Thursday, May 26, 2022

Canada Yaahidi Kushirikiana na Tanzania




Naibu Waziri wa Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki, Balozi Mbarouk N. Mbarouk akiwa katika mazungumzo na  Katibu wa Bunge wa Waziri wa Mambo ya Nje wa Canada, Mhe. Robert Oliphant yaliyofanyika jijini Dar Es Salaam



 Naibu Waziri wa Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki, Balozi Mbarouk N. Mbarouk na Katibu wa Bunge wa Waziri wa Mambo ya Nje wa Canada, Mhe. Robert Oliphant wakiwa katika picha ya pamoja na ujumbe wao baada ya mazungumzo yaliyofanyika jijini Dar Es Salaam.

Waziri wa Habari, Mawasiliano na Teknolojia ya Habari, Mhe. Nape Nnauye (kulia) akiwa katika mazungumzo na Katibu wa Bunge wa Waziri wa Mambo ya Nje wa Canada, Mhe. Robert Oliphant yaliyofanyika jijini Dar Es Salaam

Katibu wa Bunge wa Waziri wa Mambo ya Nje wa Canada, Mhe. Robert Oliphant  akisisitiza jambo wakati wa mazungumzo na Waziri wa Habari, Mawasiliano na Teknolojia ya Habari, Mhe. Nape Nnauye

Ujumbe wa Tanzania katika ukifuatilia mazungumzo kati ya Waziri wa Habari, Mawasiliano na Teknolojia ya Habari, Mhe. Nape Nnauye na Katibu wa Bunge wa Waziri wa Mambo ya Nje wa Canada, Mhe. Robert Oliphant. Wakwanza kushoto ni Mkurugenzi wa Kitengo cha Mawasiliano ya Serikali katika Wizara ya Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki, Balozi Mindi Kasiga na anayefuatia ni Mwakilishi wa Mkurugenzi wa Idara ya Ulaya na Amerika, Bi. Talha Mohammed

Waziri wa Habari, Mawasiliano na Teknolojia ya Habari, Mhe. Nape Nnauye na Katibu wa Bunge wa Waziri wa Mambo ya Nje wa Canada, Mhe. Robert Oliphant wakiwa katika picha ya pamoja na ujumbe wao baada ya mazungumzo yaliyofanyika jijini Dar Es Salaam

Waziri wa Maendeleo ya Jamii, Wanawake na Makundi Maalum, Dkt. Dorothy Gwajima akiwa katika mazungumzo na Katibu wa Bunge wa Waziri wa Mambo ya Nje wa Canada, Mhe. Robert Oliphant yaliyofanyika jijini Dar Es Salaam.

Katibu wa Bunge wa Waziri wa Mambo ya Nje wa Canada, Mhe. Robert Oliphant  akisisitiza jambo wakati wa mazungumzo na Waziri wa Maendeleo ya Jamii, Wanawake na Makundi Maalum, Dkt. Dorothy Gwajima jijini Dar Es Salaam.

Waziri wa Maendeleo ya Jamii, Wanawake na Makundi Maalum, Dkt. Dorothy Gwajima akisisitiza jambo wakati wa mazungumzo na  Katibu wa Bunge wa Waziri wa Mambo ya Nje wa Canada, Mhe. Robert Oliphant yaliyofanyika jijini Dar Es Salaam

Mkurugenzi wa Kitengo cha Mawasiliano ya Serikali katika Wizara ya Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki, Balozi Mindi Kasiga akieleza jambo wakati wa mazungumzo kati ya Waziri wa Maendeleo ya Jamii, Wanawake na Makundi Maalum, Dkt. Dorothy Gwajima na  Katibu wa Bunge wa Waziri wa Mambo ya Nje wa Canada, Mhe. Robert Oliphant

Waziri wa Maendeleo ya Jamii, Wanawake na Makundi Maalum, Dkt. Dorothy Gwajimana  na Katibu wa Bunge wa Waziri wa Mambo ya Nje wa Canada, Mhe. Robert Oliphant wakiwa katika picha ya pamoja na ujumbe wao baada ya mazungumzo yaliyofanyika jijini Dar Es Salaam

Katibu Mkuu wa Wizara ya Katiba na Sheria, Bibi Mary Makondo akiwa katika mazungumzo na Katibu wa Bunge wa Waziri wa Mambo ya Nje wa Canada, Mhe. Robert Oliphant yaliyofanyika jijini Dar Es Salaam.

Ujumbe wa Katibu wa Bunge wa Waziri wa Mambo ya Nje wa Canada, Mhe. Robert Oliphant ambaye unamjumuisha Balozi wa nchi hiyo hapa nchini, Mhe. Pamela O'Donnell (wa kwanza kulia) ukifutatilia mazungumzo kati ya Katibu Mkuu wa Wizara ya Katiba na Sheria, Bibi Mary Makondo na Katibu wa Bunge wa Waziri wa Mambo ya Nje wa Canada, Mhe. Robert Oliphant

Katibu wa Bunge wa Waziri wa Mambo ya Nje wa Canada, Mhe. Robert Oliphant  akisisitiza jambo wakati wa mazungumzo na Katibu Mkuu wa Wizara ya Katiba na Sheria, Bibi Mary Makondo

Mazungumzo kati ya Katibu Mkuu wa Wizara ya Katiba na Sheria, Bibi Mary Makondo na Katibu wa Bunge wa Waziri wa Mambo ya Nje wa Canada, Mhe. Robert Oliphant yanaendelea.







 

WATANZANIA WATAKIWA KUCHANGAMKIA FURSA ZA UFADHILI WA MASOMO ZINAZOTANGAZWA NA SERIKALI

Mkurugenzi wa Idara ya Ulaya na Amerika katika Wizara ya Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki, Balozi Swahiba Mndeme amewataka Watanzania kuendelea kuchangamkia fursa mbalimbali zikiwemo za ufadhali wa masomo zinazotangazwa na Serikali ili kunufaika nazo.


Balozi Mndeme ametoa rai hiyo leo tarehe 26 Mei 2022 jijini Dodoma alipokutana na wawakilishi wa vijana 26 wanaokwenda nchini Marekani kushiriki mafunzo chini ya Program ya YALI  kwa lengo la kuwaaga.


Amesema kuwa, Serikali kupitia Wizara mbalimbali ikiwemo Wizara ya Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki imeendelea kutangaza fursa mbalimbali zikiwemo za ajira na ufadhili wa masomo zinazopokelewa nchini kutoka nchi mbalimbali lakini bado mwitikio wa Watanzania wa kuchangamkia fursa hizo ni mdogo.


“Wizara imekuwa na utaratibu wa kutangaza fursa nyingi za ufadhili wa masomo zinazopokelewa kutoka nchi mbalimbali tunazoshirikiana nazo. Hata hivyo, bado fursa hizi hazijachangamkiwa ipasavyo. Nawaomba Watanzania mzichangamkie fursa hizi pale zinapotangazwa ili zitunufaishe” alisema Balozi Mndeme


Aidha, Balozi Mndeme aliwapongeza vijana hao kwa kufanikiwa kuchaguliwa kushiriki program hiyo ambayo inaheshimika duniani na kuwaeleza kuwa ni fursa nzuri kwao kuitumia kwa ajili ya kujifunza masuala mbalimbali yakiwemo yanayohusu Uongozi ili kupitia wao vijana wengine wengi wa Tanzania wanufaike. Pia aliwaasa kuwa Mabalozi wazuri wa Tanzania, kuzingatia nidhamu na kutanguliza maslahi ya nchi mbele wakati wote wakiwa nchini Marekani.


“Nawapongeza sana kwa kufanikiwa kupata fursa hii. Wizara inafurahi kuona vijana wa Kitanzania mmepata fursa hii kwani pamoja na kuwajenga pia ni ushahidi wa uhusiano mzuri uliopo kati ya Tanzania na Marekani. Nawaasa mkawe mabalozi wazuri wa Tanzania mzingatie nidhamu ili kulinda heshima na taswira nzuri ya nchi yetu” alisema Balozi Mndeme.


Kwa upande wao vijana hao waliishukuru na kuipongeza Wizara kwa ushirikiano iliowapatia na kuahidi kuzingatia mafunzo yote watakayoyapata wakiwa  Marekani kwa maslahi mapana ya nchi.


Program ya YALI (Young African Leaders Initiative) ilianzishwa na Serikali ya Marekani mwaka 2010 kwa lengo la kuwawezesha vijana kutoka mataifa ya Afrika kwenda nchini humo kujifunza masuala mbalimbali ya kuwajengea uwezo katika Uongozi. Vijana hao 26 wamechaguliwa kati ya Vijana wa Kitanzania 700 walioomba kujiunga na Program hiyo kwa mwaka 2022. 

Mkurugenzi wa Idara ya Ulaya na Amerika katika Wizara ya Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki, Balozi Swahiba Mndeme akizungumza wakati wa kikao kifupi cha kuwaaga  Vijana 26 wa Kitanzania (hawapo pichani) waliopata fursa ya kushiriki mafunzo nchini Marekani kupitia Program ya Young African Leaders Initiative (YALI)  kwa mwaka 2022. Pamoja na mambo mengine aliwaasa vijana hao kuwa mabalozi wazuri wa Tanzania  nchini Marekani ili kulinda heshima ya nchi. Kikao hicho kimefanyika jijini Dodoma tarehe 26 Mei 2022.

Mmoja wa vijana watakaoshiriki program ya YALI Bi. Victoria akizungumza wakati wa mkutano kati yao na Balozi Mndeme (hayupo pichani)
Sehemu ya wawakilishi wa vijana 26 wa Kitanzania watakaoshiriki program ya YALI nchini Marekani wakimsikiliza Balozi Mndeme (hayupo (ichani)
Sehemu nyingine ya vijana hao wakati wa mkutano kati yao na Balozi Mndeme
Vijana watakaoshiriki program ya YALI nchini Marekani wakifuatilia mazungumzo kati yao na Balozi Mndeme
Sehemu ya vijana hao wakati wa kikao cha kuwaaga 
Vijana watakaoshiriki program ya YALI nchini Marekani wakimsikiliza Balozi Mndeme alipozungumza nao kwa ajili ya kuwaaga
Balozi Mndeme akiwa katika picha ya pamoja na baadhi ya wawakilishi wa vijana 26 watakaoshiriki program ya YALI nchini Marekani
Picha ya pamoja
Picha ya pamoja



 

Wednesday, May 25, 2022

WAZIRI MULAMULA ASHIRIKI MKUTANO WA BARAZA LA MAWAZIRI AU

Na Mwandishi wetu, Malabo


Waziri wa Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki, Balozi Liberata Mulamula (Mb) ameshiriki Mkutano wa Baraza la Mawaziri wa Mambo ya Nje la Umoja wa Afrika (AU) ulioanza leo Jijini Malabo, Equatorial Guinea.

Kufanyika kwa mkutano huo ni utekelezaji wa maamuzi ya Mkutano wa 35 wa Wakuu wa Nchi na Serikali wa Umoja wa Afrika uliofanyika tarehe 6 - 7 Februari 2022 Jijini Addis Ababa, Ethiopia.

Mkutano wa Baraza la Mawaziri ulitanguliwa na Mkutano wa Kisekta wa Mawaziri wanaoshughulika na Wakimbizi, Wahamaji na Majanga ya Kibinadamu uliofanyika kuanzia tarehe 23 - 24 Mei, 2022 Jijini Malabo.

Mkutano huo pamoja na mambo mengine, jukumu lake kubwa ni kuandaa Mkutano Maalum wa 16 wa Wakuu wa Nchi na Serikali wa Umoja wa Afrika kuhusu majanga ya kibinadamu pamoja na masuala ya mapambano dhidi ya ugaidi na mabadiliko ya serikali yasiyozingatia Katiba unaotarajiwa kufanyika tarehe 27 – 28 Mei, 2022 Jijini Malabo.

Akiongea wakati wa Ufunguzi wa Mkutano huo, Mwenyekiti wa Kamisheni ya Umoja wa Afrika, Bw. Moussa Faki Mahamat alisema kuwa mkutano huo ni mahsusi katika kujadili changamoto mbalimbali za majanga ya kibinadamu pamoja na mapambano dhidi ya ugaidi na mabadiliko ya Serikali yasiyozingatia katiba

“Mkutano huu unafanyika wakati Afrika linapita katika changamoto nyingi ikiwa ni pamoja na za majanga ya kibinadamu,” alisema Bw. Mahamat

Aidha, Bw. Mahamat aliongeza kuwa ugaidi bado ni changamoto na mabadiliko ya Serikali yasioyofuata misingi ya katiba ambayo yametokea miaka ya hivi karibuni yamerudisha nyuma taratibu za kidemokrasia katika chaguzi katika Bara la Afrika. 

Waziri wa Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki, Balozi Liberata Mulamula akishiriki Mkutano wa Baraza la Mawaziri wa Mambo ya Nje la Umoja wa Afrika (AU) ulioanza leo Jijini Malabo, Equatorial Guinea


Waziri wa Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki, Balozi Liberata Mulamula akiteta jambo na aliyekuwa Waziri wa Mambo ya Nje wa Burundi, Balozi Alain Nyamitwe wakati wa Mkutano wa Baraza la Mawaziri wa Mambo ya Nje la Umoja wa Afrika (AU) ulioanza leo Jijini Malabo, Equatorial Guinea


Waziri wa Mambo ya Nje wa Malawi, Mhe. Nancy Gladys Tembo akizungumza na Waziri wa Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki, Balozi Liberata Mulamula katika Mkutano wa Baraza la Mawaziri wa Mambo ya Nje la Umoja wa Afrika (AU) ulioanza leo Jijini Malabo, Equatorial Guinea


Waziri wa Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki, Balozi Liberata Mulamula akipata maelezo kutoka kwa Balozi wa Tanzania nchini Ethiopia, Balozi Innocent Shiyo kabla ya kuanza kwa Mkutano wa Baraza la Mawaziri wa Mambo ya Nje la Umoja wa Afrika (AU) uliofanyika Jijini Malabo, Equatorial Guinea


Waziri wa Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki, Balozi Liberata Mulamula akipata ufafanuzi kutoka kwa Balozi wa Tanzania nchini Ethiopia, Balozi Innocent Shiyo (kulia) na Mkurugenzi wa Idara ya Afrika katika Wizara ya Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki, Balozi Naimi Aziz kabla ya kuanza kwa mkutano wa Baraza la Mawaziri wa Mambo ya Nje la Umoja wa Afrika (AU) uliofanyika Jijini Malabo, Equatorial Guinea


Mwenyekiti wa Kamisheni ya Umoja wa Afrika, Bw. Moussa Faki Mahamat akiwasilisha hotuba yake wakati wa ufunguzi wa Baraza la Mawaziri wa Mambo ya Nje la Umoja wa Afrika (AU) uliofanyika Jijini Malabo, Equatorial Guinea 


Waziri wa Mambo ya Nje wa Senegal, Mhe. Aïssata Tall Sall akihutubia washiriki wa Mkutano wa Baraza la Mawaziri wa Mambo ya Nje la Umoja wa Afrika (AU) uliofanyika Jijini Malabo, Equatorial Guinea  


Sehemu ya Ujumbe wa Tanzania ukishiriki katika Mkutano


Mkutano ukiendelea 


Waziri wa Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki, Balozi Liberata Mulamula akiwa katika picha ya pamoja na baadhi ya ujumbe wa Tanzania baada ya kumalizika kwa mkutano


Mawaziri wa Mambo ya Nje Mambo ya Nje wa Umoja wa Afrika (AU) wakiwa katika picha ya pamoja baada ya kumaliza mkutano wao  



BALOZI SOKOINE AKUTANA NA BALOZI WA ANGOLA NCHINI

 

 

Balozi wa Angola nchini Mhe. Sandro de Oliveira (katikati) akisaini kitabu cha wageni baada ya kuwasili katika Ofisi za Wizara jijini Dodoma kulia ni mwenyeji wake Katibu Mkuu Wizara ya Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki Balozi Joseph Sokoine

  

Katibu Mkuu Wizara ya Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki Balozi Joseph Sokoine akiangalia nyaraka wakati alipokutana na Balozi wa Angola nchini Mhe. Sandro de Oliveira katika Ofisi za Wizara jijii Dodoma

Balozi wa Angola nchni Mhe. Sandro de Oliveira akizungumza wakati alipokutana na Katibu Mkuu Wizara ya Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki Balozi Joseph Sokoine katika ofisi za Wizara jijini Dodoma.
  

Katibu Mkuu Wizara ya Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki Balozi Joseph Sokoine      (kulia) akizungumza na  Balozi wa Angola nchini Mhe. Sandro de Oliveira (kushoto) walipokutana katika Ofisi za Wizara jijii Dodoma

Mazungumzo kati ya Katibu Mkuu Wizara ya Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki Balozi Joseph Sokoine na Balozi wa Angola nchini Mhe. Sandro de Oliveira yakiendelea katika Ofisi za Wizara jijini Dodoma

 

 


 

Katibu Mkuu Wizara ya Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki Balozi Joseph Sokoine amekutana na kufanya mazungumzo na Balozi wa Angola nchini Mhe. Sandro de Oliveira katika Ofisi za Wizara jijini Dodoma.

Akizungumza katika kikao hicho Katibu Mkuu Wizara ya Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki Balozi Joseph Sokoine amemuhakikishia Mhe. Balozi Sandro de Oliveira utayari wa Tanzania katika kuendelea kushirikiana na Angola katika kukuza na kuimarisha uhusiano baina ya nchi hizo.

‘’Mhe. Balozi, nikuhakikishie kwamba Tanzania itaendelea kushirikiana na Angola ili kuimarisha na kukuza uhusiano kati ya Tanzania na Angola na kuongeza kuwa Tanzania inadhamiria kuufikisha uhusiano huo mbali zaidi,’’ alisema Balozi Sokoine.

Naye Balozi Sandro amemshukuru Balozi Sokoine kwa mazungumzo yao na kuahidi kwamba Angola itaendelea kushirikiana na Tanzania ili kuendelea kuulinda uhusiano ambao uliasisiwa na viongozi wa mataifa hayo.

Viongozi hao wamekubaliana kuendela kuimarisha uhusiano wa karibu na wa kindugu  uliopo kati ya Tanzania na Angola ambao umekuwepo kwa miaka mingi ulioasisiwa na waasisi wa mataifa hayo Hayati Mwalimu Julius Nyerere na Hayati Antonio Agustino Neto ikiwa  ni pamoja na Tanzania kukisaidia Chama cha MPLA cha Angola kupigania uhuru wa nchi hiyo.

Viongozi hao pia wamekubaliana kuendelea kushirikiana katika sekta mbalimbali za kidiplomasi, kiuchumi, kisiasa na kijamii ikiwa ni pamoja na kufanya kazi kwa pamoja na kushughulikia changamoto zinazojitokeza katika sekta mbalimbali ili kuchochea  ukuaji wa uchumi baina ya nchi

 

 


Monday, May 23, 2022

MKUTANO WA 19 WA MAWAZIRI WA AFRIKA NA NORDIC KUFANYIKA JUNI 2022 FINLAND

Na Mwandishi wetu, Dar

Mkutano wa 19 Mawaziri wa Mambo ya Nchi za Nje kutoka katika Bara la Afrika na Nordic  unatarajiwa kufanyika Helsinki, Finland kuanzia tarehe 13 – 15 Juni, 2022. Mkutano huo utakutanisha Mawaziri wa Mambo ya Nchi za Nje kutoka katika bara la Afrika na nchi za Finland, Norway Denmark,  Iceland.

Balozi wa Finland nchini Mhe. Riitta Swan amebainisha hayo alipokutana kwa mazungumzo na Waziri wa Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki, Balozi Liberata Mulamula (Mb) katika Ofisi Ndogo za Wizara Jijini Dar es Salaam

Mhe.  Swan amesema mkutano huo utajadili masula ya amani na usalama, maendeleo endelevu na ushirikiano kati ya nchi za NORDIC  na Afrika. 

“Mkutano huo utajadili masuala ya amani na usalama, kuhusu umuhimu wa umini pamoja maendeleo endelevu na mabadiliko ya tabia nchi,” amesema Balozi Swan.

Kwa upande wake Waziri wa Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki, Balozi Liberata Mulamula amesema mkutano huo 

umekuwa ukifanyika kila mwaka lakini kutokana na Janga la ugonjwa wa Uviko 19,  mkutano huo haujafanyika tangu ulipofanyika mara ya mwisho nchini mwaka 2019.

Katika tukio jingine, Balozi Mulamula amekutana kwa mazungumzo na Balozi wa Marekani nchini Dkt. Donald Wright.

Pamoja na mambo mengine, viongozi hao wamejadili masuala ya ushirikiano baina ya Tanzania na Marekani katika sekta za Afya, Elimu, biashara na uwekezaji.

Waziri wa Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki, Balozi Liberata Mulamula akimsikiliza Balozi wa Finland nchini Mhe. Riitta Swan walipokutana kwa mazungumzo katika Ofisi Ndogo za Wizara Jijini Dar es Salaam

Mkurugenzi wa Kitengo cha Mawasiliano ya Serikali katika Wizara ya Mambo ya Nje na Ushiurikiano wa Afrika Mashariki, Balozi Mindi Kasiga pamoja na Kaimu Mkurugenzi Idara ya Ulaya na Amerika, Bibi. Talha Waziri wakifuatilia kikao cha Mhe. Waziri Mulamula na Balozi wa Finland

Waziri wa Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki, Balozi Liberata Mulamula akizungumza na Balozi wa Marekani hapa nchini, Dkt. Donald Wright 

Waziri wa Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki, Balozi Liberata Mulamula katika picha ya pamoja na Balozi wa Marekani hapa nchini, Dkt. Donald Wright. Kulia mwa Balozi Mulamula ni Mkurugenzi wa Kitengo cha Mawasiliano ya Serikali katika Wizara ya Mambo ya Nje na Ushiurikiano wa Afrika Mashariki, Balozi Mindi Kasiga pamoja na Kaimu Mkurugenzi Idara ya Ulaya na Amerika, Bibi. Talha Waziri na Afisa kutoka Wizarani Bibi. Kisa Mwaseba.