Wednesday, June 2, 2021

BALOZI SOKOINE AKUTANA NA KUFANYA MAZUNGUMZO NA BALOZI WA RWANDA NCHINI

Balozi Joseph Edward Sokoine, Katibu Mkuu Wizara ya Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki leo tarehe 2 Juni, 2021 amekutana na kufanya mazungumzo na Mhe. Meja Generali Charles Karamba, Balozi wa Rwanda nchini Tanzania. 

Balozi Karamba amefika Ofisini kwa Katibu Mkuu kwa lengo la kujitambulisha kwake, na kumpongeza kwa kuteuliwa kuwa Katibu Mkuu wa Wizara ya Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki.

Balozi Sokoine kwa upande wake amemwahidi Balozi Karamba ushirikiano katika utekelezaji wa majukumu yake ili kuimarisha zaidi uhusiano kati ya Tanzania na Rwanda. 

Aidha, Balozi Karamba ameeleza kuridhishwa kwake na namna Bandari ya Dar-es- Salaam inavyoshughulikia kwa haraka upitishaji wa bidhaa na mizigo ya Rwanda inayopitia katika Bandari hiyo, jambo ambalo linachochea ukuaji wa biashara kati ya Tanzania na Rwanda.

Mheshimiwa Meja Generali Charles Karamba Balozi wa Rwanda nchini Tanzania akisaini kitabu cha wageni alipowasili katika Ofisi za Wizara ya Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki jijini Dodoma.

Mazungumzo yakiendelea.

Balozi Joseph Edward Sokoine Katibu Mkuu Wizara ya Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki akiwa katika picha ya pamoja na Mheshimiwa Meja Generali Charles Karamba Balozi wa Rwanda nchini Tanzania.
Balozi Joseph Edward Sokoine Katibu Mkuu Wizara ya Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki akielezea jambo wakati wa mazungumzo na Mheshimiwa Meja Generali Charles Karamba Balozi wa Rwanda nchini Tanzania.
Mheshimiwa Meja Generali Charles Karamba Balozi wa Rwanda nchini Tanzania akielezea jambo wakati wa mazungumzo na Balozi Joseph Edward Sokoine Katibu Mkuu Wizara ya Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki.

Wakati huohuo Waheshimiwa Mabalozi Wastaafu waliowahi kuiwakilisha Nchi sehemu mbalimbali duniani wamekutana na kufanya mazungumzo Watendaji wa Wizara ya Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki kwa lengo la kubadilishana uzoefu katika musuala Diplomasia na Mahusiano ya Kimataifa.  
Mheshimiwa Balozi Begum Taji akifuatilia mazungumzo yaliyokuwa yakiendelea.
Mheshimiwa Balozi Christopher C. Liundi akizungumza wakati wa kikao kati ya Mabalozi Wastaafu na Watendaji wa Wizara.
Sehemu ya Watendaji wa Wizara wakifuatilia kikao
Mkurugenzi wa Utawala na Usimamizi Rasilimali Watu Bw. Alex B.D.J Mfungo akielezea jambo wakati wa kikao kati ya Mabalozi Wastaafu na Watendaji wa Wizara


 

No comments:

Post a Comment

Note: Only a member of this blog may post a comment.