Wednesday, June 23, 2021

NAIBU WAZIRI MAMBO YA NJE WA POLAND MHE.PAWEL JABLONSKI AWASILI JIJINI DODOMA




Naibu Waziri Mambo ya Nje wa Poland anayehusika na masuala ya Siasa, Uchumi na Maendeleo kwa nchi za Afrika Mhe.Pawel Jablonski awasili jijini Dodoma kwa ziara ya kikazi.



Naibu Waziri Mambo ya Nje wa Poland anayehusika na masuala ya Siasa, Uchumi na Maendeleo kwa nchi za Afrika Mhe.Pawel Jablonski akiwa na Balozi wa Tanzania nchini Ujerumaani Mhe. Dkt. Abdallaah Possi katika uwanja wa ndege jijini Dodoma.

Naibu Waziri Mambo ya Nje wa Poland anayehusika na masuala ya Siasa, Uchumi na Maendeleo kwa nchi za Afrika Mhe.Pawel Jablonski akiwa na Balozi wa Poland nchini Mhe. Krzysztof Buzalski

Ujumbe wa wafanyabiashara na wawekezaji kutoka nchii Poland ulioambatana na Naibu Waziri wa Mambo ya Nje anayeshughulikia Naibu Waziri Mambo ya Nje wa Poland anayehusika na masuala ya Siasa, Uchumi na Maendeleo kwa nchi za Afrika ambaye yuko nchni kwa ziara ya kikazi kufuatiaa mwaliko wa Wizara ya Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki  



Naibu Waziri Mambo ya Nje wa Poland anayehusika na masuala ya Siasa, Uchumi na Maendeleo kwa nchi za Afrika Mhe.Pawel Jablonski awasili jijini Dodoma kwa ziara ya kikazi.

Mhe. Powel  ameambatana na Balozi wa Tanzania nchini Ujerumani Dkt. Abdallah Possi pamoja na Balozi wa Poland hapa nchini Mhe. Krzysztof Buzalski. 

Naibu Waziri huyo atakutana na kufanya mazungumzo ya pamoja na watendaji wa Wizara za Elimu, Sayansi na Teknolojia, Maji, Uwekezaji, Viwanda na Biashara, Uwekezaji, Kilimo na Fedha na Mipango hapa jijini Dodoma. 

Naibu Waziri huyo ameambatana na timu ya wawekezaji na wafanyabiashara  waliobobea katika maeneo ya teknolojia ya kisasa katika sekta za kibenki (smart teknologies) teknolojia ya kisasa katika sekta ya umeme (smart technologies for electricity sector -smart meter connection and lighting systems) na ulipaji kwa kutumia teknolojia za kisasa ( smart payment apps). 

Wataalamu hao wakiwa jijini Dar es Salaam watakutana na Ofisi ya Mkuu wa  Mkoa wa Dar es Salaam, TANESCO, TPSF, Benki za CRDB, NMB na NSSF



No comments:

Post a Comment

Note: Only a member of this blog may post a comment.