Sunday, October 13, 2019

WIZARA YA MAMBO YA NJE YAKABIDHIWA JENGO JIPYA NA CHINA

Waziri wa Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki, Prof. Palamagamba John Kabudi (Mb) na Balozi wa China hapa Nchini, Balozi Wang Ke,wakikata utepe kuashiria ufunguzi rasmi wa Jengo jipya  la Wizara ya Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Masharii lililojengwa kwa ufadhili wa Serikali ya Jamhuri ya Watu China na kukabidhiwa Serikaali ya Tanzania. Tukio hilo limefanyika jijini Dar es Salaam. 

Naibu katibu Mkuu, Mizara ya Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki Balozi Ramadhani Mwinyi na Balozi wa China hapa Nchini, Balozi Wang Ke wakisaini mkataba wa makabidhiano ya jengo jipya la Wizara ya Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki. Anayeshuhudia ni Waziri wa Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki, Prof. Palamagamba John Kabudi (Mb).

Balozi wa China Nchini, Balozi Wang Ke akishikana mkono na Naibu katibu Mkuu, Wizara ya Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki Balozi Ramadhani Mwinyi mara baada ya kubadilishana nyaraka walizosaini za kukabidhiana Jengo jipya la Wizara ya Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki lililojengwa kwa msaada wa Jamhuri ya Watu wa China Jijini Dar es Salaam.

Balozi wa China hapa Nchini, Balozi Wang Ke akisoma hotuba yake wakati wa makabidhiano ya jengo jipya  la Wizara ya Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki yaliyofanyika jijini Dar es salaam

Waziri wa Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki, Prof. Palamagamba John Kabudi (Mb), akisoma hotuba yake wakati wa makabidhiano ya jengo jipya la Wizara ya Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki yaliyofanyika jijini Dar es salaam

Waziri wa Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki, Prof. Palamagamba John Kabudi (Mb), Balozi wa China nchini nchini Tanzania Wang Ke na Naibu Katibu Mkuu Wizara ya Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki wakiwa katika picha ya pamoja na baadhi ya watumishi wa Wizara ya Mambo ya Nje mara baada ya kukabidhiana jengo jipya la wizara hiyo.


Jengo jipya la Wizara ya Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki lililopo jijini Dar Es Salaam  lililojengwa kwa msaada wa Jamhuri ya Watu wa China kwa jailli ya matumizi ya Ofisi za Wizara hiyo.

No comments:

Post a Comment

Note: Only a member of this blog may post a comment.