Wednesday, January 28, 2015

Tanzania na China kuendeleza ushirikiano katika Maeneo Maalum ya Uwekezaji


Mkurugenzi wa Eneo la  Mamlaka ya Ukanda Maalum wa Uwekezaji (EPZA) nchini, Kanali Mstaafu Joseph Simbakalia akizungumza na Bw. Li Xuhang, Naibu Mkuu wa masuala ya Siasa katika Ubalozi wa China hapa nchini kuhusu mikakati ya Serikali ya Tanzanania katika kuhamasisha uwekezaji nchini katika Maeneo Maalum na kuimarisha ushirikiano na Serikali ya China katika masuala ya uwekezaji kwenye Maeneo Maalum. Mazungumzo  yao yalifanyika Wizara ya Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Kimataifa.
Sehemu ya Wajumbe kutoka Ubalozi wa China hapa nchini waliofuatana na Bw. Li Xuhang.
Ujumbe kutoka Wizara ya Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Kimataifa na EPZA wakifuatilia mazungumzo kati ya Kanali Mstaafu Simbakalia na Bw. Li Xuhang. Katikati ni Kaimu Mkurugenzi wa Idara ya Asia na Australasia, Bw. Nathaniel Kaaya, Bw. Lamau Mpolo (kushoto), Mkurugenzi wa Mipango na Maendeleo wa EPZA na  Bw. Iman Njalikai (kulia), Afisa Mambo ya Nje. 
Mazungumzo yakiendelea
Kanali Mstaafu Simbakalia akiwaeleza jambo Bw. Li na Afisa kutoka Ubalozi wa China mara baada ya mazungumzo yao.

Picha na Reuben Mchome







No comments:

Post a Comment

Note: Only a member of this blog may post a comment.