Wednesday, May 5, 2021

RAIS SAMIA SULUHU HASSAN ASHIRIKI DHIFA YA KITAIFA KATIKA IKULU YA NAIROBI

Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mhe. Samia Suluhu Hassan  katika picha na Rais wa Kenya Mhe. Uhuru Kenyatta pamoja na Mke wa Rais Kenyatta Mama Margaret Kenyatta kabla ya kwenda kwenye Dhifa ya Kitaifa aliyoandaliwa na Rais Kenyatta katika Ikulu ya Nairobi nchini Kenya tarehe 04 Mei, 2021.

Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mhe. Samia Suluhu Hassan katika picha ya Pamoja na Mke wa Rais Kenyatta Mama Margaret Kenyatta kabla ya kwenda kwenye Dhifa ya Kitaifa aliyoandaliwa na Rais Kenyatta katika Ikulu ya Nairobi nchini Kenya tarehe 04 Mei, 2021.

Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mhe. Samia Suluhu Hassan akiwa na Mwenyeji wake Rais wa Kenya Mhe. Uhuru Kenyatta wakielekea kwenye Dhifa ya Kitaifa aliyoandaliwa na Rais Kenyatta katika Ikulu ya Nairobi nchini Kenya tarehe 04 Mei, 2021.

Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mhe. Samia Suluhu Hassan akiwa amesimama na Mwenyeji wake Rais wa Kenya Mhe. Uhuru Kenyatta pamoja na Mke wa Rais Kenyatta Mama Margaret Kenyatta wakati wa nyimbo za Taifa zikipigwa katika Dhifa ya Kitaifa aliyoandaliwa na Rais Kenyatta katika Ikulu ya Nairobi nchini Kenya tarehe 04 Aprili, 2021.

Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mhe. Samia Suluhu Hassan akizungumza katika Dhifa hiyo ya Kitaifa iliyoandaliwa kwa heshima yake na mwenyeji wake Rais wa Kenya Mhe. Uhuru Kenyatta katika Ikulu ya Nairobi nchini Kenya tarehe 04 Mei, 2021.

Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mhe. Samia Suluhu Hassan akipokea zawadi ya Kitabu kutoka kwa Rais wa Kenya Mhe. Uhuru Kenyatta mara baada ya Dhifa ya Kitaifa iliyofanyika katika Ikulu ya Nairobi.

Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mhe. Samia Suluhu Hassan akiagana na Rais wa Kenya Mhe. Uhuru Kenyatta pamoja Mke wa Rais Kenyatta Mama Margaret Kenyatta mara baada ya Dhifa ya Kitaifa katika Ikulu ya Nairobi nchini Kenya tarehe 04 Mei 2021. picha na Ikulu


 

Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mhe. Samia Suluhu Hassan ameshiriki dhifa ya kitaifa iliyoandaliwa kwa heshima yake na mwenyeji wake Rais wa Jamhuri ya Kenya Mhe. Uhuru Kenyatta katika Ikulu ya Nairobi iliyofanyika jioni ya tarehe 04 Mei,2021.

Katika siku ya pili ya ziara yake tarehe 05/05/2021 Mhe. Rais akiwa na mwenyeji wake Rais Uhuru Kenyatta atahutubia Mabunge ya Kenya na baadaye atafungua Kongamano la wafanyabiashara wa Kenya na Tanzania linalofanyika jijini Nairobi.

Mhe. Rais Samia yuko nchini Kenya kwa ziara rasmi ya siku mbili kufuatia mwaliko wa mwenyeji wake Mhe. Rais Kenyata anatarajiwa kurejea nyumbani tarehe 05/05/2021




No comments:

Post a Comment

Note: Only a member of this blog may post a comment.