Saturday, June 26, 2021

BALOZI MULAMULA AKUTANA NA WAWAKILISHI WA St. EGIDIO

 

Waziri wa Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki Mhe. Balozi Liberata Mulamula akionesha zawadi iliyotolewa na wawakilishi wa Jumuiya ya St. Egidio ya nchini Italia walipomtembelea ofisini kwake jijini Dodoma tarehe 25/06/2021.


Waziri wa Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki Mhe. Balozi Liberata Mulamula akiangalia zawadi iliyotolewa na wawakilishi wa Jumuiya ya St. Egidio ya nchini Italia walipomtembelea ofisini kwake jijini Dodoma tarehe 25/06/2021.


Waziri wa Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki Mhe. Balozi Liberata Mulamula akizungumza na wawakilishi wa Jumuiya ya St. Egidio ya nchini Italia walipomtembelea ofisini kwake jijini Dodoma tarehe 25/06/2021.

mazungumzo yakiendelea

Mmoja wa wawakilishi wa Jumuiya ya St. Egidio ya nchini Italia Bw. Andrea Bartoli akizungumza wakati wawakilishi hao walipomtembelea Balozi Mulamula ofisini kwake jijini Dodoma tarehe 25/06/2021






Waziri wa Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki Mhe. Balozi Liberata Mulamula (Mb) amekutana na kufanya mazungumzo na wawakilishi wa Jumuiya ya Mtakatifu Egidio ya nchini Italia.

Katika mazungumzo hayo wawakilishi wa Jumuiya hiyo wakiongozwa na Bw. Andrea Bartoli wamemuhakikishia Mhe. Waziri Mulamula kuwa Jumuiya yao itaendelea na kazi ya kuhakikisha amani inatamalaki katika nchi mbalimbali barani Afrika ikiwemo Tanzania.

Akizungumza nao Mhe. Waziri amewahakikishia wawakilishi hao kwamba Tanzania itaendelea kuwaunga mkono katika harakati zao za kuwa na jamii salama kwani kufanya hivyo kunasaidia dunia kuwa salama.

Amewaomba kuendelea na kazi ya kuifahamisha jamii juu ya kazi zinazofanywa na Jumuiya hiyo katika sehemu mbalimbali nchini na barani Afrika kwa ujumla.

Jumuiya hiyo inajihusisha na masuala ya utafutaji wa amani kwa njia ya midahalo na mazungumzo ikiwa ni pamoja na kutoa misaada ya kijamii katika jumuiya mbalimbali nchini na katika Bara la Afrika.


No comments:

Post a Comment

Note: Only a member of this blog may post a comment.