Wednesday, October 9, 2019

UBALOZI WA TANZANIA NCHINI INDIA WAANZA MAJUKUMU YA UENYEKITI WA KUNDI LA MABALOZI KUTOKA NCHI ZA SADC WALIOPO NCHINI HUMO

Balozi wa Tanzania nchini India, Mhe. Baraka Luvanda akipokea Makabrasha kutoka kwa Balozi wa Namibia nchini India, Mhe. Gabriel P. Sinimbo ikiwa ni ishara ya kukabidhiwa uenyekiti wa Kundi la Mabalozi wa nchi za Jumuiya ya Maendeleo Kusini mwa Afrika (SADC ) waliopo India. Tanzania ilipokea uenyekiti wa Jumuiya hiyo kutoka kwa Namibia mwezi Agosti 2019 wakati wa Mkutano wa Wakuu wa Nchi na Serikali wa SADC uliofanyika jijini Dar es Salaam.
Balozi Luvanda (katikati) akizungumza mara baada ya kupokea uenyekiti wa kundi la Mabalozi kutoka Nchi za SADC waliopo India. Katika picha ni Balozi Sinimbo (kulia) kutoka Namibia na Balozi E.A Ferreira (kushoto) kutoka Msumbiji.
Mkutano ukiendelea
Mhe. Balozi Luvanda akiwa katika picha ya pamoja na na Mabalozi kutoka nchi za SADC waliopo India pamoja na Maafisa wa Ubalozi mara baada ya kikao cha Mabalozi hao kilichofanyika kwenye Jengo la Ubalozi jijini New Delhi.
Mhe. Balozi Luvanda akiwa katika picha ya pamoja na Balozi wa Zambia nchini India, Mhe. Judith K. Kapijimpanga ambaye kabla ya kuiwakilisha Zambia nchini India alihudumu katika nafasi hiyo nchini Tanzania.
Maafisa wa Ubalozi wa Tanzania, New Delhi, Dkt. Kheri Goloka (kushoto) na Bi. Natihaika Msuya (katikati) wakiwa katika picha ya pamoja na Mwenyekiti wa kundi la Mabalozi wa nchi za SADC nchini India aliyemaliza muda wake Balozi wa Namibia  Mhe. Gabriel P. Sinimbo.




No comments:

Post a Comment

Note: Only a member of this blog may post a comment.