Thursday, July 20, 2023

DKT. TAX AONGOZA UJUMBE WA TANZANIA MKUTANO WA 25 WA KAMATI YA MAWAZIRI WA ASASI YA SADC YA SIASA, ULINZI NA USALAMA

Waziri wa Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki, Mhe. Dkt. Stergomena Tax ameongoza ujumbe wa Tanzania katika Mkutano wa 25 wa Kawaida wa Kamati ya Mawaziri wa Asasi ya Ushirikiano katika masuala ya Siasa, Ulinzi na Usalama wa Jumuiya ya Maendeleo Kusini mwa Afrika (MCO) unaofanyika jijini Windhoek, Namibia tarehe 20 na 21 Julai, 2023.

 

Mkutano huo ambao ulitanguliwa na Mkutano wa Kamati ya Kudumu ya Makatibu Wakuu wa Asasi ya Siasa, Ulinzi na Usalama ya SADC uliofanyika kuanzia tarehe 17 hadi 19 Julai 2023, pamoja na mambo mengine umepokea na kujadili agenda mbalimbali zilizowasilishwa ikiwemo Mapitio ya Utekelezaji wa Maamuzi ya Mkutano wa 24 wa MCO na Wakuu wa Nchi na Serikali wa SADC; Hali ya Siasa, Ulinzi na Usalama ya Kanda; na Uimarishaji wa Demokrasia katika Kanda.

 

Akizungumza wakati wa ufunguzi wa Mkutano huo, Mwenyekiti wa Kamati hiyo ambaye pia ni Naibu Waziri Mkuu na Waziri wa Mambo ya Nje wa Namibia, Mhe. Dkt. Netumbo Nandi-Ndaitwah amezipongeza nchi wanachama kwa ushirikiano katika kuendelea kuimarisha amani, usalama na utulivu katika Kanda ambavyo amevitaja kama msingi  wa maendeleo endelevu.

 

Amesema kuwa kwa ujumla hali ya usalama katika kanda inaridhisha na kwamba Jumuiya ya SADC itaendelea na jitihada mbalimbali katika kuhakikisha amani ya kudumu inapatikana katika maeneo yenye changamoto za usalama ikiwemo eneo la mashariki mwa Jamhuri ya Kidemokrasia ya Congo (DRC) na lile la Kaskazini mwa Jimbo la Cabo Delgado nchini Msumbiji.

 

Ameongeza kusema nchi wanachama zinaendelea kuunga mkono jitihada mbalimbali zinazofanyika katika kutafuta suluhu ya kudumu kwa ya hali ya usalama mashariki mwa Congo ili hatimaye eneo hilo lifikie hali ya utulivu na amani ya kudumu.

 

Akizungumzia hali ya usalama Kaskazini mwa Jimbo la Cabo Delgado la nchini Msumbiji, Mhe. Nandi-Ndaitwah amesema hali kwa kiasi kikubwa ni shwari na vitendo vya ugaidi vimedhibitiwa huku maisha ya wananchi hususan wale waliokimbia makazi yao yakirejea katika hali ya kawaida.

 

Kadhalika ametoa wito kwa nchi wanachama kuendelea na jitihada za pamoja katika kukabiliana na biashara haramu ya usafirishaji binadamu kwa kuimarisha masuala ya sheria, kuwajengea uwezo wataalam  na kuendelea kutoa elimu kwa wananchi kuhusu suala hili.

 

Kadhalika ametoa rai nchi wanachama ambazo hazijasaini au kuridhia Itifaki ya Uhuru wa raia wa Kanda ya SADC kutembea kwenye nchi za Jumuiya hiyo ya mwaka 2005 kufanya hivyo ili kuwawezesha wananchi kunufaika kikamilifu na  agenda ya Mtangamano wa SADC.

 

 “Nazihamasisha nchi ambazo hazijasaini au kuridhia Itifaki ya Uhuru wa Raia katika Kanda Kutembea ya mwaka 2005 kufanya hivyo. Itifaki hii ikianza kutekelezwa itaimarisha utalii miongoni mwetu na kuwawezesha raia kufanya biashara na uwekezaji katika kanda kwa uhuru zaidi, alisisitiza Mhe. Nandi-Ndaitwah.

 

Awali akizungumza, Katibu Mtendaji wa SADC, Bw. Elias Mpedi Magosi amesema kuwa Sekretarieti ya SADC itaendelea kushirikiana na Nchi Wanachama hususan katika kukabiliana na changamoto mbalimbali zilizopo katika kanda zikiwemo za kiusalama, kijamii na kiuchumi ili hatimaye kuwa na Kanda tulivu kwa ajili ya maendeleo endelevu.

 

Pia alimpongeza Mwenyekiti wa Kamati ya Mawaziri anayemaliza muda wake Mhe. Nandi-Ndaitwa kwa kazi nzuri aliyofanya katika kipindi chote na kumkaribisha na kumwahidi ushirikiano Mwenyekiti mpya ambaye ni Waziri wa Mambo ya Nje wa Zambia.

 

Pia alitumia fursa hiyo kumtambulisha kwa Mawaziri Mkurugenzi mpya wa Asasi ya Siasa, Ulinzi na Usalama ya SADC, Prof. Kula Ishmael Theletsane kutoka Afrika Kusini.

 

Mbali na Mhe. Dkt. Tax, Ujumbe wa Tanzania ulimjumuisha pia Waziri wa Ulinzi na Jeshi la Kujenga Taifa, Mhe. Innocent Bashungwa, Mwakilishi wa Mkuu wa Majeshi ya Ulinzi na Mnadhimu Mkuu wa Jeshi, Lt. Jenerali Salum Othman, Katibu Mkuu wa Wizara ya Ulinzi na Jeshi la Kujenga Taifa, Dkt. Faraji Mnyepe, Katibu Mkuu wa Wizara ya Mambo ya Ndani ya Nchi, Mhe. Kaspar Mmuya, Naibu katibu Mkuu wa Wizara ya Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki, Balozi Fatma Mohammed Rajab na Balozi wa Tanzania nchini Namibia, Mhe. Dkt. Modestus Kipilimba.

Mwenyekiti wa Kamati ya Mawaziri wa Asasi ya Siasa, Ulinzi na Usalama ya Jumuiya ya Maendeleo Kusini mwa Afrika ambaye pia ni Naibu Waziri Mkuu na Waziri wa Mambo ya Nje wa Namibia, Mhe. Dkt. Netumbo Nandi-Ndaitwah akifungua rasmi Mkutano wa Kamati hiyo unaofanyika jijini Windhoek, Namibia tarehe 20 na 21 Julai 2023
 

Mhe. Nandi-Ndaitwah akiwa na wajumbe wa meza kuu wakati wa ufunguzi rasmi wa Mkutano wa Kawaida wa 25 wa Kamati Mawaziri wa Asasi ya Ushirikiano katika masuala ya Siasa, Ulinzi na Usalama wa Jumuiya ya Maendeleo Kusini mwa Afrika (MCO) unaofanyika jijini Windhoek, Namibia tarehe 20 na 21 Julai 2023
Waziri wa Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki, Mhe. Dkt. Stergomena Tax akiongoza ujumbe wa Tanzania kwenye Mkutano wa Kawaida wa 25 wa Kamati Mawaziri wa Asasi ya Ushirikiano katika masuala ya Siasa, Ulinzi na Usalama wa Jumuiya ya Maendeleo Kusini mwa Afrika (MCO) unaofanyika jijini Windhoek, Namibia tarehe 20 na 21 Julai 2023. 
Katibu Mtendaji wa Sekretarieti ya Jumuiya ya Maendeleo Kusini mwa Afrika, Mhe. Elias Mpedi Magosi akizungumza wakati wa ufunguzi rasmi wa Mkutano wa Kawaida wa 25 wa Kamati Mawaziri wa Asasi ya Ushirikiano katika masuala ya Siasa, Ulinzi na Usalama wa Jumuiya ya Maendeleo Kusini mwa Afrika (MCO) unaofanyika jijini Windhoek, Namibia tarehe 20 na 21 Julai 2023
Mhe. Dkt. Tax akishiriki taratibu za ufunguzi rasmi wa Mkutano wa Kawaida wa 25 wa Kamati Mawaziri wa Asasi ya Ushirikiano katika masuala ya Siasa, Ulinzi na Usalama wa Jumuiya ya Maendeleo Kusini mwa Afrika (MCO) unaofanyika jijini Windhoek, Namibia tarehe 20 na 21 Julai 2023. Wengine katika picha ni Waziri wa Ulinzi na Jeshi la Kujenga Taifa, mhe. Innocent Bashungwa (kushoto), Katibu Mkuu wa Wizara ya Ulinzi na Jeshi la Kujenga Taifa, Dkt. Faraji Mnyepe na Naibu Katibu Mkuu wa Wizara ya Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki, Balozi Fatma Mohammed Rajab.
Ufunguzi ukiendelea
Mhe. Bashungwa akiteta jambo na Katibu Mkuu wa Wizara yake, Dkt. Mnyepe. Kulia ni Balozi Fatma
Mkutano ukiendelea
Mkutano ukiendelea
Sehemu ya Sekretarieti ya SADC wakati wa mkutano
Mnadhimu Mkuu wa Jeshi, Lt. Jenerali Salum Othma akibadilisha mawazo na mmoja wa wajumbe wanaoshiriki Mkutano wa  Kamati ya Mawaziri wa Asasi ya Ushirikiano katika masuala ya Siasa, Ulinzi na Usalama wa Jumuiya ya Maendeleo Kusini mwa Afrika (MCO), unaofanyika nchini Namibia  kuaniza tarehe 20 hadi 21 Julai 2023
Sehemu ya ujumbe wa Tanzania wakifuatilia hafla ya ufunguzi wa Mkutano wa Kawaida wa 25 wa Kamati Mawaziri wa Asasi ya Ushirikiano katika masuala ya Siasa, Ulinzi na Usalama wa Jumuiya ya Maendeleo Kusini mwa Afrika (MCO) unaofanyika jijini Windhoek, Namibia tarehe 20 na 21 Julai 2023
Sehemu nyingine ya ujumbe wa Tanzania wakati wa Mkutano
Kikundi cha Utamaduni kutoka Windhoek kikitoa burudani kwa Mawaziri wakati wa ufunguzi wa Mkutano wa Kawaida wa 25 wa Kamati Mawaziri wa Asasi ya Ushirikiano katika masuala ya Siasa, Ulinzi na Usalama wa Jumuiya ya Maendeleo Kusini mwa Afrika (MCO) unaofanyika jijini Windhoek, Namibia tarehe 20 na 21 Julai 2023
Picha ya pamoaja
Mhe. Dkt. Tax akizungumza  na Naibu Waziri Mkuu na Waziri wa Mambo ya Nje wa Namibia ambaye pia ni Mwenyekiti wa Kamati ya Mawaziri wa Asasi ya Ushirikiano katika masuala ya Siasa, Ulinzi na Usalama wa Jumuiya ya Maendeleo Kusini mwa Afrika (MCO), Mhe. Dkt. Netumbo Nandi-Ndaitwah kabla ya kuanza kwa Mkutano wa Kamati hiyo
Mhe. Dkt. Tax akizungumza  na  Waziri wa Mambo ya Nje wa Afrika Kusini, Mhe. Dkt. Naledi Pandor  walipokutana jijini Windhoek Namibia wakati wa Mkutano wa  Kamati ya Mawaziri wa Asasi ya Ushirikiano katika masuala ya Siasa, Ulinzi na Usalama wa Jumuiya ya Maendeleo Kusini mwa Afrika (MCO), unaofanyika nchini Namibia  kuaniza tarehe 20 hadi 21 Julai 2023
Mhe. Dkt. Tax akizungumza  na Waziri wa Mambo ya Nje wa Jamhuri ya Kidemokrasia ya Congo (DRC) walipokutana jijini Windhoek Namibia wakati wa Mkutano wa  Kamati ya Mawaziri wa Asasi ya Ushirikiano katika masuala ya Siasa, Ulinzi na Usalama wa Jumuiya ya Maendeleo Kusini mwa Afrika (MCO), unaofanyika nchini Namibia  kuaniza tarehe 20 hadi 21 Julai 2023
Mhe. Dkt. Tax akizungumza  na Waziri wa Ulinzi na Jeshi la Kujenga Taifa, Mhe. Innocent Bashungwa, kabla ya kushiriki Mkutano wa  Kamati ya Mawaziri wa Asasi ya Ushirikiano katika masuala ya Siasa, Ulinzi na Usalama wa Jumuiya ya Maendeleo Kusini mwa Afrika (MCO), unaofanyika nchini Namibia  kuaniza tarehe 20 hadi 21 Julai 2023
Mhe. Dkt. Tax akisalimiana  na  Katibu Mtendaji wa SADC, Mhe. Elias Mpedi Magosi walipokutana jijini Windhoek, Namibia wakati wa Mkutano wa  Kamati ya Mawaziri wa Asasi ya Ushirikiano katika masuala ya Siasa, Ulinzi na Usalama wa Jumuiya ya Maendeleo Kusini mwa Afrika (MCO), unaofanyika nchini Namibia  kuaniza tarehe 20 hadi 21 Julai 2023


Dkt. Mnyepe akizungumza na Katibu Mkuu wa Wizara ya Mambo ya Ndani ya Nchi, Mhe. Kaspar Mmuya kabla ya kuanza kwa Mkutano wa  Kamati ya Mawaziri wa Asasi ya Ushirikiano katika masuala ya Siasa, Ulinzi na Usalama wa Jumuiya ya Maendeleo Kusini mwa Afrika (MCO), unaofanyika nchini Namibia  kuaniza tarehe 20 hadi 21 Julai 2023
Mhe. Dkt. Tax akipokelewa na Naibu Katibu Mkuu wa Wizara ya Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki, Balozi Fatma Mohammed Rajab mara baada ya kuwasili katika ukumbi wa mikutano kwa ajili ya kushiriki Mkutano wa  Kamati ya Mawaziri wa Asasi ya Ushirikiano katika masuala ya Siasa, Ulinzi na Usalama wa Jumuiya ya Maendeleo Kusini mwa Afrika (MCO), unaofanyika nchini Namibia  kuaniza tarehe 20 hadi 21 Julai 2023
































 

No comments:

Post a Comment

Note: Only a member of this blog may post a comment.