Thursday, June 17, 2021

WAZIRI MULAMULA AFUNGUA MKUTANO WA MABALOZI WA EAC AZUNGUMZA NA VIONGOZI WA EAC JIJINI ARUSHA

Waziri wa Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki Mhe. Balozi Liberata  Mulamula akisaini kitabu cha wageni ofisini kwa Katibu Mkuu wa Jumuiya ya Afrika Mashariki (EAC) Dkt.Peter Mathuki muda mfupi baada ya kuwasili katika ofisi za makao makuu ya jumuiya hiyo jijiini Arusha leo.


Mhe. Waziri Mulamula  akiwa katika mazungumzo na Spika wa Bunge la Afrika Mashariki Mhe.Martin Ngoga  katika Makao Makuu ya jumuiya ya Afrika Mashariki jijini Arusha.

Rais wa Mahakama ya Afrika Mashariki Mh.Jaji Nestory Kayobera akimkabidhi Waziri Mulamula  machapisho mbalimbali yahusuyo Mahakama hiyo wakati Mhe. Waziri alipomtembela Rais huyo ofisini kwake makao makuu ya Mahakama hiyo iliyopo jijii Arsuha.

Rais wa Mahakama ya Afrika Mashariki Mh.Jaji Nestory Kayobera akimtembeza Mhe.Waziri Mulamula katika chumba cha Mahakama hiyo.

Mhe. Waziri Balozi Mulamulla akifungua Mkutano wa Mashauriano wa Mabalozi wa Jumuiya ya Afrika Mashariki uliofanyika jijini Arusha                                                                
  
  
Mhe. Waziri Balozi Mulamulla akifungua Mkutano wa Mashauriano wa Mabalozi wa Jumuiya ya Afrika Mashariki uliofanyika jijini Arusha leo

Waziri wa Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki Mhe. Balozi Liberata Mulamula (MB) ametembelea Makao Makuu ya Jumuiya ya Afrika Mashariki yaliyopo Jijii Arusha. 

Mhe. Balozi Mulamula amefungua Mkutano wa Mashauriano wa Mabalozi wa Jumuiya ya Afrika Mashariki na kukutana na kufanya mazungumzo na viongozi wakuu wa Taasisi za Jumuiya hiyo yenye makao yake Makuu jijini Arusha. 

Mhe. Mulamula kwanza amekutana na kufanya mazungumzo na Katibu Mkuu wa Jumuiya ya Afrika Mashariki Dkt.Peter Mathuki na baadaye amekutana na kufanya mazungumzo na Rais wa Mahakama ya Afrika Mashariki Mhe. Jaji Nestory Kayobera katika Makao Makuu ya jumuiya hiyo. 

Katika ziara hiyo Mhe. Waziri Mulamula pia amekutana na kufanya mazungumzo na Spika wa Bunge la Afrika Mashariki Mhe.Martin Ngoga. Mikutano kati ya Mhe. Waziri na Mhe. Ngoga umefanyika katika Makao Makuu ya jumuiya ya Afrika Mashariki jijini Arusha.

No comments:

Post a Comment

Note: Only a member of this blog may post a comment.