Thursday, August 7, 2014

Mkurugenzi wa Ushirikiano wa Kimataifa azungumza na Mwakilishi wa UNFPA nchini

Mkurugenzi wa Idara ya Ushirikiano wa Kimataifa katika Wizara ya Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Kimataifa, Balozi Celestine Mushy akizungumza na Mwakilishi wa Shirika la Umoja wa Mataifa linaloshughulikia Idadi ya Watu (UNFPA) hapa nchini, Dkt. Nathalia Kanem alipofika Ofisini kwake kwa ajili ya kuzungumzia masuala mbalimbali yanayohusu idadi ya watu na maendeleo. 
Dkt. Kanem  akichangia jambo wakati wa mazungumzo na Balozi Mushy.
Bibi Samira Diria, Afisa Mambo ya Nje akinukuu mazungumzo kati ya Balozi Mushy na Dkt. Kanem (hawapo pichani). Mwingine katika picha ni Afisa kutoka UNFPA nchini.

Picha na Reginald Philip

No comments:

Post a Comment

Note: Only a member of this blog may post a comment.