Friday, July 7, 2023

WATUMISHI WA WIZARA YA MAMBO YA NJE WASHIRIKI BONANZA LA MICHEZO


Timu ya mpira ya miguu ikiongozwa na nahodha wake Mkurugenzi wa Siasa, Ulinzi na Usalama katika Wizara ya Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki Balozi Stephen Mbundi wakiwa kwenye picha ya pamoja muda mfupi kabla ya kuwakabili wapinzania wao kwenye bonanza la michezo lililofanyika katika uwanja wa Dodoma Sekondari jijini Dodoma.

Watumishi wa Wizara ya Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki leo tarehe 7/7/2023 kwa shauku na morali ya hali juu wameshiriki bonanza la michezo lililofanyika kwenye uwanja wa Dodoma Sekondari jijini Dodoma.

Bonanza hilo ambalo limeandaliwa na Wizara limehusisha michezo mbalimbali kama vile mazoezi ya pamoja ya viungo, mpira wa miguu, mpira wa pete na riadha.

Bonanza hilo pamoja na masuala mengine lililenga kuhamasisha upimaji wa afya kwa watumishi wake hususani kwa Magonjwa Sugu Yasiyoabukiza (MSY), ikiwa ni miongoni mwa hatua mbalimbali zinazoendelea kuchukuliwa na Wizara katika utekelezaji wa Afua za VVU na MSY kwa mujibu wa Mwongozo wa Kudhibiti VVU, UKIMWI na Magonjwa Sugu Yasiyoambukiza wa mwaka 2014. 

Kwa upande wake Mkurugenzi wa Utawala na Usimamizi Rasilimali Watu katika Wizara ya Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki Bi. Chiku Kiguhe ameeleza kuridhishwa kwake na namna watumishi walivyohamasika kushiriki zoezi la upimaji afya na michezo ya pamoja. Vilevile, ametumia fursa hiyo kutoa wito kwa Watumishi wa Wizara kuendelea kujitokeza kwa wingi katika kushiriki michezo, kupima afya mara kwa mara na kuzingatia ushauri na miongozo inayotolewa na wataalam wa afya kuhusu masuala mbalimbali yanayolenga kuboresha afya zao. 

Watumishi wa Wizara waliojitokeza katika bonanza hilo kwa nyakati tofauti wameeleza furaha yao kuhusu namna Uongozi wa Wizara unavyozigatia na kujali suala la utimamu wa afya ya Watumishi wake, hususani kwa kuandaa programu mbalimbali za mara kwa mara ikiwemo michezo, elimu kuhusu masuala ya afya na upimaji. 
Wachezaji wa mpira wa miguu wakiwania mpira kwenye bonanza la michezo lililofanyika katika uwanja wa Dodoma Sekondari jijini Dodoma.
Wachezaji wa mpira wa pete wakiwania mpira 
kwenye bonanza la michezo lililofanyika katika uwanja wa Dodoma Sekondari jijini Dodoma.
Washiriki wa michezo wakiwa katika hali ya furaha kwenye ufunguzi wa Bonanza la michezo lililofanyika katika uwanja wa Dodoma Sekondari jijini Dodoma
Mkurugenzi wa Siasa, Ulinzi na Usalama katika Wizara ya Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki Balozi Stephen Mbundi akianzisha mpira kwneye bonanza la michezo lililofanyika katika uwanja wa Dodoma Sekondari jijini Dodoma
Washiriki wa michezo wakiwa katika hali ya furaha kwenye ufunguzi wa Bonanza la michezo lililofanyika katika uwanja wa Dodoma Sekondari jijini Dodoma
Mkurugenzi wa Utawala na Usimamizi Rasilimali Watu katika Wizara ya Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki Bi. Chiku Kiguhe akiwatoka wapinzani kwenye mpira wa pete katika bonanza la michezo lililofanyika katika uwanja wa Dodoma Sekondari jijini Dodoma.
Mchezo wa mpira wa miguu ukiendelea







No comments:

Post a Comment

Note: Only a member of this blog may post a comment.