Sunday, January 21, 2018

Mabalozi watano wawasilisha Nakala za Hati za Utambulisho


Balozi Mteule wa Ugiriki
Balozi Mteule wa Ugiriki nchini Tanzania mwenye makazi yake Nairobi, Kenya, Mhe. Konstantinos Moatsos (kushoto) akisalimiana na Waziri wa Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki,Mhe. Balozi Dkt. Augustine Mahiga kabla ya kuwasilisha Nakala za Hati za Utambulisho leo jijin Dar es Salaam.
Balozi Mteule wa Ugiriki nchini Tanzania mwenye makazi yake Nairobi, Kenya, Mhe. Konstantinos Moatsos akiwasilisha Nakala za Hati za Utambulisho kwa Waziri wa Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki, Mhe. Balozi Dkt. Augustine Mahiga ofisini kwake jijini Dar es Salaam.
Waziri wa Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki, Mhe. Balozi Dkt. Augustine Mahiga akiwa katika mazungumzo na Balozi Mteule wa Ugiriki nchini Tanzania mwenye makazi yake Nairobi, Kenya, Mhe. Konstantinos Moatsos. Mazungumzo yao yalijikita katika kuboresha ushirikiano kati ya Tanzania na Ugiriki hususan kwenye eneo la uwekezaji na biashara.



Balozi Mteule wa Mali

Balozi Mteule wa Mali nchini Tanzania mwenye makazi yake Nairobi, Kenya, Mhe. Fafre Camara akiwasilisha Nakala za Hati za Utambulisho kwa Waziri wa Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki, Mhe. Balozi Dkt. Augustine Mahiga ofisini kwake jijini Dar es Salaam.

Waziri wa Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki, Mhe. Balozi Dkt. Augustine Mahiga akiwa katika mazungumzo na Balozi Mteule wa Mali nchini Tanzania mwenye makazi yake Nairobi, Kenya, Mhe. Fafre Camara. Wawili hao walijadili namna nchi zao zitakavyoweza kushirikiana katika kutatua changamoto za pamoja kama vile ugaidi na imani kali.


Waziri wa Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki, Mhe. Balozi Dkt. Augustine Mahiga (wa pili kutoka kulia) akiwa katika picha ya pamoja na Balozi Mteule wa Mali nchini Tanzania mwenye makazi yake Nairobi, Kenya, Mhe. Fafre Camara. Wengine katika picha ni Mkurugenzi Msaidizi wa Idara ya Afrika, Bw. Suleiman Salehe (kulia) na Afisa wa Ubalozi wa Mali.
Balozi Mteule wa Colombia
Waziri wa Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki, Mhe. Balozi Dkt. Augustine Mahiga akisalimiana na Balozi Mteule wa Colombia nchini Tanzania mwenye makazi yake Nairobi, Kenya, Mhe. Elizabeth Taylor kabla ya zoezi la kuwasilisha Nakala za Hati za Utambulisho
.
Balozi Mteule wa Colombia nchini Tanzania mwenye makazi yake Nairobi, Kenya, Mhe. Elizabeth Taylor akiwasilisha Nakala za Hati za Utambulisho kwa Waziri wa Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki, Mhe. Balozi Dkt. Augustine Mahiga ofisini kwake jijini Dar es Salaam.
Waziri wa Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki, Mhe. Balozi Dkt. Augustine Mahiga akiwa katika mazungumzo na Balozi Mteule wa Colombia nchini Tanzania mwenye makazi yake Nairobi, Kenya, Mhe. Elizabeth Taylor. Wawili hao walijadili namna nchi zao zitakavyoweza kushirikiana katika masuala mbalimbali ikiwemo uwekezaji na biashara.

Waziri wa Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki, Mhe. Balozi Dkt. Augustine Mahiga (wa pili kutoka kulia) akiwa katika picha ya pamoja na Balozi Mteule wa Colombia nchini Tanzania mwenye makazi yake Nairobi, Kenya, Mhe. Elizabeth Taylor. Wengine katika picha ni Kaimu Mkurugenzi wa Idara ya Ulaya na Amerika, Bw. Salvator Mbilinyi (kulia) na Afisa wa Ubalozi wa Colombia.

 Balozi Mteule wa Argentina

Waziri wa Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki, Mhe. Balozi Dkt. Augustine Mahiga akisalimiana na Balozi Mteule wa Argentina nchini Tanzania mwenye makazi yake Nairobi, Kenya, Mhe. Martin Gomez Bustillo kabla ya kuwasilisha Nakala za Hati za Utambulisho.
Balozi Mteule wa Argentina nchini Tanzania mwenye makazi yake Nairobi, Kenya,  Mhe. Martin Gomez Bustillo akiwasilisha Nakala za Hati za Utambulisho kwa Waziri wa Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki, Mhe. Balozi Dkt. Augustine Mahiga ofisini kwake jijini Dar es Salaam.
Waziri wa Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki, Mhe. Balozi Dkt. Augustine Mahiga akiwa katika mazungumzo na Balozi Mteule wa Argentina nchini Tanzania mwenye makazi yake Nairobi, Kenya, Mhe. Martin Gomez Bustillo. Wawili hao walijadili namna nchi zao zitakavyoweza kushirikiana katika masuala mbalimbali ikiwemo uwekezaji na biashara.

Waziri wa Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki, Mhe. Balozi Dkt. Augustine Mahiga (katikati) akiwa katika picha ya pamoja na Balozi Mteule wa Argentina nchini Tanzania mwenye makazi yake Nairobi, Kenya, Mhe. Martin Gomez Bustillo. Wengine katika picha ni Kaimu Mkurugenzi wa Idara ya Ulaya na Amerika, Bw. Salvator Mbilinyi (kulia).
 Balozi Mteule wa Ufilipino

Waziri wa Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki, Mhe. Balozi Dkt. Augustine Mahiga akisalimiana na Balozi Mteule wa Ufilipino nchini Tanzania mwenye makazi yake Nairobi, Kenya, Mhe. Uriel Norman Garibay kabla ya kuwasilisha Nakala za Hati za Utambulisho.

Balozi Mteule wa Ufilipino nchini Tanzania mwenye makazi yake Nairobi, Kenya,  Mhe. Uriel Norman Garibay akiwasilisha Nakala za Hati za Utambulisho kwa Waziri wa Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki, Mhe. Balozi Dkt. Augustine Mahiga ofisini kwake jijini Dar es Salaam.


Waziri wa Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki, Mhe. Balozi Dkt. Augustine Mahiga akiwa katika mazungumzo na Balozi Mteule wa Ufilipino nchini Tanzania mwenye makazi yake Nairobi, Kenya,  Mhe. Uriel Norman Garibay. Wawili hao walijadili namna nchi zao zitakavyoweza kushirikiana katika masuala mbalimbali ikiwemo uwekezaji na biashara.

Waziri wa Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki, Mhe. Balozi Dkt. Augustine Mahiga (wa pili kutoka kulia) akiwa katika picha ya pamoja na Balozi Mteule wa Ufilipino nchini Tanzania mwenye makazi yake Nairobi, Kenya,  Mhe. Uriel Norman Garibay. Wengine katika picha ni Kaimu Mkurugenzi wa Idara ya Asia na Australasia, Bibi Justa Nyange (kulia) na Afisa wa Ubalozi wa Ufilipino.

Saturday, January 20, 2018

Wizara yawanoa Wabunge wa Tanzania wa Bunge la Nne la Afrika Mashariki

   Balozi Dkt. Augustine Mahiga, Waziri wa Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki akifungua Semina Elekezi kwa Wabunge wa Tanzania wa Bunge la Nne la Afrika Mashariki iliyofanyika kwenye Kituo cha Kimataifa cha Mikutano cha Julius Nyerere tarehe 19-20 Januari, 2018.

Wajumbe wa Semina hiyo wakimsikiliza Mheshimiwa Dkt. Mahiga wakati wa ufunguzi wa Semina ya siku mbili ya kuwaongezea uwezo Wabunge wa Tanzania watakaowakilisha nchi kwenye Bunge la Nne la Afrika Mashariki.

Dkt. Suzan Kolimba, Naibu Waziri wa Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki akiwatambulisha baadhi ya Wakurugenzi wa Wizara hiyo kwa Wabunge wa Tanzania wa Bunge la Afrika Mashariki wakati wa Semina elekezi iliyoandaliwa na Wizara kwa ajili ya Wabunge hao. 

   Waheshimiwa Dkt. Mahiga na Dkt. Kolimba kwenye picha ya pamoja na baadhi ya Wabunge wa Bunge la Nne la Afrika Mashariki. Kulia kwa Waziri Mahiga ni Mwenyekiti wa Wabunge hao Mhe. Dkt. Abdullah Makame. Wengine waliosimama kutoka kushoto ni Mhe. Dkt. Ngwaru Maghembe, Mhe. Happiness Lugiko, Mhe. Mhandisi Mohamed Habib Mnyaa, Mhe. Pamela Maasay na Mhe. Adam Kimbisa.

Waheshimiwa Dkt. Mahiga na Dkt. Kolimba kwenye picha ya pamoja na baadhi ya Wakurugenzi na maafisa wa Wizara ya Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki na Waheshimiwa Wabunge wa Bunge la Nne la Afrika Mashariki kwenye Semina elekezi iliyoandaliwa na Wizara kwa lengo la kuwaongezea uzoefu Wabunge hao. 

Mheshimiwa Adam Kimbisa akisalimiana na Mheshimiwa Dkt. Mahiga wakati wa Semina hiyo ya siku mbili iliyofanyika kwenye Kituo cha Mikutano cha Kimataifa cha Julius Nyerere tarehe 19-20 Januari, 2018. 

Mheshimiwa Pamela Maasay akijitambulisha wakati wa Semina elekezi ya Wabunge wa Bunge la Afrika Mashariki. 


Mheshimiwa Dkt. Ngwaru Maghembe akijitambulisha wakati wa Semina elekezi ya Wabunge wa Bunge la Afrika Mashariki
Mkurugenzi wa Sera na Mipango wa Wizara ya Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki akijitambulisha wakati wa Semina elekezi ya Wabunge wa Bunge la Afrika Mashariki. Wengine kwenye picha waliokaa kuanzia kulia ni Mkurugenzi Mkuu wa Idara Kuu ya Usalama wa Taifa  Dkt. Modestus Kapilimba, Prof. Adolf Mkenda, Katibu Mkuu wa Wizara na Balozi Ramadhan Mwinyi Naibu Katibu Mkuu wa Wizara.


Mheshimiwa Mhandisi Mohamed Habib Mnyaa akijitambulisha wakati wa Semina elekezi ya Wabunge wa Bunge la Afrika Mashariki



Mkurugenzi Mkuu wa Taasisi ya Kuzuia na Kupambana na Rushwa (TAKUKURU) Valentino Mlowola akitoa mada kuhusu mapambano ya rushwa wakati wa Semina elekezi kwa Wabunge wa Bunge la Afrika Mashariki. Kabla ya mada hiyo Mkurugenzi Dkt. Kapilimba wa Idara Kuu ya Usalama wwa Mataifa alitoa mada kuhusu uzalendo na usalama wa nchi.

Mheshimiwa Adam Kimbisa akichangia hoja kuhusu mapambano ya rushwa nchini iliyowasilishwa na Mkurugenzi wa TAKUKURU Bw. Valentino Mlowola wakati  wa Semina elekezi kwa Wabunge wa Afrika Mashariki iliyoandaliwa na Wizara ya Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki.


Dkt. Benard Achiula, Kaimu Mkuu wa Chuo cha Diplomasia akiwasilisha mada kuhusu itifaki na diplomasia wakati wa Semina hiyo. Pichani Dkt. Achiula akiwa na sahani na vyombo vya kulia chakula akionesha mfano wa kula kwenye dhifa za kitaifa. Mada hiyo iliambatana pia na andiko kuhusu Diplomasia ya Uchumi ambao ndio mwelekeo wa Sera ya Mambo ya Nje ya Tanzania. 

Jaji (Mstaafu) Harold Nsekela, Kamishna wa Maadili, Ofisi ya Rais - Sekretarieti ya Maadili ya Viongozi wa Umma  akitoa mada kuhusu maadili ya Mbunge wa Afrika Mashariki na Taswira ya Nchi katika uwakilishi wa Taifa.

Dkt. Maduka Kessy, Katibu Mtendaji wa Tume ya Mipango akitoa mada kuhusu Dira ya Taifa ya Maendeleo 2025 na mipango mbalimbali ya maendeleo kwenye maeneo ya kimkakati katika Mtangamano wa Afrika Mashariki.

Bw. Stephen Mbundi, Mkurugenzi wa Idara ya Siasa, Ulinzi na Usalama ya Wizara akichangia mada wakati wa Semina Elekezi ya Wabunge wa Bunge la nne  la Afrika Mashariki.


Friday, January 19, 2018

Rais Magufuli azungumza na Watumishi wa Wizara ya Mambo ya Nje

Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Mhe. Dkt. John Pombe Joseph Magufuli wa nne kutoka kushoto akiongea na wafanyakazi wa Wizara ya Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki leo kwenye Ukumbi wa Kimataifa wa Julius Nyerere jijini Dar Es Salaam. Wengine katika picha kutoka kulia kwa Mhe. Rais ni Waziri wa Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki, Mhe. Balozi Dkt. Augustine Mahiga; Waziri wa Ujenzi, Uchukuzi na Mawasiliano, Prof. Makame Mbarawa na Naibu Waziri wa Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki, Mhe. Dkt. Suzan Kolimba. Kutoka kushoto kwa Mhe. Rais ni Waziri wa Ujenzi, Mawasiliano na Usafirishaji wa Serikali ya Zanzibar, Mhe. Baloz Ali Karume; Naibu Katibu Mkuu wa Wizara ya Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki, Balozi Ramadhan Mwinyi na Katibu Mkuu wa Wizara ya Fedha na Mipango, Bw. Doto James.
Watumishi wa Wizara ya Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki wakisikiliza kwa makini maelekezo na maagizo ya Mhe. Rais Magufuli. Mhe. Rais aliagiza Wizara iongeze nguvu katika kuratibu masuala ya kimataifa kati yake na Wizara/taasisi za kisekta ili kusiwe na ucheleweshwaji wa utekelezaji wa masuala mbalimbali ikwemo uwekezaji, biashara, utalii na huduma za kijamii kama afya na elimu.

Watumishi wakiendelea kumsikiliza Mhe. Rais Magufuli.
Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Mhe. Dkt. John Pombe Joseph Magufuli akisisitiza jambo katika kikao hicho.
Mtumishi wa Wizara ya Mambo ya Nje, Bibi Helen Maduhu akichangia jambo katika kikao hicho. Mhe. Rais aliwataka watumishi wabainishe bila woga changamoto zote zinazowakabili ili kwa pamoja wajadili namna ya kuzipatia ufumbuzi.
Mkurugenzi wa Idara ya Ushirikiano wa Kimataifa, Balozi Celestine Mushy akichangia hoja zitakazosaidia kuboresha utendaji wa Serikali ili malengo ya Serikali ya Awamu ya Tano yaweze kufikiwa.
Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Mhe. Dkt. John Pombe Joseph Magufuli akiagana na watumishi wa Wizara baada ya kikao kumalizika. Katika picha ni Katibu Mtendaji wa APRM Tanzania, Bibi Rehema Twalibu akiagana na Mhe. Rais Magufuli.

Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Mhe. Dkt. John Pombe Joseph Magufuli akifurahi jambo na Kaimu Mkurugenzi wa Afrika, Balozi Grace Mujuma.
Mkurugenzi wa Idara ya Ushirikiano wa Kimataifa, Balozi Celestine Mushy akiagana na Mhe. Rais Magufuli.


Watumishi wakiendelea kuagana na Mhe. Rais, pichani ni Bw. Ally Kondo naye akishikana mikono na Mhe. Rais.

Thursday, January 18, 2018

Tanzania yawa mwenyeji wa Mkutano wa pili wa India - Afrika

Waziri wa Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki, Mhe. Balozi Dkt. Augustine Mahiga akitoa hotuba ya ufunguzi katika Mkutano wa pili wa India - Afrika uliofanyika katika ofisi za ubalozi wa India nchini Jijini Dar es Salaa tarehe 18 Januari 2017.

Mkutano huo wa siku mbili unatarajiwa kumalizika tarehe 19 Januari 2018 ambapo umewakutanisha  wajumbe kutoka serikali ya India, wajumbe wa nchi wanachama wa Afrika Mashariki (EAC) na wa Jumuiya ya Maendeleo Kusini mwa Afrika(SADC) kwa lengo la kujadili masuala ya ushirikiano pamoja na kubuni maeneo mapya ya ushirikiano kwa manufaa ya wananchi wa India na wa jumuiya hizo 

Balozi wa India nchini, Mhe. Sandeep Arya akihutubia ambapo alieleza pamoja na kujadili masuala ya ushirikiano Serikali ya India itatumia fursa ya Mkutano huo kukusanya maoni, taarifa na mapendekezo yatakayotolewa na wadau hususan katika masuala ya ulinzi, amani na maendeleo ili kila Taifa liweze kufikia malengo ya kitaifa na kuboresha maisha ya wananchi wake.

Waziri Mkuu Mstaafu, Dr. Salim Ahmed Salim akihutubia katika Mkutano huo ambapo alieleza kuwa India ni mfano wa Taifa kubwa linaloendeshwa kidemokrasia licha ya kuwa na idadi kubwa ya watu na hivyo akasisitiza ni muhimu kwa nchi za Jumuiya ya Afrika Mashariki na zile za Jumuiya ya Maendeleo kusini mwa Afrika zikafata mfano huo ili ziweze kuruhusu shughuli za maendeleo kufanyika kwa amani na kuwaletea wananchi maendeleo.

Mkurugenzi Mkuu wa Baraza linaloshughulikia masuala ya Ulimwengu nchini India, Bw. Nalin Surie akihutubia katika ufunguzi wa Mkutano huo ambapo alieleza India imejidhatiti katika kuhakikisha ushirikiano wake na mataifa ya Afrika unaimarika na kuwa wa manufaa kiuchumi huhusan kwa nchi wananchama wa Jumuiya ya Afrika Mashariki na Jumuiya ya Maendeleo Kusini mwa Afrika.
Mkurugenzi wa Idara ya Biashara, uwekezaji na Sekta za Uzalishaji katika Wizara ya Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki, Bw. Bernard Haule (wa pili toka kulia) pamoja na wajumbe wengine wakifuatilia Mkutano.


Kutoka kushoto ni Mkurugenzi wa Idara ya Siasa, Ulinzi na Usalama katika Wizara ya Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki, Bw. Stephen Mbundi na Kaimu Mkuu wa Chuo cha Diplomasia, Dkt. Bernard Achiula wakifuatilia Mkutano. 

Sehemu ya wajumbe kutoka nchi wananchama wa Jumuiya ya Afrika Mashariki na Jumuiya ya Maendeleo kusini mwa Afrika wakifuatilia Mkutano.

Sehemu nyingine ya Wajumbe wakifuatilia Mkutano
Wajumbe wakishuhudia hafla ya ufunguzi wa Mkutano.

Waandishi wa Habari wakifanya mahojiano na Mhe. Waziri Mahiga mara baada ya hafla ya ufunguzi kumalizika.