Wednesday, May 5, 2021

RAIS SAMIA AHUTUBIA MABUNGE YA KENYA

Wabunge wa Mabunge Mawili ya Kenya (Bunge la Taifa pamoja na Bunge la Senate la Kenya) wakiwa tayari kumsikiliza Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mhe. Samia Suluhu Hassan aliyekwenda kuwahutubia wabunge hao Jijini Nairobi tarehe 05, Mei, 2021 wakati ya ziara yake rasmi nchini Kenya.

Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mhe. Samia Suluhu Hassan akihutubia Mabunge ya Kenya Jijini Nairobi tarehe 05, Mei, 2021 wakati ya ziara yake rasmi ya siku mbili nchini Kenya.

Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mhe. Samia Suluhu Hassan akihutubia Mabunge ya Kenya Jijini Nairobi tarehe 05, Mei, 2021

Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mhe. Samia Suluhu Hassan akihutubia Mabunge ya Kenya Jijini Nairobi tarehe 05, Mei, 2021

Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Mhe. Samia Suluhu Hassan amehutubia Mabunge Mawili ya Kenya (Bunge la Taifa pamoja na Bunge la Senate la Kenya) Jijini Nairobi tarehe 05, Mei, 2021.

Akiwahutubia wabunge hao wa Mabunge hayo ya Kenya Mhe. Rais Samia amewataka kuendeleza udugu wa kihistoria uliopo kati ya Tanzania na Kenya.

Amesema Tanzania na Kenya ni ndugu wa siku nyingi udugu ambaoo utaendelea kuwepo siku zote na ndio maana hata wanyama aina ya nyumbu huishi kwa kuhama kati ya Kenya na Tanzania kama mzunguko wa maisha yao

Mhe. Rais Samia alikuwa nchini Kenya kwa ziara rasmi ya kiserikali ya siku mbili kufuatia mwaliko wa mwenyeji wake Rais wa Jamhuri ya Kenya Mhe. Uhuru. Kenyatta.

Mhe. Rais na ujumbe wake wamerejea nchini joini ya tarehe 05/05/2021 baada ya kukamilika kwa ziara hiyo.

 

 

No comments:

Post a Comment

Note: Only a member of this blog may post a comment.