Thursday, May 6, 2021

KIKAO CHA MAKATIBU WAKUU WA SEKTA YA FEDHA NA UCHUMI WA EAC CHAFANYIKA ARUSHA

Kikao cha Makatibu Wakuu wanaoshughulikia masuala ya Fedha na Uchumi kutoka Nchi Wanachama wa Jumuiya ya Afrika Mashariki kimefanyika Arusha tarehe 6 Mei 2021.


Kikao hicho kimefanyika kwa lengo la kukamilisha agenda mbalimbali za msingi zitakazowasilishwa kwenye Mkutano wa 12 wa Baraza la Kisekta la Mawaziri wanaoshughulikia masuala ya Fedha na Uchumi pamoja na Mkutano wa Mawaziri wa Fedha wa Jumuiya ya Afrika Mashariki kuhusu Mashauriano ya Kibajeti unaotarajiwa kufanyika  tarehe 7 Mei 2021.


Miongoni mwa Agenda zitakazowasilishwa kwenye Mkutano wa 12 wa Baraza la Kisekta la Mawaziri wa Fedha na Uchumi ni  pamoja na Taarifa ya Utafiti wa Kuboresha Mfumo na Muundo wa Uendeshaji wa Jumuiya ya Afrika Mashariki kulingana na Rasilimali zilizopo pamoja na kupokea Taarifa ya Utekelezaji wa Maazimio mbalimbali yaliyofikiwa wakati wa Mkutano wa 11 wa Baraza hilo la Kisekta.

 

Ujumbe wa Tanzania kwenye Mkutano wa ngazi ya Makatibu Wakuu unaongozwa na Dkt. Juma Malik Akil, Katibu Mkuu, Ofisi ya Rais, Fedha na Mipango, Zanzibar na kuhudhuriwa pia na Bi. Amina KH. Shaaban, Naibu Katibu Mkuu kutoka Wizara ya Fedha na Mipango.


 Katibu Mkuu, Ofisi ya Rais,  Fedha na Mipango, Zanzibar, Mhe. Dkt. Juma Malik Akil akizungumza kama kiongozi wa ujumbe wa Tanzania wakati wa kikao cha Makatibu Wakuu wanaoshughulikia Sekta ya Fedha na Uchumi kutoka Nchi Wanachama wa Jumuiya ya Afrika Mashariki kilichofanyika jijini Arusha tarehe 6 Mei 2021 kwa ajili ya kuandaa Mkutano wa 12 wa Baraza la Kisekta la Mawaziri wa Fedha na Uchumi unaotarajiwa kufanyika jijini humo tarehe 7 Mei 2021. Kulia ni Naibu Katibu Mkuu, Wizara ya Fedha na Mipango, Bi. Amina KH. Shaaban.

Ujumbe wa Burundi ukiwa kwenye kikao cha Makatibu Wakuu wanaoandaa Mkutano wa 12 wa Baraza la Kisekta la Mawaziri wa Fedha na uchumi kutoka Jumuiya ya Afrika Mashariki

Ujumbe wa Uganda nao ukishiriki kikao cha Makatibu Wakuu

Ujumbe wa Sekretarieti ya Jumuiya ya Afrika Mashariki ukishiriki kikao cha Makatibu Wakuu

Sehemu nyingine ya ujumbe wa Tanzania ukiwa kwenye kikao cha Makatibu Wakuu. Kushoto ni Katibu Mkuu wa Wizara ya Kazi, Uchumi na Uwekezaji, Zanzibar, Bw. Mussa Haji Ali na Kamishna Msaidizi kutoka Wizara ya Fedha na Mipango, Bw. James Msina

Kamishna wa Uchambuzi wa Sera kutoka Wizara ya Fedha na Mipango, Bw. William Mhoja (kulia) akiwa na Kamishna wa Forodha kutoka Mamlaka ya Mapato Tanzania, Bw. Said Athumni wakati wa kikao cha Makatibu Wakuu wa Sekta ya Fedha na Uchumi wa Jumuiya ya Afrika Mashariki

Ujumbe wa Tanzania kwenye kikao cha Makatibu Wakuu

Kikao kikiendelea

Sehemu nyingine ya ujumbe wa Tanzania

Ujumbe wa Tanzania

Wajumbe wakifuatilia kikao

Kikao kikiendelea

No comments:

Post a Comment

Note: Only a member of this blog may post a comment.