Wednesday, July 5, 2023

BALOZI KAYOLA AWASILISHA HATI ZA UTAMBULISHO KWA RAIS WA MALAWI

Balozi wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania nchini Malawi, Mheshimiwa Agnes Kayola amewasilisha Hati za Utambulisho kwa Rais wa Jamhuri ya Malawi, Mheshimiwa Lazarus Chakwera, tarehe 04 Julai 2023 Ikulu, Jijini Lilongwe Malawi.

Julai 1, 2023 Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Mheshimiwa Dkt. Samia Suluhu alimteua Balozi Kayola kuwa Balozi wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania nchini Malawi. 

Rais wa Jamhuri ya Malawi, Mheshimiwa Lazarus Chakwera akipokea Hati za Utambulisho kutoka kwa Balozi wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania nchini Malawi, Mheshimiwa Agnes Kayola tarehe 04 Julai 2023 Ikulu, Jijini Lilongwe Malawi

Rais wa Jamhuri ya Malawi, Mheshimiwa Lazarus Chakwera akimpongeza Balozi wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania nchini Malawi, Mheshimiwa Agnes Kayola mara baada ya kuwasilisha Hati za Utambulisho, Ikulu Jijini Lilongwe

Picha ya Pamoja



No comments:

Post a Comment

Note: Only a member of this blog may post a comment.