzo na Balozi wa Syria nchini

Waziri wa Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki Dkt. Augustine Mahiga(Mb.) amekutana na kufanya mazungumzo na Balozi wa Syria nchini Tanzania Mhe. Abdulmonem Annan (kushoto) mwenye makazi yake nchini Kenya. Katika mazungumzo yao yaliyojikita katika kuboresha mahusiano kati ya Tanzania na Syria ambayo ni ya muda mrefu  pamoja na  Balozi Annan kutumia fursa hiyo kujitambulisha rasmi kwa Waziri Mahiga. 
Sehemu ya Watumishi wa Wizara ya Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki wakifuatilia mazungumzo hayo. 
Balozi Annan akimweleza jambo Mhe. Mahiga wakati wa mazungumzo hayo.
Mazungumzo yakiendelea

Thursday, January 5, 2017

Waziri wa Mambo ya Nje wa China kufanya ziara nchini

Mkuu wa Kitengo cha Mawasiliano na Msemaji wa Wizara ya Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki,  Bi. Mindi Kasiga akizungumza katika mkutano na waandishi wa habari kuhusu  ziara ya Waziri wa Mambo ya Nje wa Jamhuri ya Watu wa China atakayoifanya hapa nchini tarehe 09 Januari, 2017.Mkutano huo umefanyika katika Ukumbi wa  Mikutano wa Kimataifa wa JNICC Jijini Dar es Salaam leo.
Sehemu ya Waandishi wa Habari wakifuatilia kwa makini wakati Bi. Mindi Kasiga (hayupo pichani) akiendelea kuzungumza nao.
Sehemu nyingine ya Waandishi wa Habari wakifuatilia mkutano.
Mkutano na Waandishi wa Habari ukiendelea.



TAARIFA KWA VYOMBO VYA HABARI 
Ziara ya Waziri wa Mambo ya Nje wa China nchini
Waziri wa Mambo ya Nje wa Jamhuri ya Watu wa China, Mhe. WANG Yi anatarajiwa kufanya ziara ya kikazi nchini tarehe 09 Januari 2017. Mhe. Waziri Wang Yi atapokelewa na mwenyeji wake Waziri wa Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki, Mhe. Balozi Dkt. Augustine Mahiga.
  
Madhumuni ya  ziara hiyo ni kukuza mahusiano mazuri na ya kihistoria baina ya China na Tanzania ambayo yamedumu kwa zaidi ya miaka hamsini tangu kuanzishwa kwake pamoja ‎na kuangalia maeneo mapya ya ushirikiano wa kiuchumi baina ya Tanzania na China.
Wakati wa ziara hiyo Mhe. Wang Yi atakutana na Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mhe. Dkt. John Pombe Joseph Magufuli kwa lengo la kumsalimia. 
Aidha, Mhe. Wang Yi atafanya mazungumzo rasmi na Mhe. Dkt. Mahiga kuhusu masuala mbalimbali ya ushirikiano baina ya Tanzania na China na ushirikiano wa kimataifa.
Itakumbukwa kwamba mwezi Desemba 2015 kwenye Mkutano wa Wakuu wa Nchi za Afrika na China, China iliichagua Tanzania kuwa miongoni mwa nchi nne Barani Afrika zitakazowezeshwa kupiga hatua kwenye maendeleo ya viwanda. Kupitia mpango huo inatarajiwa viwanda takriban 200 vitajengwa au kuwekezwa nchini kutoka China kabla ya mwaka 2020.
Mpango huu unaenda sambamba na Mpango wa Taifa wa Maendeleo wa mwaka 2016/2020 na pia ahadi za Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Mhe. Dkt. John Pombe Joseph Magufuli ya kujenga Tanzania ya viwanda. Ni matarajio yetu ni kuwa, Watanzania takriban laki mbili watanufaika na ajira kupitia mpango huu mahsusi wa kuendeleza viwanda.
Mbali na mpango wa uendelezaji wa viwanda, viongozi hawa wawili watazungumzia miradi mingine ya miundombinu ambapo China imeahidi kuisadia Tanzania ikiwa ni pamoja na maboresho makubwa ya Reli ya TAZARA; Ujenzi wa Bandari ya Bagamoyo pamoja na ujenzi wa Reli ya Kati.
Aidha, Mhe. Wang anatarajiwa kuzungumza na Mwenyeji wake kuhusu masuala ya ushirikiano wa kimataifa ikiwa ni pamoja na mageuzi ya Baraza la Usalama la Umoja wa Mataifa ambapo China inaunga mkono msimamo wa Afrika na wa Tanzania wa kutaka Afrika ipewe viti viwili vya kudumu kwenye Baraza hilo na kura ya turufu. 
Vilevile viongozi hao watazungumzia masuala ya amani na usalama katika eneo la Afrika Mashariki pamoja na eneo la Bahari ya Kusini mwa China.
Mazungumzo hayo yatafuatiwa na Mkutano wa Mawaziri na Vyombo vya Habari (Joint Press Conference) ambapo wataeleza makubaliano waliyofikia kwenye mazungumzo yao.
-Mwisho-
Imetolewa na:
Kitengo cha Mawasiliano ya Serikali,
Wizara ya Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki, Dar es Salaam
05 Januari, 2017



Wednesday, January 4, 2017

Waziri Mahiga akutana kwa mazungumzo na Balozi wa China nchini

Waziri wa Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki, Mhe. Dkt. Augustine Mahiga akizungumza na Balozi wa China nchini, Mhe. Lu Youqing alipofika Wizarani kwa ajili ya mazungumzo kuhusu ushirikiano kati ya Tanzania na China.
Sehemu ya Ujumbe kutoka Wizara ya Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki wakifuatilia mazungumzo kati ya Mhe. Mahiga na Balozi Lu (hawapo pichani). Kutoka kushoto ni Mkurugenzi wa Idara ya Asia na Australasia, Balozi Mbelwa Kairuki, Mkuu wa Kitengo cha Mawasiliano ya Serikali, Bi. Mindi Kasiga, Maafisa Mambo ya Nje, Bw. Emmanuel Luangisa na Bw. Benedict Msuya.
Ujumbe kutoka Ubalozi wa China
Mhe. Dkt. Mahiga akiagana na  Balozi Lu mara baada ya mazungumzo yao.

Monday, January 2, 2017

PUBLIC ANNOUNCEMENT






PUBLIC ANNOUNCEMENT

Visa exemption for Tanzanian diplomatic and official/service passport holders 

The United Republic of Tanzania and the Republic of India have started to implement the agreement signed by the two Governments on 10 July, 2016 on visa exemption for each other’s diplomats and official/service passport holders. 

The agreement became effective on 26 December 2016. 

The agreement states that, holders of diplomatic and official/service passports of the two countries do not require visa to travel to the other country from 26 December 2016, except when employed in each other’s country.

Issued by: Government Communication Unit,
Ministry of Foreign Affairs and East African Cooperation, 
Dar es Salaam.
02nd January, 2017

Friday, December 30, 2016

Katibu Mkuu wa Mambo ya Nje akutana na Naibu Balozi wa China nchini

Katibu Mkuu wa Wizara ya Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki, Balozi Dkt. Aziz Mlima akizungumza na Naibu Balozi wa China nchini, Bw. Gou Haudong alipofika Wizarani kwa ajili ya kuzungumzia masuala mbalimbali ya ushirikiano kati ya Tanzania na China.
Sehemu ya ujumbe kutoka Ubalozi wa China nchini ukifuatilia mazungumzo kati ya Balozi Mlima na Bw. Gou (hawapo pichani)

Kaimu Mkurugenzi wa Idara ya Asia na Australasia katika Wizara ya Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki, Bw. Emmanuel Luangisa (kushoto) akiwa na Bw. Humphrey Shangarai, Afisa Mambo ya Nje nao wakifuatilia mazungumzo
Bw. Gou akisisitiza jambo wakati wa mazungumzo na Balozi Mlima.

Thursday, December 29, 2016

TAARIFA KWA VYOMBO VYA HABARI




Ufafanuzi kuhusu taarifa za kukamatwa kwa Watanzania wanaodaiwa ni majasusi nchini Malawi

Baadhi ya Vyombo vya habari vya hapa nchini hivi karibuni vilitoa taarifa kuwa, Watanzania 8 wanaodaiwa kuwa ni majasusi wa Serikali ya Tanzania wamekamatwa nchini Malawi kwa tuhuma za kuingia kwenye mgodi wa urani wa Kayerekera uliopo nchini Malawi kinyume cha sheria. 
Taarifa hiyo kwa mara ya kwanza ilitolewa na chombo cha habari cha Malawi ambacho kilidai kuwa watu hao wametumwa na Serikali ya Tanzania ili kuchunguza kama Serikali ya Malawi inatengeneza silaha za nyuklia kwa kutumia madini ya urani ya kutoka mgodi huo.

Kufuatia taarifa hizo, Wizara kupitia Ubalozi wa Tanzania nchini Malawi ulifuatilia ili kubaini ukweli wa tukio hilo. Baada ya kufuatilia ilibainika kuwa ni kweli Watanzania 8 kutoka taasisi ya CARITAS iliyo chini ya Kanisa Katoliki Songea mkoani Ruvuma walikamatwa na vyombo vya usalama katika Wilaya ya Karonga ambayo inapakana na Wilaya ya Kyela.  Watanzania hao mara moja walifunguliwa kesi kwa kutuhumiwa kufanya kosa la jinai la kuingia eneo la mgodi bila kibali (criminal trespass).

Ubalozi uliwasiliana na Taasisi ya CARITAS kutaka kufahamu madhumuni ya watu hao kufanya ziara nchini Malawi. Ubalozi ulielezwa kuwa ziara hiyo ilikuwa ni ya mafunzo ambapo walitaka kufahamu juu ya madhara yatokanayo na machimbo ya madini ya urani. Watanzania hao kwa sasa wapo katika gereza kuu la Mzuzu hadi kesi yao itakapotajwa tena tarehe 04 Januari 2017.

Ubalozi unaendelea kufanya mawasiliano na Kanisa Katoliki Songea ili kupata maelezo zaidi kuhusu ziara ya watu hao kwa madhumuni ya kuyawasilisha mamlaka husika ili watuhumiwa waweze kutolewa.
Aidha, Wizara kupitia Ubalozi umebaini kuwa CARITAS iliruhusu watu hao kufanya ziara nchini Malawi bila kupata kibali kutoka mamlaka husika na bila kutoa taarifa Ofisi ya Ubalozi kuhusu ziara hiyo. 

Aidha, kipindi cha kufanya ziara hiyo nchini Malawi hakikuwa muafaka kwa kuwa watumishi wa Serikali ya Malawi wanakuwa katika likizo ya mwaka kuanzia tarehe 22 Desemba hadi 03 Januari 2017. Hii inakwamisha juhudi za kuwafuatilia watu hao ikiwa ni pamoja na kukwama kwa maombi ya kibali cha kuwatembelea watu hao tarehe 28 Desemba 2016.

Wizara inatoa wito kwa mara nyingine kwa taasisi za dini, vyuo vya elimu na watu binafsi kuomba vibali na kufuata sheria za nchi nyingine wanapofanya ziara za mafunzo au ziara nyinginezo ikiwa ni pamoja na kuwasiliana na ofisi za Balozi zetu kwa madhumuni ya kufahamishwa taratibu zinazotakiwa kufuatwa kabla ya kufanya ziara husika ili kuepuka usumbufu unaoweza kujitokeza. 

Wizara, kupitia Ubalozi wa Tanzania nchini Malawi unaendelea na jitihada za kuhakikisha kuwa suala hilo linapatiwa ufumbuzi kwa haraka.

Imetolewa na:
Kitengo cha Mawasiliano ya Serikali,
Wizara ya Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki
Dar es Salaam, 29 Desemba  2016.