Monday, October 7, 2019

Simbu afuzu moja kwa moja kushiriki mashindano ya mwakani

Balozi wa Tanzania nchini Qatar, Mhe. Fatma Rajab akiwa na wakimbiaji wa Tanzania walioshiriki mbio za marathon jijini Doha, Qatar. wakimbiaji hao walienda Ubalozini kuaga kabla ya kuanza safari ya kurejea nyumbani.

Wakimbiaji wa Tanzania walimaliza rasmi mashindano ya mbio za Marathon na kwa bahati mbaya wanariadha wawili hawakuweza kumaliza mbio hizo kutokana na maumivu ya goti na misuli. Mwanariadha Alphonce Simbu ambaye alikuwa anatetea medali yake ya shaba alishika nafasi ya 16 na alikuwa miongoni mwa wakimbiaji 20 bora ambao wamefuzu moja kwa moja kushiriki mashindano ya mwakani.

Wakimbiaji wa Ethiopia walishinda medali za dhahabu na fedha na Mkenya alishinda medali ya shaba.

Kwa mujibu wa Balozi wa Tanzania nchini Qatar, Mhe. Fatma Rajab, Mwanariadha Simbu anaonekana ana uwezo mkubwa wa kuweza kushinda na amewasihi wakimbiaji hao waendelee kuwasiliana na ofisi ya Ubalozi ili kuwasaidia kupata ufadhili wa kuwajengea uwezo ikiwemo kupatiwa msaada wa mafunzo na vifaa.

No comments:

Post a Comment

Note: Only a member of this blog may post a comment.