Friday, June 11, 2021

RAIS WA JAMHURI YA BOTSWANA MHE. DKT. MASISI ATEMBELEA KIWANDA CHA KUSAGA NAFAKA CHA AZAM


Rais wa Jamhuri ya Botswana, Mheshimiwa Dkt. Mokgweetsi Eric Keabetswe Masisi (wa pili kushoto) akisikiliza maelezo kutoka kwa mmoja wa Watendaji wa kiwanda cha Azam alipotembelea kiwanda hicho kilichopo Buguruni jijini Dar es Salaam, ili kujionea uwekezaji unaofanywa na Wawekezaji binafsi wa Kitanzania. Katika ziara hiyo Mheshimiwa Dkt. Masisi aliambatana na Waziri wa Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki Mhe. Balozi Liberata Mulamula (Mb).
Rais wa Jamhuri ya Botswana, Mheshimiwa Dkt. Mokgweetsi Eric Keabetswe Masisi  akiwa ameambatana na Waziri wa Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki Mhe. Balozi Liberata Mulamula (Mb) wakilakiwa na baadhi ya Watendaji wa Kiwanda cha kusaga nafaka cha Azam waliopowasili kiwandani hapo kwa lengo la kujionea uwekezaji unaofanywa na Wawekezaji binafsi wa Kitanzania.

Rais wa Jamhuri ya Botswana, Mheshimiwa Dkt. Mokgweetsi Eric Keabetswe Masisi  na Waziri wa Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki Mhe. Balozi Liberata Mulamula (Mb) wakiwasili katika kiwanda cha Azam kilichopo Buguruni jijini Dar es Salaam
Rais wa Jamhuri ya Botswana, Mheshimiwa Dkt. Mokgweetsi Eric Keabetswe Masisi akizungumza na baadhi ya Watendaji (hawapo pichani) wa Kiwanda cha Azam
Rais wa Jamhuri ya Botswana, Mheshimiwa Dkt. Mokgweetsi Eric Keabetswe Masisi  ameondoka nchini leo Juni 11, 2021 baada ya kuhitimisha ziara yake ya siku mbili.


No comments:

Post a Comment

Note: Only a member of this blog may post a comment.