Friday, August 29, 2014

Naibu Waziri wa Mambo ya Nje wa Japan afanya ziara nchini

Katibu Mkuu wa Wizara ya Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Kimataifa Bw. John Haule akisalimiana na Naibu Waziri wa Mambo ya Nje kutoka Japan Mhe. Hirotaka Ishihara mara baada ya kuwasili katika Uwanja wa Ndege wa Kimataifa wa Julius Nyerere Jijini Dar es Salaam kwa ziara ya kikazi ya siku tatu hapa nchini. Katika ziara hiyo Mhe. Ishihara amembatana na ujumbe wa Wafanyabiashara kutoka Japan.Anayeshuhudia katikati ni Kaimu Mkurugenzi wa Idara ya Asia na Australasia, Bw. Nathaniel Kaaya.
Katibu Mkuu wa Wizara ya Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Kimataifa, Bw. hAULE  pamoja na Naibu  Waziri wa Mambo ya Nje wa Japan Mhe. Ishihara wakimsikiliza Balozi wa Japan nchini Mhe. Masaki Okada alipokuwa akiwaeleza jambo mara baada ya mapokezi ya Mhe. Ishihara.


Picha na Reginald Philip.

No comments:

Post a Comment

Note: Only a member of this blog may post a comment.