Thursday, June 17, 2021

NAIBU WAZIRI AFANYA MAZUNGUMZO NA WAANDAAJI MASHINDANO YA UREMBO AFRIKA MASHARIKI

 

Naibu Waziri Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki Mhe, Balozi Mbarouk Nassor Mbarouk akizungumza na waandaaji wa mashindano ya urembo kwa nchi za Afrika Mashariki (Miss East Africa beauty Pegeant) ofisini kwake jijini Dodoma

Mkurugenzi wa Idara ya Miundombinu na Huduma za Jamii Bw. Eliabi Chodota akizungumza wakati Naibu Waziri Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki Mhe, Balozi Mbarouk Nassor Mbarouk wakati walipokutana na akizungumza na waandaaji wa mashindano ya urembo kwa nchi za Afrika Mashariki (Miss East Africa beauty Pegeant) ofisini kwa Naibu Waziri jijini Dodoma

Makamu Rais wa Kamati ya Waandaaji wa Mashindano ya Urembo Afrika Mashariki bi Jolly Mutesi wa Rwanda (katikati) akizungumza akiwa na bi Mariam Ikoa kutoka Tanzania wakia na naibu Waziri Ofisini kwake jiini Dodoma.

mazungumzo yakiendelea

Naibu Waziri Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki Mhe, Balozi Mbarouk Nassor Mbarouk katika picha ya pamoja na waandaaji wa mashindano ya urembo kwa nchi za Afrika Mashariki (walioko Kulia kwake) walipomtembelea ofisini kwake jijini Dodom


Naibu Waziri Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki Mhe, Balozi Mbarouk Nassor Mbarouk amekutana na kufanya mazungumzo na waandaaji wa mashindano ya urembo kwa nchi za Afrika Mashariki (Miss East Africa beauty Pegeant) ofisini kwake jijini Dodoma.

Waandaaji hao ni  bi Jolly Mutesi ambaye ni makamu wa Rais anayetokea nchini Rwanda na bi Mariam Ikoa ambaye ni muandaaji wa kimataifa anayetokea Tanzania.

Katika mazungumzo hayo  na waandaaji hao wa mashindano ya urembo kwa nchi za Afrika Mashariki Mhe. Balozi Mbarouk amewapongeza waandaaji hao  kwa kuja na wazo  hilo pamoja na kutaka kufahamu miongozo na itifaki za kufuatilia ili kufanikisha mashindano hayo.

Akizungumza  katika kikao hicho Mratibu wa mashindanoo hayo Bi Mariam Ikoa amemuelezea Mhe. Naibu Waziri Mbarouk kwamba ujio wao Wizarani una lengo la kujitambulisha pamoja na kupata miongozo na itifaki za jinsi ya kuendelea na taratibu za mashindano hayo ya urembo kwa ukanda wa Afrika Mashariki.

Amesema mashindano hayo yamepangwa  kufanyika jijini Dar es Salaam kuanzia tarehe 26 Oktoba hadi Novemba 20 2021

SADC yaitaka EU Kuiondolea Vikwazo Zimbabwe

SADC yaitaka EU Kuiondolea Vikwazo Zimbabwe

Na Mwaandishi Maalum, Dodoma

Tanzania imeendelea kutoa wito wa kuiondolea vikwazo vya kiuchumi Zimbabwe, ambavyo vimetajwa kuwa vinadumaza jitihada za nchi hiyo za kujiletea maendeleo. Wito huo umetolewa wakati wa Mkutano wa majadiliano wa Mawaziri wa Mambo ya Nje wa nchi wanachama wa Jumuiya ya Maendeleo Kusini mwa Afrika (SADC) na Umoja wa Ulaya (EU) uliofanyika kwa njia ya mtandao tarehe 16 Juni 2021.


“Hakuna sababu ya kuendelea kuiwekea vikwazo Zimbabwe ilihali imefanya mabadiliko ya kimfumo katika maeneo mengi yakiwemo ya siasa, uchumi na mifumo ya sheria”, walisikika wakisema Mawaziri wa SADC, baada ya ujumbe wa Tanzania ambao uliongozwa na Waziri wa Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki, Balozi Liberata Mulamula (Mb) kuwasilisha hoja hiyo.

Ikijibu hoja hiyo, EU kupitia Waziri wa Mambo ya Nje wa Ureno, Mhe. Augusto Santos Silva ilisisitiza umuhimu wa Zimbabwe kuendelea kufanya mabadiliko katika mifumo yake na kudai kuwa vikwazo vilivyosalia havina athari yoyote kwa watu wa Zimbabwe. Ilisema, licha ya vikwazo hivyo, EU imeendelea kushirikiana na Zimbabwe kwa kuipatia misaada ya maendeleo na ya kibinadamu ambapo Euro milioni 366 na milioni 66 mutawalia zimetolewa kwa Zimbabwe katika kipindi cha miaka saba iliyopita.

 

Katika majadiliano hayo yenye lengo la kusaidia kukuza uchumi na maendeleo katika kanda ya SADC, Waheshimiwa Mawaziri walijadili kuhusu janga la UVIKO-19 na athari zake katika ukuaji wa uchumi na mikakati ya kujikwamua kiuchumi baada ya ugonjwa huo kudhibitiwa. EU iliahidi kuendelea kushirikiana na nchi za SADC kupitia programu mbalimbali zikiwemo za kuhakikisha kuwa kila mtu anapata chanjo na programu nyingine za unafuu wa kulipa madeni na misaada ya fedha za kukabiliana na athari za UVIKO-19.

Kuhusu mikakati ya kukabiliana na UVIKO-19, Nchi za SADC kupitia Waziri wa Mambo ya Nje wa Msumbiji, Mhe. VerĂ³nica Macamo alizihimiza nchi za EU kuzijengea uwezo nchi za SADC wa kutengeneza vifaa vya kukabiliana na UVIKO-19 badala ya kuagiza vifaa hivyo kutoka nchi zilizoendelea.

Kwa upande wa agenda ya hali ya siasa, ulinzi na usalama katika kanda ya SADC, Waheshimiwa Mawaziri walieleza kuwa hali ni ya kuridhisha, isipokuwa kumekuwepo na matishio na mashambulizi ya kigaidi katika Jamhuri ya Kidemokrasia ya Congo (DRC) na Msumbiji. EU iliahidi kuendelea kushirikiana na nchi hizo ili kukabiliana na changamoto za kiusalama katika Mashaiki ya DRC na jimbo la Cabo Delgado nchini Msumbiji.

Nchi za SADC, zilitoa shukrani kwa misaada ya kiusalama inayopokea kutoka EU na kuzisihi nchi hizo kuendelea kutoa misaada hiyo kwa kuwa suala la ulinzi na usalama ni ndiyo moyo wa progarumu za ushirikiano wao kuendelea. Kutokana na umuhimu wa usalama katika kanda, EU iliombwa kuunga mkono mchakato wa uanzishaji wa Kituo cha Kukabiliana na Ugaidi cha SADC (SADC Regional Counter Terrorism Centre-RCTC).

Suala lingine lililojadiliwa na Waheshimiwa Mawaziri ni biashara na uwekezaji ambapo EU imepongeza jitihada zinazoendelea za kuwa na Soko Huru la SADC-EAC-ECOWAS na la Bara la Afrika (AFCFTA). Ilielezwa kuwa masoko hayo itakuwa chachu katika uwekezaji, ujenzi wa miundombinu, kuongezeka kwa ajira na kumaliza umasikini barani Afrika.


Waziri wa Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki, Balozi Liberata Mulamula (Mb) akiongea wakati wa Mkutano wa Mawaziri wa Mambo ya Nje wa Nchi wanachama wa Jumuiya ya Maendeleo Kusini mwa Afrika (SADC) na Umoja wa Ulaya (EU) uliofanyika kwa njia ya Mtandao.
Naibu Waziri wa Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki, Balozi Mbarouk N. Mbarouk akifuatilia majadiliano ya Mkutano wa  Mawaziri wa Mambo ya Nje wa Nchi wanachama wa Jumuiya ya Maendeleo Kusini mwa Afrika (SADC) na Umoja wa Ulaya (EU) uliofanyika kwa njia ya Mtandao.


Maafisa waandamizi kutoka taasisi za Serikali wakifuatilia majadiliano ya Mkutano wa Mawaziri wa Mambo ya Nje wa Nchi wanachama wa Jumuiya ya Maendeleo Kusini mwa Afrika (SADC) na Umoja wa Ulaya (EU) uliofanyika kwa njia ya Mtandao. 

Waziri wa Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki, Balozi Liberata Mulamula (Mb) akiwa na Kaimu Mkurugenzi wa Ushirikiano wa Kikanda, Balozi Mteule Agnes Kayola na Bw. Joseph Haule kutoka Wizara ya Fedha na Mipango kabla ya kuanza  Mkutano wa Mawaziri wa Mambo ya Nje wa Nchi wanachama wa Jumuiya ya Maendeleo Kusini mwa Afrika (SADC) na Umoja wa Ulaya (EU) uliofanyika kwa njia ya Mtandao. 




 

Wednesday, June 16, 2021

TANZANIA KUWA MWENYEJI WA KONGAMANO LA BIASHARA NA VIWANDA LA AFRIKA MASHARIKI


Waziri wa Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki, Mhe. Balozi Liberata Mulamula (Mb.) amekutana na kufanya mazungumzo na Rais wa Chama cha Wafanyabiashara, Wenye Viwanda, na Wakulima Tanzania (TCCIA) Bw. Paul Koyi pamoja na Mratibu wa Kanda wa Chama cha Wafanyabiashara, Wenye viwanda na Wakulima  Afrika Mashariki (EACCIA) Bw. Charles Kahuthu walipomtembelea ofisini kwake tarehe 16 Juni 2021 Jijini Dodoma.

Ujumbe huo unaosimamia masuala mbalimbali ya sekta binafsi ulikutana na Mhe. Balozi Mulamula kwa lengo la kuwasilisha serikalini kusudi la sekta hiyo kuipendekeza Tanzania kuwa mwenyeji wa Kongamano la Biashara na Viwanda linalotarajiwa kufanyika kuanzia tarehe 30 Agosti  hadi  3 Septemba 2021 katika kituo cha Mikutano cha Kimataifa cha Julius Nyerere Jijini Dar es Salaam.

Lengo la kongamano hili ni kuziunganisha sekta binafsi ili zipate uzoefu zaidi katika masuala ya viwanda na biashara. Pia kuviandaa vyama vya biashara, viwanda na kilimo vya kanda kuwa tayari kwa ushindani wakati huu ambapo mataifa ya Afrika yanajiweka tayari kuingia katika soko huru la biashara la Afrika (CFTA).

Aidha, Rais wa TCCIA Bw. Koyi alieleza kuwa  kongamano hilo litaambatana na maonesho ya bidhaa na huduma mbalimbali zinazotolewa na sekta binafsi hivyo, itakuwa ni fursa nzuri kwa sekta binafsi na wananchi kwa ujumla kushiriki katika kongamano hilo ili kujifunza masuala ya biashara na uwekezaji.

Naye mratibu wa kanda wa EACCIA, Bw. Charles Kahuthu alifafanua malengo madhubuti ya chama hicho katika kuhakikisha kongamano hilo linakuwa tofauti na makongamano mengine yaliyokwishafanyika ni pamoja na kuhakikisha kinaongeza ushirikiano na kanda nyingine ndani ya Afrika ili kuweza kufungua fursa zaidi kwa wananchi wake.

“Sisi waratibu wa sekta binafsi tumepanga Kongamano hili liwakutanishe wafanyabiashara kutoka nchi za Afrika Mashariki, nchi za Maziwa makuu, na nchi nyingine ndani ya Afrika” alisema Bw. Kahuthu

Akiongea na ujumbe huu Mhe. Balozi Mulamula ameihakikishia sekta binafsi juu ya utayari wa serikali katika kuhakikisha inafanikisha jitihada hizi zenye lengo la kuinua uchumi na kwamba itakuwa bega kwa bega kutoa ushirikiano wakati wa maandalizi na wakati wa kongamano.

Vilevile, ametoa wito kwa TCCIA kuiandaa sekta binafsi kushiriki kikamilifu kuzinadi fursa mbalimbali katika kongamano hilo. Pia akaongeza kuwa kongamano litasaidia katika kupeana uzoefu wa kukuza mitaji na masoko ya biashara nje ya mipaka ya Tanzania sambamba na kuvutia uwekezaji.

Kadhalika, ametoa wito kwa wananchi kujiandaa kutumia fursa mbalimbali zitakazopatikana kupitia ugeni huo utakaowasili nchini.

Chama cha Wafanyabiashara, Wenye Viwanda na Wakulima Afrika Mashariki (EACCIA) chenye makao yake makuu nchini Kenya ni mdau muhimu katika kusimamia masuala ya sekta binafsi ndani ya jumuiya na pia kimekuwa kikiainisha vipaumbele mbalimbali vya sekta binafsi ndani ya jumuiya kwa kushirikiana na vyama vya kitaifa vinavyosimamia sekta hiyo.  

Waziri wa Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki, Mhe. Balozi Liberata Mulamula (Kulia) akizungumza na Rais wa Chama cha Wafanyabiashara,Wenye Viwanda na Wakulima Tanzania (TCCIA), Bw. Paul Koyi alipomtembelea ofisini kwake tarehe 16 Juni 2021 Jijini Dodoma.
Bw. Koyi alimueleza Mhe, Balozi Mulamula lengo la ujio wake pamoja na kumtambulisha Mratibu wa Kanda wa Chama cha Wafanyabiashara, Wenye Viwanda na Wakulima Afrika Mashariki(EACCIA) Bw. Charles Kahuthu(hayupo pichani)
Mhe. Balozi Mulamula akieleza nia ya dhati ya serikali katika kuhakikisha sekta binafsi inapewa ushirikiano ili kukuza na kuimarisha biashara ya kimataifa sambamba na uwekezaji. 
Wa kwanza kushoto ni Mratibu wa Kanda wa Chama cha Wafanyabiashara, Wenye Viwanda na Wakulima Afrika Mashariki (CCIA) Bw. Charles Kahuthu.
Kaimu Mkurugenzi wa Idara ya Biashara, Uwekezaji na Sekta za Uzalishaji,Wizara ya Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki, Bw. Bernard Haule (wa kwanza kulia) akifafanua programu mbalimbali za kitaifa na kikanda zilizofanyika katika kuhamasisha sekta binafsi na umma kwa ujumla juu ya fursa zinazopatikana katika soko la Afrika Mashariki na kuwaandaa wananchi kuingia katika ushindani wa soko huru la biashara la Afrika (CFTA).
Mazungumzo yakiendelea.

WANAFUNZI WA CHUO CHA DIPLOMASIA NA WAKUFUNZI WAO WATEMBELEA WIZARA YA MAMBO YA NJE NA USHIRIKIANO WA AFRIKA MASHARIKI

Mwakilishi wa Katibu Mkuu Wizara ya Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki, Mkurugenzi  wa Kitengo cha wa Diaspora Balozi Anisa Mbega akizungumza kuwakaribisha Wanafunzi wa kozi ya Astashahada ya uzamili kutoka Chuo cha Diplomasia (CFR) na wakufunzi wao  waliotembelea Wizara ya Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki kwa ajili ya kujifunza 

Mkurugenzi wa Idara ya Siasa, Ulinzi na Usalama Wizara ya Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki, Balozi Stephen Mbundi akizungumza baada ya kukamilika kwa mazungumzo kati ya Wanafunzi wa kozi ya Astashahada ya uzamili kutoka Chuo cha Diplomasia (CFR) na wakufunzi wao  waliotembelea Wizara ya Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki kwa ajili ya kujifunza

Baadhi ya Wanafunzi wa kozi ya Astashahada ya uzamili kutoka Chuo cha Diplomasia (CFR) waliotembelea Wizarani kwa ajili ya kujifunza shughuli mbalimbali za Wizara wakisikiliza mawasilisho mbalimbali yaliyokuwa yakitolewa na watendaji wa  Wizara ya Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki 


Baadhi ya Wanafunzi wa kozi ya Astashahada ya uzamili kutoka Chuo cha Diplomasia (CFR) waliotembelea Wizarani kwa ajili ya kujifunza shughuli mbalimbali za Wizara wakisikiliza mawasilisho mbalimbali yaliyokuwa yakitolewa na watendaji wa Wizara ya Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki


Baadhi ya Wanafunzi wa kozi ya Astashahada ya uzamili kutoka Chuo cha Diplomasia (CFR) waliotembelea Wizarani kwa ajili ya kujifunza shughuli mbalimbali za Wizara wakisikiliza mawasilisho mbalimbali yaliyokuwa yakitolewa na watendaji wa Wizara ya Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki

Baadhi ya Wanafunzi wa kozi ya Astashahada ya uzamili kutoka Chuo cha Diplomasia (CFR) waliotembelea Wizarani kwa ajili ya kujifunza shughuli mbalimbali za Wizara wakisikiliza mawasilisho mbalimbali yaliyokuwa yakitolewa na watendaji wa Wizara ya Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki

Baadhi ya Wanafunzi wa kozi ya Astashahada ya uzamili kutoka Chuo cha Diplomasia (CFR) waliotembelea Wizarani kwa ajili ya kujifunza shughuli mbalimbali za Wizara wakisikiliza mawasilisho mbalimbali yaliyokuwa yakitolewa na watendaji wa Wizara ya Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki



Wakufunzi wa Chuo cha Diplomasia (CFR) wakisikiliza mawasilisho mbalimbali yaliyokuwa yakitolewa na watendaji wa  Wizara ya Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki, walipowaongoza Wanafunzi wa kozi ya stashahada ya uzamili kutembelea Wizarani kwa ajili ya kujifunza shughuli mbalimbali za Wizara


Baadhi ya Wanafunzi wa kozi ya Astashahada ya uzamili kutoka Chuo cha Diplomasia (CFR) walotembelea Wizarani kwa ajili ya kujifunza wakiwa katika picha ya pamoja na watendaji wa Wizara ya Wizara ya Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki jijini Dodoma


Baadhi ya Wanafunzi wa kozi ya Astashahada ya uzamili kutoka Chuo cha Diplomasia (CFR) walotembelea Wizarani kwa ajili ya kujifunza wakiwa katika picha ya pamoja na watendaji wa Wizara ya Wizara ya Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki jijini Dodoma



 



Wanafunzi wa kozi ya Astashahada ya uzamili kutoka Chuo cha Diplomasia (CFR) na wakufunzi wao wamefanya ziara ya mafunzo kwa kutembelea Wizara ya Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki jijini Dodoma na kuzungumza na watendaji wa Wizara kwa ajili ya kujifunza namna Wizara watendaji wa Wizara wanavyotekeleza diplomasia ya uchumi kupitia kazi zao.

Wanafunzi hao kutoka kampasi ya Dar es Salaam na Dodoma walipata nafasi ya kusikiliza mada za muundo na majukumu ya Wizara ya Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki pamoja na Sera ya Mambo ya Nje ya Mwaka 2001.

Akizungumza wakati wa kuwakaribisha wanachuo hao kwa niaba ya Katibu Mkuu Wizara ya Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki, Mkurugenzi wa Kitengo cha wa Diaspora Balozi Anisa Mbega aliwataka wanachuo hao kusikiliza kwa umakini mada zitakazotolewa na watendaji wa Wizara ambao wanafanya shughuli za kidiplomasia kwa vitendo ili kujiongezea ujuzi zaidi.

Balozi Anisa aliwaambia wanachuo hao kuwa Wizara inaona fahari kuwa na chuo hicho kwani kinawezesha upatikanaji wa elimu ya diplomasia kwa wananchi wengi na kuwataka wanachuo hao kuitumia elimu wanayoipata kwa manufaa yao na taifa kwa ujumla

Akizungumza kukamilisha mazungumzo kati ya wanachuo hao na watendaji wa Wizara Mkurugenzi wa Idara ya Siasa, Ulinzi na Usalama Balozi Stephen Mbundi aliwataka wanachuo hao kuwa tayari na kujiandaa na dunia ya sasa ili waende na wakati uliopo na aliwaahidi kuwa Wizara iko tayari muda wowote kuwasaidia ili waweze kuitendea haki elimu waliyoipata.

Wanachuo hao na wakufunzi wao walikuwa na ziara ya siku mbili jijini Dodoma ambapo siku ya kwanza walienda kutembelea Bunge kwa mwaliko wa Naibu Waziri –Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki Mhe. Balozi Nassor Mbarouk na kujionea jisni Bunge la Tanzania linavyoendesha shughuli zake.

Tuesday, June 15, 2021

BALOZI MULAMULA AKUTANA NA KUFANYA MAZUNGUMZO NA BALOZI WA MAREKANI HAPA NCHINI

Waziri wa Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki, Mhe. Balozi Liberata Mulamula (Mb.) amekutana kwa mazungumzo na Balozi wa Marekani hapa nchini Mhe. Dkt. Donald J. Wright, jijini Dodoma leo tarehe 15 Juni 2021.

Pamoja na mambo mengine, viongozi hao wamejadili umuhimu wa kuendelea kuimarisha ushirikiano baina nchi hizi mbili. 

Akizungumza kwenye mkutano huo, Balozi Mulamula amemhakikishia Balozi Wright ushirikiano hususan kupitia Sekta muhimu ambazo nchi hizi mbili zinashirikiana kwa muda mrefu ikiwemo sekta ya afya, elimu, miundombinu, teknolojia, uwekezaji na biashara.

"Leo nimekutana na Balozi wa Marekani hapa nchini ikiwa ni utaratibu niliojiwekea wa kukutana na Mabalozi wawanaowakilisha nchi zao hapa Tanzania mara kwa mara kwa  lengo la kubadilishana nao mawazo kuhusu namna bora ya kuimarisha uhusiano wetu na nchi hizo. Katika mazungumzo yangu na Balozi Wright tumejadili masuala mbalimbali ya ushirikiano ikiwemo mpango wanaoufadhili wa kupambana na UKIMWI wa PEPFAR na jambo kubwa amenijulisha kuwa Marekani ipo tayari kushirikiana na Tanzania na kwamba kampuni nyingi za nchi hiyo zipo tayari kuja kuwekeza na kufanya biashara hapa nchini wakati wowote kuanzia sasa” alisema Balozi Mulamula.

“Pia amenifahamisha kuwa, Tanzania mwaka huu imekuwa miongoni mwa nchi za Afrika zinazostahili kupeleka bidhaa zake za kilimo nchini Marekani bila kutozwa ushuru kupitia Mpango wa AGOA. Hii ni fursa muhimu kwetu na kinachotakiwa sasa ni sisi kujiimarisha katika kuzalisha bidhaa bora zitakazokidhi vigezo vya kuingia kwenye soko la Marekani” alisisitiza  Mhe. Waziri.

Kwa upande wake, Balozi Wright amemshukuru Mhe. Balozi Mulamula kwa kumpokea na kueleza kuwa nchi yake inathamini na kuuenzi ushirikiano wa muda mrefu uliopo kati yake na Tanzania na kwamba itaendelea kuuimarisha ushirikiano huo kwa kuchangia sekta mbalimbali.

“Nimekuwa na mkutano mzuri na Mhe. Balozi Mulamula na tumejadili masuala muhimu na yenye manufaa kwa nchi zetu mbili hususan umuhimu wa kuimarisha ushirikiano kupitia sekta mbalimbali. Marekani inaihesabu Tanzania kama rafiki na mshirika muhimu hivyo mkutano huu ni moja ya jitihada za kuimarisha ushirikiano na urafiki huo” alieleza Balozi Wright.

Waziri wa Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki, Mhe. Balozi Liberata Mulamula (Mb.) akizungumza na Balozi wa Marekani nchini, Mhe. Dkt. Donald J. Wright walipokutana kwa mazungumzo Ofisini kwake jijini Dodoma tarehe 15 Juni 2021. 

Kaimu Mkurugenzi wa Idara ya Ulaya na Amerika katika Wizara ya Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki, Bw. Hassan Mwamweta akiwa na Msaidizi wa Waziri, Balozi Grace Martin wakifuatilia mazungumzo kati ya Mhe. Waziri Mulamula na Balozi Wright (hawapo pichani)

Maafisa kutoka Ubalozi wa Marekani walioongozana na Mhe. Balozi Wright nao wakifuatilia mazungumzo

Mazungumzo yakiendelea

Mazungumzo yakiendelea

Picha ya pamoja kati ya  Mhe. Waziri Mulamula na Mhe. Balozi Wright

Picha ya pamoja

 



Friday, June 11, 2021

MKUTANO WA 31 WA BARAZA LA MAWAZIRI WA EAC WANAOSHUGHULIKIA MASUALA YA AFRIKA MASHARIKI NA MIPANGO WAFANYIKA ARUSHA

Mkutano wa 31 wa Baraza la Mawaziri la Kisekta linaloshughulikia masuala ya Afrika Mashariki na Mipango umefanyika jijini Arusha leo tarehe 11 Juni 2021 huku Mawaziri wakipitisha agenda mbalimbali zilizowasilishwa kwao.

 

Katika hotuba yake ya ufunguzi, Mwenyekiti wa Mkutano huo ambaye ni Waziri wa Ushirikiano wa Afrika Mashariki na Maendeleo ya Kikanda wa Kenya, Mhe. Aden Mohammed amepongeza kazi kubwa iliyofanywa na vikao vilivyotangulia vya Wataalam na Makatibu Wakuu ya kukamilisha agenda mbalimbali muhimu na kwamba anayo furaha kwa mikutano mbalimbali kuanza kufanyika jijini Arusha na kuhudhuriwa na Wajumbe kutoka Nchi Wanachama baada ya vikao hivyo kufanyika kwa muda mrefu kwa njia ya mtandao kutokana na mlipuko wa ugonjwa wa corona.

 

Naye Katibu Mkuu wa Jumuiya ya Afrika Mashariki, Mhe. Dkt. Peter Muthuki aliwakaribisha Mawaziri kwenye Makao Makuu ya[H1]  Jumuiya hiyo na alitumia fursa hiyo kuzipongeza Tanzania na Uganda kwa kuendesha zoezi la uchaguzi kwenye nchi zao kwa amani na utulivu. Kadhalika, alitoa shukrani kwa Nchi Wanachama kwa kuendelea kushirikiana kikamilifu na Sekretarieti ya Jumuiya hiyo na kuiwezesha kutekeleza majukumu yake ya kila siku kwa ufanisi.


Kwa upande wake, Waziri wa Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki, Mhe. Balozi Liberata Mulamula ambaye alishiriki mkutano huo kwa mara ya kwanza kwa njia ya mtandao akiwa jijini Dar es Salaam, alitumia fursa hiyo kumpongeza Mwenyekiti wa mkutano huo pamoja na Katibu Mkuu wa Jumuiya ya Afrika Mashariki kwa kuteuliwa kuiongoza Jumuiya hiyo na kuwahakikishia ushirikiano kutoka kwake binafsi na kwa  Serikali ya Jamhuri ya Muungano wa Tanzania.


Mkutano wa Mawaziri ulitanguliwa na Mkutano kwa Ngazi ya Wataalam uliofanyika tarehe 7 hadi 9 Juni 2021 na kufuatiwa na Mkutano wa Makatibu tarehe 10 Juni 2021.


Pamoja na mambo mengine Mkutano huo umepokea na kupitisha agenda mbalimbali zilizowasilishwa ikiwa ni pamoja Taarifa ya Utekelezaji wa maazimio yaliyofikiwa kwenye vikao vilivyopita; Taarifa kuhusu hatua iliyofikiwa katika utekelezaji wa Itifaki ya Soko la Pamoja la Jumuiya ya Afrika Mashariki; Taarifa kuhusu ombi la Jamhuri ya Kidemokrasia ya Congo la kujiunga na EAC; Taarifa kuhusu hatua iliyofikiwa ya utatu wa Jumuiya za EAC-COMESA-SADC katika Eneo Huru la Biashara Barani Afrika na Taarifa ya Uchangiaji wa Bajeti ya EAC kutoka Nchi Wanachama.


Ujumbe wa Tanzania kwenye Mkutano wa Ngazi ya Mawaziri umeongozwa na Waziri wa Nchi, Ofisi ya Rais, Menejimenti ya Utumishi wa Umma na Utawala Bora, Mhe. Mohammed Mchengerwa aliyemwakilisha Mhe. Balozi Mulamula ambaye alishiriki kwa njia ya mtandao.

 

Viongozi wengine walioshiriki Mkutano huo ni pamoja na Mwanasheria Mkuu wa Serikali, Prof. Adelardus Kilangi, Waziri wa Nchi, Ofisi ya Rais, Uwekezaji, Uchumi na Ajira Zanzibar, Mhe. Mudrick Ramadhan Soraga, Naibu Waziri wa Afya, Maendeleo ya Jamii, Jinsia, Wazee na Watoto, Mhe. Dkt. Godwin Mollel, Katibu Mkuu, Ofisi ya Rais, Menejimenti ya Utumishi na Utawala Bora, Dkt. Laurean Ndumbaro, Katibu Mkuu wa Wizara ya Kazi, Uchumi na Uwekezaji Zanzibar, Bw. Mussa Haji Ali na   Mkurugenzi wa Idara ya Siasa, Ulinzi na Usalama katika Wizara ya Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki, Balozi Stephen Mbundi. 

Waziri wa Nchi, Ofisi ya Rais, Menejimenti ya Utumishi na Utawala Bora, Mhe. Mohammed Mchengerwa akiongoza ujumbe wa Tanzania kwenye Mkutano wa 31 wa Baraza la Mawaziri la Kisekta linaloshughulikia masuala ya Afrika Mashariki na Mipango uliofanyika jijini Arusha tarehe 11 Juni 2021. Kulia ni Mwanasheria Mkuu wa Serikali, Prof. Adelardius Kilangi.

Mhe. Mchengerwa akichangia hoja wakati wa Mkutano wa 31 wa Baraza la Mawaziri la Kisekta linaloshughulikia masuala ya Afrika Mashariki na Mipango uliofanyika jijini Arusha tarehe 11 Juni 2021

Mhe. Prof. Kilangi naye akichangia jambo wakati wa Mkutano wa 31 wa Baraza la Mawaziri la Kisekta linaloshughulikia masuala ya Afrika Mashariki na Mipango uliofanyika jijini Arusha tarehe 11 Juni 2021

Mwenyekiti wa Mkutano wa Mawaziri ambaye ni Waziri Afrika Mashariki na Maendeleo ya Kikanda wa Kenya, Mhe. Adan Mohammed akifungua rasmi Mkutano wa 31 wa Baraza la Mawaziri la Kisekta linaloshughulikia masuala ya Afrika Mashariki na Mipango uliofanyika jijini Arusha tarehe 11 Juni 2021

Katibu Mkuu wa Jumuiya ya Afrika Mashariki (EAC), Mhe. Dkt. Peter Mathuki akizungumza wakati wa Mkutano wa 31 wa Baraza la Mawaziri la Kisekta linaloshughulikia masuala ya Afrika Mashariki na Mipango uliofanyika jijini Arusha tarehe 11 Juni 2021

Ujumbe wa Burundi ukiongozwa na Mhe. Balozi Ezechiel Nabigira (kushoto), Waziri anayeshughulikia masuala ya Afrika Mashariki, Vijana, Michezo na Utamaduni

Ujumbe wa Rwanda ukiongozwa na Mhe. Prof. Manasseh Nshuti (kushoto), Waziri wa Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Kimataifa


Ujumbe wa Kenya ukiwa kwenye Mkutano wa 31 Baraza la Mawaziri la Kisekta linaloshughulikia masuala ya Afrika Mashariki na Mipango uliofanyika jijini Arusha tarehe 11 Juni 2021

Ujumbe wa Uganda ukishiriki Mkutano wa 31 wa Baraza la Mawaziri la Kisekta linaloshughulikia masuala ya Afrika Mashariki na Mipango uliofanyika jijini Arusha tarehe 11 Juni 2021


Ujumbe wa Sudan Kusini ukishiriki Mkutano wa 31 wa Baraza la Mawaziri la Kisekta linaloshughulikia masuala ya Afrika Mashariki na Mipango uliofanyika jijini Arusha tarehe 11 Juni 2021

Waziri wa Nchi, Ofisi ya Rais, Uwekezaji, Uchumi na Ajira Zanzibar, Mhe. Mudrick Ramadhan Soraga (kulia) akiwa  na Naibu Waziri wa Afya, Maendeleo ya Jamii, Jinsia, Wazee na Watoto, Mhe. Dkt. Godwin Mollel kwenye Mkutano wa 31 wa Baraza la Mawaziri la Kisekta linaloshughulikia masuala ya Afrika Mashariki na Mipango uliofanyika jijini Arusha tarehe 11 Juni 2021. 

Mhe. Soraga na Mhe. Mollel wakiwa na Katibu Mkuu wa Wizara ya Katiba na Sheria, Prof. Sifuni Mchome wakati wa Mkutano wa 31 wa Baraza la Mawaziri la Kisekta linaloshughulikia masuala ya Afrika Mashariki na Mipango uliofanyika jijini Arusha tarehe 11 Juni 2021

Katibu Mkuu wa Ofisi ya Rais, Menejimenti ya Utumishi wa Umma na Utawala Bora, Dkt. Laurean Ndumbaro (katikati) kwa pamoja na Katibu Mkuu wa Wizara ya Kazi, Uchumi na Uwekezaji Zanzibar, Bw. Mussa Haji Ali na Mkurugenzi wa Idara ya Siasa, Ulinzi na Usalama katika Wizara ya Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki, Balozi Stephen Mbundi wakiwa kwenye Mkutano wa 31 wa Baraza la Mawaziri la Kisekta linaloshughulikia masuala ya Afrika Mashariki na Mipango uliofanyika jijini Arusha tarehe 11 Juni 2021

Ujumbe wa Tanzania ukishiriki Mkutano wa 31 wa Baraza la Mawaziri la Kisekta linaloshughulikia masuala ya Afrika Mashariki na Mipango uliofanyika jijini Arusha tarehe 11 Juni 2021


Sehemu nyingine ya ujumbe wa Tanzania




RAIS WA JAMHURI YA BOTSWANA MHE. DKT. MASISI ATEMBELEA KIWANDA CHA KUSAGA NAFAKA CHA AZAM


Rais wa Jamhuri ya Botswana, Mheshimiwa Dkt. Mokgweetsi Eric Keabetswe Masisi (wa pili kushoto) akisikiliza maelezo kutoka kwa mmoja wa Watendaji wa kiwanda cha Azam alipotembelea kiwanda hicho kilichopo Buguruni jijini Dar es Salaam, ili kujionea uwekezaji unaofanywa na Wawekezaji binafsi wa Kitanzania. Katika ziara hiyo Mheshimiwa Dkt. Masisi aliambatana na Waziri wa Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki Mhe. Balozi Liberata Mulamula (Mb).
Rais wa Jamhuri ya Botswana, Mheshimiwa Dkt. Mokgweetsi Eric Keabetswe Masisi  akiwa ameambatana na Waziri wa Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki Mhe. Balozi Liberata Mulamula (Mb) wakilakiwa na baadhi ya Watendaji wa Kiwanda cha kusaga nafaka cha Azam waliopowasili kiwandani hapo kwa lengo la kujionea uwekezaji unaofanywa na Wawekezaji binafsi wa Kitanzania.

Rais wa Jamhuri ya Botswana, Mheshimiwa Dkt. Mokgweetsi Eric Keabetswe Masisi  na Waziri wa Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki Mhe. Balozi Liberata Mulamula (Mb) wakiwasili katika kiwanda cha Azam kilichopo Buguruni jijini Dar es Salaam
Rais wa Jamhuri ya Botswana, Mheshimiwa Dkt. Mokgweetsi Eric Keabetswe Masisi akizungumza na baadhi ya Watendaji (hawapo pichani) wa Kiwanda cha Azam
Rais wa Jamhuri ya Botswana, Mheshimiwa Dkt. Mokgweetsi Eric Keabetswe Masisi  ameondoka nchini leo Juni 11, 2021 baada ya kuhitimisha ziara yake ya siku mbili.