Wednesday, July 26, 2023

MHE. MARIAM CHABI TALATA AREJEA BENIN

Makamu wa Rais wa Benin, Mheshimiwa Mariam Chabi Talata ameondoka nchini na kurejea Benin baada ya kumalizika kwa Mkutano wa Wakuu wa Nchi kuhusu Rasilimali Watu (Africa Human Capital Heads of State Summit) ulianza tarehe 25 na kumalizika tarehe 26 Julai 2023.

Katika Uwanja wa Ndege wa Kimataifa wa Julius Nyerere Dar es Salaam, Mhe. Mariam Chabi amesindikizwa na Waziri wa Maji, Mhe. Juma Aweso (Mb.), Mkuu wa Mkoa wa Dar es Salaam, Mhe. Albert Chalamila na viongozi mbalimbali waandamizi wa Serikali.

Makamu wa Rais wa Benin, Mheshimiwa Mariam Chabi Talata akiwasili katika Uwanja wa Ndege wa Kimataifa wa Julius Nyerere tayari kuondoka nchini Tanzania na kurejea Benin baada ya kumalizika kwa Mkutano wa Wakuu wa Nchi kuhusu Rasilimali Watu (Africa Human Capital Heads of State Summit) ulianza tarehe 25 na kumalizika tarehe 26 Julai 2023


Makamu wa Rais wa Benin, Mheshimiwa Mariam Chabi Talata akizungumza na Waziri wa Maji Mhe. Juma Aweso, Mkuu wa Mkoa wa Dar es Salaam, Mhe. Albert Chalamila kabla ya kuondoka nchini na kurejea Benin baada ya kumalizika kwa Mkutano wa Wakuu wa Nchi kuhusu Rasilimali Watu (Africa Human Capital Heads of State Summit) ulianza tarehe 25 na kumalizika tarehe 26 Julai 2023










No comments:

Post a Comment

Note: Only a member of this blog may post a comment.