Monday, January 9, 2017

Waziri wa Mambo ya Nje wa China awasili nchini kwa ziara ya kikazi

Waziri wa Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki, Dkt. Augustine Mahiga akimpokea Waziri wa Mambo ya Nje wa Jamhuri ya Watu wa China, Mhe. Wang Yi (wa kwanza kulia) mara baada ya kuwasili katika Uwanja wa Ndege wa Kimataifa wa Juliusi Nyerere. Waziri Wang Yi yupo nchini kwa ziara ya siku moja.
Waziri Mahiga pamoja na Balozi Mbelwa Kairuki, Mkurugenzi wa Idara ya Asia na Australasia wakimtazama Waziri Wang Yi wakati akiteremka kwenye ndege aliyowasili nayo.
Waziri Mahiga akizungumza na mgeni wake Waziri Wang Yi mara baada ya kuwasili Uwanja wa Ndege wa Kiamataifa wa Julius Nyerere
Balozi Kairuki (katikati), Balozi wa China nchini Tanzania Lu Younqing (wa kwanza kushoto), pamoja na Afisa Mambo ya Nje, Bw. Humphrey Shangarai (wa kwanza kulia) nao wakiwa katika mazungumzo hayo
Sehemu ya ujumbe alioambatana nao Mhe. Waziri Wang Yi

No comments:

Post a Comment

Note: Only a member of this blog may post a comment.