Saturday, October 5, 2019

RAIS MAGUFULI AZINDUA KITUO CHA HUDUMA PAMOJA (OSBP) MPAKANI TUNDUMA/NAKONDE

Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mhe. Dkt. John  Pombe Magufuli, akiwa na Waziri wa Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki Mhe. Prof. Palamagamba John Kabudi (Mb), alipowasili katika Kituo cha Kutoa Huduma kwa Pamoja (OSBP) Mpakani Tunduma/Nakonde.

Kituo hicho kimefunguliwa leo tarehe 5 Oktoba 2019, na 
Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mhe. Dkt. John  Pombe Magufuli na Rais wa Jamhuri ya Zambia Mhe. Edgar Changwa Lungu.

Wakizungumza na mamia ya wananchi waliojitokeza katika zoezi la uzinduzi wa kituo hicho, kwa nyakati tofauti Mhe. Dkt. Magufuli na Mhe. Lungu walieleza kuwa wataendelea kudumisha uhusiano mzuri wa kidiplomasia uliodumu kwa muda mrefu baina ya nchi hizo mbili (Tanzania na Zambia) kwa maendeleo ya wananchi.

Aidha, Rais Magufuli alizungumzia umuhimu wa kuiongezea ufanisi Reli ya TAZARA ili kuchagiza kasi ya biashara baina ya Tanzania na Zambia.

Kadhalika, Mhe. Rais Magufuli amewahimiza Wananchi wa mji wa Tunduma kuulinda mpaka kwa kuepuka kujenga katika eneo la mpaka huo.

Wakati huo huo Waziri wa Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki amewapongeza Wananchi wa Mji wa Tunduma kwa kuendelea kulinda na kudumisha amani mpakani hapo. Vilevile ametumia fursa hiyo kuwasihi kuendelea na juhudi za kukuza biashara baina yao na Zambia ili kuboresha maisha yao.
Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mhe. Dkt. John  Pombe Magufuli akisalimiana na Katibu Mkuu wa Wizara ya Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki Dkt. Faraji Kasidi Mnyepe, alipowasili katika Kituo cha Kutoa Huduma kwa Pamoja (OSBP) Mpakani Tunduma/Nakonde kwa ajili ya ufunguzi.
Taswira ya Kituo cha Kutoa Huduma kwa Pamoja (OSBP) Mpakani Tunduma/Nakonde.
Taswira ya Kituo cha Kutoa Huduma kwa Pamoja (OSBP) Mpakani Tunduma/Nakonde.
Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mhe. Dkt. John  Pombe Magufuli, akizungumza na Waziri wa Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki Mhe. Prof. Palamagamba John Kabudi (Mb) alipowasili katika Kituo cha Kutoa Huduma kwa Pamoja Mpakani (OSBP) Tunduma/Nakonde
Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mhe. Dkt. John  Pombe Magufuli  akifuatilia maelezo kutoka  kwa Waziri Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki Mhe. Prof. Palamagamba John Kabudi (Mb) kabla ya kuanza kwa zoezi la ufunguzi wa Kituo cha Kutoa Huduma kwa Pamoja Mpakani (OSBP) Tunduma/Nakonde. 
Waziri Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki Mhe. Prof. Palamagamba John Kabudi (Mb)  akizungumza na wananchi (hawapo pichani) wakati wa ufunguzi wa Kituo cha Kutoa Huduma kwa Pamoja Mpakani (OSBP) Tunduma/Nakonde.
Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mhe. Dkt. John  Pombe Magufuli, na Rais wa Jamhuri ya Zambia Mhe. Edgar Changwa Lungu ,wakiangalia jiwe la msingi wakati wa zoezi la ufunguzi wa Kituo cha Kutoa Huduma kwa Pamoja (OSBP) mpakani Tunduma/Nakonde tarehe 5 Oktoba, 2019 
Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mhe. Dkt. John  Pombe Magufuli, na Rais wa Jamhuri ya Zambia Mhe. Edgar Changwa Lungu, pamoja na Wafadhili wa Ujenzi wa Kituo cha Kutoa Huduma kwa Pamoja (OSBP) mpakani Tunduma/Nakonde wakipanda mti katika zoezi la uzinduzi wa Kituo hicho 
Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mhe. Dkt. John  Pombe Magufuli na Rais wa Jamhuri ya Zambia Mhe. Edgar Changwa Lungu wakikata utepe kuashiria kufunguliwa rasmi kwa Kituo cha Kutoa Huduma kwa Pamoja (OSBP) mpakani Tunduma/Nakonde tarehe 05 Oktoba, 2019.

No comments:

Post a Comment

Note: Only a member of this blog may post a comment.