Tuesday, January 24, 2017

Rais Magufuli ampokea Rais wa Uturuki Ikulu



Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mhe.Dkt John Pombe Magufuli  na mgeni wake Rais wa Jamhuri ya Uturuki Mhe. Recep Tyyip Erdogan wakiwasalimia wananchi walijiotokeza kwenye hafla ya kumkaribisha katika viwanja vya Ikulu Jijini Dar es Salaam

Rais wa Jamhuri ya Uturuki Mhe. Recep Tyyip Erdogan akikabidhiwa ua na mtoto, Amara Asenath Tarimo wakati wa hafla ya kumkaribisha Rais huyo iliyofanyika Ikulu Jijini Dar es Salaam

Rais Mhe. Dkt Magufuli na Rais wa Jamhuri ya Uturuki Mhe. Erdogan wakiwa wamesimama wakati wimbo wataifa ukipigwa
Rais Mhe.Erdogan akikagua gwaride mara baada ya kuwasili Ikulu Jijini Dar es Salaam


Rais Mhe. Erdogan akipiga moja ya ngoma zilikuwepo wakati wa hafla ya mapokezi ya kumkaribisha Ikulu Jijini Dar es Salaam


Waziri wa Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki, Mhe. Balozi Dkt. Augustine Mahiga na Katibu Mkuu Kiongozi, Balozi Eng. John Kijazi wakifuatilia mazungumzo yaliyokuwa yakindelea 

Rais Mhe. Dkt. John Pombe Magufuli akizungumza na hadhira waliojitokeza kwenye ukumbi wa Mikutano Ikulu Jijini Dar es Salaam

No comments:

Post a Comment

Note: Only a member of this blog may post a comment.