Friday, January 27, 2017

Watanzania 14 washiriki maonesho ya Sanaa nchini Kenya

Maonesho ya sanaa za uchoraji ya Wasanii 14 kutoka Tanzania yameanza rasmi tarehe 25 Januari 2017 kwenye ukumbi wa maonesho wa Village Market Nairobi.
Watu waliotembelea maonesho hayo siku ya kwanza ni pamoja na Mabalozi na wadau mbalimbali wa sanaa kutoka Kenya na nchi za nje. Maonesho hayo yatachukua wiki mbili.
Kaimu Balozi wa Tanzania nchini Kenya, Bi. Talha Mohamed Waziri (kulia) akimkaribisha Balozi wa Msumbiji kwenye maonesho hayo.

Ofisa wa Ubalozi wa Venezuela Nairobi, Jose Gregorio Ayila Torres (katikati) akibadilishana mawazo na Kaimu Balozi wa Tanzania (kulia). Kushoto ni mmoja wa wasanii wa Tanzania, Raza Mohamed.
Raia wa Uswisi waliofika kwenye maonesho.

Wapenda sanaa wa Kenya wakikagua kazi za wasanii wa Tanzania

Wadau wa sanaa wakifurahia maonesho



No comments:

Post a Comment

Note: Only a member of this blog may post a comment.