Wednesday, January 28, 2015

Waziri Membe akagua majengo ya mapya Ubalozi wa Tanzania nchini Paris

Majengo (mawili ya katikati) ya Ubalozi wa Tanzania Paris Ufaransa kama yanavyoonekana kwa nje siku ya uzinduzi rasmi tarehe 28 Januari 2015.

Mhe. Bernard Membe, Waziri wa Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Kimataifa akipata maelezo kutoka kwa Katibu Mkuu wa Wizara Bw. John Haule wakati viongozi hao wakiwa kwenye maandalizi ya mwisho kabla ya uzinduzi rasmi unaotarajiwa kufanyika baadae leo na Mhe. Jakaya Mrisho Kikwete, Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania. 

Mhe. Membe akiwa na Katibu Mkuu wa Wizara ya Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Kimataifa Bw. John Haule kwenye ukaguzi wa nyumba ya makazi ya balozi ikiwa ni sehemu ya majengo mawili (ofisi za ubalozi na makazi ya balozi) yatakayozinduliwa baadaye leo na Mhe. Jakaya Mrisho Kikwete, Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania. 

No comments:

Post a Comment

Note: Only a member of this blog may post a comment.