Wednesday, January 28, 2015

NEPAD yasaidia harakati za kutafuta tiba na chanjo ya ugonjwa wa Ebola, Prof. Ambali

Naibu Waziri wa Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Kimataifa, Mhe. Dkt. Mahadhi Juma Maalim (Mb) kulia akiongea na mmoja wa viongozi wa Wizara ya Mambo ya Nje ya Argentina walipokutana jijini Addis Ababa katika Mkutano wa Wakuu wa Nchi na Serikali wa Umoja wa Afrika.


Na Ally Kondo, Addis Ababa

Nchi za Afrika zimehimizwa kuweka mazingira mazuri na wezeshi kwa ajili ya kufanya tiba na chanjo za maribio dhidi ya ugonjwa wa Ebola. Kauli hiyo ilitolewa na Mkuu na Mshauri wa Kituo cha Sayansi, Teknolojia na Ubunifu cha NEPAD, Prof. Aggrey Ambali  wakati alipokuwa anawasilisha mada kuhusu ugonjwa wa Ebola kwenye kikao cha Kamati ya Uongozi wa NEPAD jijini Addis Ababa siku ya Jumanne tarehe 27 Januari 2015.

Prof. Ambali alieleza kuwa mashirika mengi yanayohusika na udhibiti wa madawa barani Afrika yanakabiliwa na ugumu wa kushughulikia masuala ya kimaadili na kanuni zinazosimamia tiba za majaribio kwenye nchi wanachama.

Alitoa mfano wa masuala ya kimaadili na kisera ambayo yanahitaji ufumbuzi ili kuwezesha kukusanya na kusafirisha damu na plasma kwenye nchi zinazohusika.

Kwa kuliona hilo, NEPAD kupitia Programu ya Afrika ya Kuoanisha Kanuni za Udhibiti wa Madawa inafanya kazi kwa kushirikiana na Jumuiya za Kikanda pamoja na Mashirika ya Kitaifa ya Udhibiti wa Madawa ili kupata nguvu inayohitajika ya kusimamia tiba za majaribio na kushughulikia masuala ya kimaadili

Kwa msaada wa NEPAD na Shirika la Afya Duniani, Jumuiya ya Afrika Mashariki inafanya tathmini ya pamoja ya chanjo ya Ebola ambayo itafanyika tarehe 02 – 04 Februari 2015. Nchi zinazolengwa kwa ajili ya majaribio hayo ni Tanzania, Uganda na Kenya lakini tathmini ya pamoja itafanywa na nchi zote za EAC.

Prof. Ambali alihitimisha mada yake kwa kusema kuwa tiba za majaribio kwa ajili ya chanjo mbili za Ebola yanafanyika huko Afrika Magharibi na majaribio mengine kadhaa yanatarajiwa kufanyika hivi klaribuni. 


No comments:

Post a Comment

Note: Only a member of this blog may post a comment.