Friday, October 25, 2019

Mabalozi wa SADC, Qatar watoa wito kuiondolea vikwazo Zimbabwe.

Waheshimiwa Mabalozi wakiwa wanaendelea kutekeleza jukumu lao.
Baada ya kumaliza kazi wanapongezena kwa kushikana mikono ikiwa ni kiashiria cha mshikamamo hadi Zimbabwe inaondolewa vikwazo.


Balozi wa Tanzania nchini Qatar, Mhe. Fatma Rajab akiongea na Waheshimiwa Mabalozi wa Nchi za Eswatini na Afrika Kusini ambao wanaunda kundi la Mabalozi wa nchi za SADC nchini Qatar. Waheshimiwa Mabalozi walikuwa wanakamilisha mpango mkakati wa kutumia siku ya tarehe 25 Oktoba kama ilivyoamuliwa na Viongozi wa Nchi za SADC kupaza sauti kwa njia mbalimbali kutoa wito kwa nchi za Magharibi kuiondolea vikwazo vya uchumi ilivyowekewa Zimbabwe. Mabalozi hao wamepanga kupeleka Waraka wa Kidiplomasia Wizara ya Mambo ya Nje ya Qatar, Balozi za EU na Ubalozi wa Marekani pamoja na kutoa makala kwenye vyombo vya habari kuelezea athari za vikwazo katika uchumi wa Zimbabwe. 

No comments:

Post a Comment

Note: Only a member of this blog may post a comment.