Saturday, June 26, 2021

BALOZI MULAMULA AZINDUA BARAZA LA WAFANYAKAZI LA WIZARA

Waziri wa Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki Mhe. Balozi Liberata Mulamula (katikati) akiwa na viongozi wa Baraza la Wafanyakazi la Wizara wakiimba wimbo wa mshikamano daima alipowasili ukumbini kwa ajili ya kuzindua Baraza jipya la Wafanyakazi wa wizara jijini Dodoma tarehe 25/06/2021

Wajumbe wa Baraza la Wafanyakazi Wizara ya Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki wakiimba wimbo wa mshikamano daima baada ya mgeno rasmi kuwasili ukumbini kwa ajili ya kuzindua rasmi Baraza hilo jijini Dodoma 

Wajumbe wa Baraza la Wafanyakazi Wizara ya Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki wakiimba wimbo wa mshikamano daima baada ya mgeni rasmi kuwasili ukumbini kwa ajili ya kuzindua Baraza hilo jijini Dodoma 

Wajumbe wa Baraza la Wafanyakazi Wizara ya Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki katika picha ya pamoja na mgeni rasmi ambaye ni Waziri wa Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki Mhe. Liberata Mulamula mara baada ya kuzindua Baraza hilo jijini Dodoma tarehe 25/06/2021.
Wajumbe wa Baraza la Wafanyakazi Wizara ya Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki katika picha ya pamoja na mgeni rasmi ambaye ni Waziri wa Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki Mhe. Liberata Mulamula mara baada ya kuzindua Baraza hilo jijini Dodoma tarehe 25/06/2021.


wajumbe wa Baraza la Wafanyakazi Wizara ya Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki katika picha ya pamoja na Mhe. Waziri Mulamula

Wajumbe wa Baraza la Wafanyakazi Wizara ya Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki katika picha ya pamoja na mgeni rasmi ambaye ni Waziri wa Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki Mhe. Liberata Mulamula mara baada ya kuzindua Baraza hilo jijini Dodoma tarehe 25/06/2021.


Waziri wa Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki Mhe. Balozi Liberata Mulamula (Mb) amezindua Baraza jipya la Wizara na kuwataka wajumbe wa Baraza la Wafanyakazi wa Wizara kuwa mabalozi wazuri wa watumishi wa Wizara wanaowawakilisha.

Mhe. Waziri Mulamula ametoa rai hiyo jijini Dodoma alipokuwa akizindua Baraza hilo jijini Dodoma baada ya baraza la awali kumaliza muda wake.

Amesema kwamba uongozi wake kwa kushirikiana na watendaji wengine wa Wizara wako tayari kuyasikiliza na kuyafanyia kazi mapendekezo watakayoyapeleka kwa uongozi wa Wizara na kuwataka kuyafanyia kazi mapendekezo yanayotolewa na wafanyakazi ili yaweze kushughulikiwa.

Mhe. Waziri pia amewaambia wajumbe wa Baraza hio kwamba uongozi wake hautovumilia tabia au vitendo vya utovu wa nidhamu kama vile rushwa vitakavyolalamikiwa kufanywa na watumishi wa Wizara dhidi ya watu wanaowahudumia.

Amesema ni matarajio yake kwamba watumishi wa Wizara watakuwa waadilifu na wenye tabia njema wanapowahudumia wadau mbalimbali wa Wizara na hivyo kutekeleza majukumu yao kwa kufuata Sheria, Taratibu na Kanuni za Utumishi wa Umma na hivyo kutekeleza majukumu ya wizara ipasavyo.

Amesema kuwa Wizara imejipanga kuhakikisha inatoa vifaa na vitendea kazi kwa watumishi wake ili kuhakikisha utekelezaji wa majukumu ya Wizara unakamilika na kuwa na ufanisi.

Kikao hicho cha Baraza kiliwapitisha wajumbe wake katika mpango wa Bajeti wa mapato na matumizi ya wizara iliyopitishwa na Bunge mapema mwezi huu, kiliwachagua Bibi Judica Nagunwa kuwa Katibu na Bw. Hassan Mnondwa kuwa katibu Msaidizi wa Baraza hilo jipya ambalo litakaa madarakani kwa muda wa miaka mitatu.


No comments:

Post a Comment

Note: Only a member of this blog may post a comment.