Sunday, February 26, 2017

Rais Magufuli awaapisha mabalozi wanne

Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mhe. Dkt. John Pombe Magufuli akimuapisha Balozi wa Tanzania nchini Kenya, Mhe. Pindi Hazara Chana. Hafla za uapisho zimeanyika leo jijini Dar es Salaam
Mhe. Magufuli akimkabidhi vitendea kazi Balozi Chana
Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mhe. Dkt. John Pombe Magufuli akimuapisha Balozi wa Tanzania nchini Khartoum, Sudan Mhe. Silima Kombo Haji. Hafla za uapisho zimeanyika leo jijini Dar es Salaam
Mhe. Magufuli akimkabidhi vitendea kazi Balozi Silima
Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mhe. Dkt. John Pombe Magufuli akimuapisha Balozi wa Tanzania nchini Mascut, Oman Mhe. Abdallha Abas Kilima. Hafla za uapisho zimeanyika leo jijini Dar es Salaam

Mhe. Magufuli akimkabidhi vitendea kazi Balozi Kilima
Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mhe. Dkt. John Pombe Magufuli akimuapisha Balozi wa Tanzania nchini Seoul, Korea Kusini, Mhe. Matilda Swila Masuka. Hafla za uapisho zimeanyika leo jijini Dar es Salaam
Mhe. Magufuli akimkabidhi vitendea kazi Balozi Masuka
Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mhe. Dkt. John Pombe Magufuli (wa nne kutoka kushoto), Makamu wa Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mhe. Samia Hassani Suluhu (wa tatu kutoka kushoto), Waziri Mkuu wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mhe. Majaliwa Kasim Majaliwa (wa nne kutoka kulia), Katibu Mkuu Kiongozi Mhe Eng. John   Herbert Kijazi (wa pili kutoka kushoto), Katibu Mkuu wa Wizara ya Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki Dkt. Azizi Mlima (wa tatu kutoka kulia), wakiwa katika picha ya pamoja na Mabalozi wateule mara baada ya kuapishwa, Ikulu jijini Dar es Salaam.
TAARIFA KWA VYOMBO VYA HABARI 
Mabalozi wapya wanne waapishwa na kupangiwa vituo
Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mhe. Dkt. John Pombe Joseph Magufuli amewapangia vituo na kuwaapisha Mabalozi wapya wanne ambao uteuzi wao ulifanyika    tarehe 03 Desemba 2016. 

Mabalozi hao ambao waliapishwa leo na Mhe. Rais Ikulu jijini Dar Es Salaam ni Balozi wa Tanzania nchini Kenya, Mhe. Dkt. Pindi Chana ambaye anajaza nafasi iliyoachwa wazi na Mhe. John Haule. Mhe. Haule ambaye aliwahi kuwa Katibu Mkuu wa  iliyokuwa Wizara ya Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Kimataifa alistaafu kwa mujibu wa sheria mwaka 2016.

Mhe. Chana kabla ya kuteuliwa kuwa Balozi aliwahi kushika nyadhifa mbalimbali ikiwemo Ubunge wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania na Unaibu Waziri wa Maendeleo ya Jamii, Jinsia na Watoto katika Serikali ya awamu ya nne.

Balozi mwingine aliyeapishwa ni Mhe. Silima Kombo Haji anayekwenda kuwa Balozi wa kwanza wa Tanzania nchini Jamhuri ya Sudan baada ya Mhe. Rais kuamua kuufungua upya Ubalozi huo ambao ulifungwa miaka ya nyuma kutokana na sababu za kiuchumi. Kabla ya uteuzi huo Balozi Silima alikuwa Mkurugenzi wa Idara ya Mambo ya Nje Zanzibar katika Wizara ya Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki.

Walioapishwa pia ni Mhe. Abdallah Kilima ambaye anakwenda nchini Oman kujaza nafasi iliyoachwa wazi na Mhe. Ali Saleh aliyestaafu kwa mujibu wa sheria. Balozi Kilima kabla ya kuteuliwa kushika wadhifa huo alikuwa Mkurugenzi wa Idara ya Mashariki ya Kati katika Wizara ya Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki.

Balozi wa kwanza wa Tanzania nchini Jamhuri ya Korea, Mhe. Matilda Masuka naye aliapishwa na Mhe. Rais leo. Balozi Masuka kabla ya kukabidhiwa majukumu hayo mapya alikuwa Mkuu wa Utawala katika Ubalozi wa Tanzania nchini China.   Jamhuri ya Korea ni moja kati ya nchi sita ambazo Mhe. Rais Magufuli amefungua Balozi mpya. Nchi nyingine ni Algeria, Jamhuri ya Sudan, Uturuki, Israel na Qatar.

  Imetolewa na:

Kitengo cha Mawasiliano ya Serikali,

Wizara ya Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki

Dar es Salaam, 26 Februari, 2017.




Saturday, February 25, 2017

Tanzania yaahidi kuimarisha Diplomasia ya Uchumi na Uganda

Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Mhe. Dkt. John Pombe Magufuli akihutubia kwenye mkutano na waandishi wa habari uliofanyika Ikulu, Dar es Salaam wakati wa ziara ya Rais wa Uganda hapa nchini, Mhe. Yoweri Museveni (anayeonekana ameketi kulia). Katika hotuba yake Rais Magufuli aliahidi kuimarisha urafiki na undugu uliodumu kwa miaka mingi baina ya mataifa hayo mawili.
Mhe. Rais Museveni nae akihutubia katika mkutano na waandishi wa habari wakati wa ziara yake nchini.
 Pamoja na kuzungumzia masuala ya ushirikiano wa kidiplomasia, Rais Museveni aliishukuru Serikali ya Jamhuri ya Muungano wa Tanzania kwa kuikomboa  Uganda dhidi ya adui Nduli Idd Amin Dada na ukombozi wa kiuchumi kwa kujenga reli ya kati " standard gauge" ambayo itaenda sambamba na ujenzi wa bandari kavu "Dry Port" Jijini Mwanza ili kurahisisha usafirishaji wa mizigo ya Uganda kutoka Bandari ya Dar es Salaam. 
Sehemu ya Mawaziri na Maafisa Waandamizi wa Serikali ya Tanzania waliohudhuria mkutano huo ambao ulitanguliwa na hafla ya utiaji saini wa mkataba wa ushirikiano katika masuala ya Siasa na Diplomasia. 
Waziri wa Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki, Balozi Dkt. Augustine Mahiga (kulia) pamoja na Waziri wa Nchi Ofisi ya Rais anayeshughulikia masuala ya Kimataifa wa Uganda, Mhe. Okello Oryem wakisaini Mkataba wa Ushirikiano katika masuala ya Siasa na Diplomasia.
Wakibadilishana mkataba mara baada ya kuusaini.
Marais wakipongezana mara baada ya kutoa hotuba.

Rais Museveni awasili nchini kwa ziara ya kitaifa ya siku mbili


Rais wa  Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Mhe. John Pombe Joseph Magufuli akimkaribisha nchini Rais wa Uganda, Mhe. Yoweri Kaguta Museveni alipowasili kwenye Uwanja wa Ndege wa Kimataifa cha Julius Nyerere tayari kwa kuanza ziara ya siku mbili hapa. Katika ziara hiyo Mhe. Museveni anatarajiwa kufanya mzungumzona mwenyeji wake Magufuli pamoja na kutembelea Kiwanda cha Azam.
Makamu wa Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mhe. Samia Suluhu Hassan (kushoto) akiwa  na Waziri Mkuu wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Mhe.  Kassim Majaliwa (katikati) pamoja na Waziri wa Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki, Dkt. Augustine Mahiga (Mb.) wakati wa mapokezi ya Rais wa Uganda, Mhe. Yoweri Museveni
Rais Museveni pamoja na mwenyeji wake Rais Dkt. Magufuli wakisikiliza nyimbo za mataifa yao
Makamu wa Rais akiwa uwanja wa ndege na Viongozi mbalimbali wa ngazi za juu Serikalini wakati wa mapokezi ya Rais Museveni.
Rais Museveni pamoja na Rais Magufuli wakitizama moja ya kikundi cha ngoma kilichokuwa kikitoa burudani uwanjani hapo.
Rais Yoweri Kaguta Museveni pamoja na Rais Dkt. John Pombe Magufuli wakizungumza jambo.
===================================================
 TAARIFA KWA VYOMBO VYA HABARI
 


Tanzania na Uganda sio nchi rafiki tu bali ni ndugu wa kweli lakini Kiwango cha biashara kati ya nchi hizo hakitafsri ipasavyo ukubwa wa udugu na urafiki uliopo kati ya yao. 

Hayo yalibainishwa leo na Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Mhe. Dkt. John Pombe Joseph Magufuli Ikulu jijini Dar es Salaam akiwa na Mgeni wake Rais wa Uganda, Mhe. Yoweri Kaguta Museveni. 

Rais Museveni yupo nchini Tanzania kwa ziara ya Kiserikali ya Siku mbili kuanzia tarehe 25 hadi 26 Februari 2017.

“Tanzania iliuza bidhaa zenye thamani ya Shilingi bilioni 126.744 mwaka 2016 ikilinganishwa na bidhaa zenye thamani ya Shilingi bilioni 99.882 zilizouzwa mwaka 2015”. “Hiki ni kiwango kidogo sana ukilinganisha na udugu mkubwa tulionao kati ya nchi zetu mbili”alisema Dkt. Magufuli.

Rais Magufuli alieleza kuwa ili kukuza kiwango cha biashara kati ya nchi hizo mbili, Serikali yake imeanza mkakati wa kuboresha miundombinu ya usafirishaji ikiwemo ujenzi wa reli ya kiwango cha kimataifa kutoka Dar es Salaam-Mwanza-Isaka hadi Burundi na Rwanda. Rais Magufuli alisema pia kuwa Serikali itajenga Bandari Kavu jijini Mwanza ili kuwarahisishia wafanyabiashara wa Uganda kuchukulia bidhaa zao Mwanza badala ya kusafiri hadi Dar es Salaam. 

Sanjari na hayo Serikali itaboresha bandari ya Bell na itapunguza vizuizi vya barabarani na kubaki vitatu ili kupunguza muda mwingi unaopotezwa na malori ya mizigo kwenye vizuizi hivyo.

Kuhusu ujenzi wa bomba la kusafirisha mafuta kutoka Hoima hadi Bandari ya Tanga, Rais Magufuli alisema Serikali yake ilishafanyia kazi vikwazo vyote saba vilivyowasilishwa ikiwemo kodi ya ongezeko la thamani (VAT) na kutoa mwito kwa mwekezaji kuanza ujenzi wa bomba hilo haraka kwani hakuna kisingizio kingine. Rais Magufuli alisisitiza umuhimu wa kupanga tarehe ya uwekaji wa jiwe la msingi wa ujenzi wa bomba hilo  na kwamba yupo tayari kusafiri kwenda nchini Uganda kama itakubalika jiwe hilo kuwekwa nchini humo. 

Aidha, Rais Magufuli alizungumzia jitihada za Serikali yake kufufua Shirika la Ndege la ATCL kwa kununua ndege sita kwa lengo la kuimarisha usafiri wa anga nchini na nchi jirani. Alimuomba Rais Museveni muda utakapofika ndege hizo ziweze kwenda Uganda jambo ambalo liliafikiwa.

Akizungumzia Mkataba wa Ubia wa Kiuchumi baina ya nchi za Jumuiya ya Afrika Mashariki na nchi za Umoja wa Ulaya (EPA), Rais Magufuli aliuona mkataba huo kama kikwazo katika juhudi za Serikali za kuifanya Tanzania kuwa nchi ya viwanda ifikapo mwaka 2020. Hivyo alimuomba Rais Museveni kumuunga mkono kuepuka mkataba huo kwa manufaa ya wananchi wa EAC.

“Rais Museveni alibebwa na Tanzania wakati wa utawala wa Baba wa Taifa, Mwalimu Julius Nyerere, hivyo namuomba Rais Museveni naye anibebe katika suala hili la EPA kwa manufaa ya wananchi wa nchi zetu na Jumuiya yetu” alisisitiza Rais Magufuli. 

Kwa upande wake, Rais Museveni alibainisha kuwa, hadi leo tatizo kubwa kwa Bara la Afrika lililopelekea hadi kutawaliwa na wakoloni huko nyuma ni ukosefu wa umoja na msimamo wa pamoja.  Alisema amekuja Tanzania kujadiliana na Rais Magufuli ili kupata msimamo wa pamoja kuhusu Mkataba wa EPA wenye manufaa kwa wananchi kwani undugu na umoja  uliopo kati ya nchi hizi mbili ni zaidi ya mkataba huo.

Kuhusu mpango wa Tanzania kujenga reli ya kiwango cha kimataifa, Rais Museveni aliupongeza mpango huu na kuutaja kama mchango wa pili wa Tanzania katika ukombozi wa Uganda. Alisema reli hiyo itakuwa msaada mkubwa kwa uchumi wa Uganda kwa kuwa utakuwa ni usafiri wa haraka na gharama nafuu.

Rais Museveni kabla ya kuondoka nchini kesho tarehe 26 Februari 2017 atatembelea kiwanda cha AZAM kilichopo Vingunguti jijini Dar es Salaam. AZAM pia imefanya uwekezaji nchini Uganda.  


Imetolewa na:
Kitengo cha Mawasiliano ya Serikali,
Wizara ya Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki, 
Dar es Salaam, 25 Februari, 2017




Friday, February 24, 2017

Waziri Mahiga afungua Mkutano wa Mawaziri wa SADC-ISPDC

Waziri wa Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki, Dkt. Augustine Mahiga akizungumza wakati wa ufunguzi wa Mkutano wa Kamati Ndogo ya Mawaziri wa Siasa na Diplomasia wa Jumuiya ya Maendeleo Kusini mwa Afrika (SADC). Mkutano huo umefanyika kwenye Kituo cha Kimataifa cha Mikutano cha Julius Nyerere Jijini Dar es Salaam
Naibu Waziri wa Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki, Dkt. Susan Kolimba ( kulia) akifuatilia  ufunguzi wa mkutano huo pamoja na washiriki wengine.
Waziri wa Mambo ya Nje wa Msumbiji akifuatilia ufunguzi wa mkutao huo
Baadhi ya Wakurugenzi kutoka Wizara ya Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki nao wakimsikiliza Waziri Mahiga alipokuwa akizungumza katika ufunguzi wa mkutano huo., Kushoto ni Mkurugenzi wa Kitengo cha Sheria, Balozi Baraka Luvanda akifuatiwa na Mkurugenzi wa Idara ya Mashariki ya Kati, Balozi Abdallah Kilima
Katibu  Mtendaji wa SADC, Dkt. Stregomena Tax naye akizungumza wakati wa Mkutano huo.
Mkurugenzi wa Idara ya Ushirikiano wa Kikanda, Balozi Innocent Shiyo akitoa ratiba ya mkutano kwa wajumbe
Sehemu ya wajumbe kutoka Zimbabwe wakiwa  na Balozi wao anayeiwakilisha Zimbabwe hapa nchini Mhe. Edzai Chimonyo (katikati)
Sehemu ya Watumishi wa Mambo ya Nje wakifuatilia  ufunguzi wa mkutano huo
Mkutano ukiendelea
===========================================================================================


OPENING REMARKS BY HON. DR. AUGUSTINE P. MAHIGA (MP) MINISTER FOR FOREIGN AFFAIRS AND EAST AFRICAN COOPERATION OF THE UNITED REPUBLIC OF TANZANIA
AND THE CHAIRPERSON OF INTER-STATE POLITICS AND
DIPLOMACY COMMITTEE, (ISPDC) MEETING HELD ON
24THFEBRUARY, 2017 DAR ES SALAAM, TANZANIA



Honorable Ministers,
Distinguished Delegates,
Ladies and Gentlemen,
Good Morning.
It is a great honor and privilege for me to host this important Statutory Meeting of the Inter-State Politics and Diplomacy Committee (ISPDC) of the Organ on Politics, Defence and Security Cooperation. As was indicated by the Executive Secretary, a gathering of this nature draws its mandate from Article 6 (5) of the Protocol on Politics, Defence and Security Cooperation, which makes provision for the Chairperson of the ISPDC to convene at least one meeting of the committee per year.  I wish to welcome you brothers and sisters to the United Republic of Tanzania, a country where hospitality is our tradition.

Distinguished Delegates,
It is my first time to host this meeting since Tanzania assumed the Chair of the SADC Organ on Politics, Defense and Security Cooperation in August, 2016. As our role entails, we are here to discuss, deliberate on and come up with fruitful decisions on the political, peace and security situation in the region.

I wish to acknowledge and commend efforts made by member states to ensure that there is peace, security and stability particularly in our fellow Member States of the Kingdom of Lesotho and the Democratic Republic of Congo.
Since the last meeting, there have been a number of political developments within these two Member States and the Organ and MCO have initiated several interventions. In the Kingdom of Lesotho, the Oversight Committee (OC) continues with its work on the ground, I am glad to announce that on 12th February 2017, the SADC Facilitator and members of the Oversight Committee welcomed the leaders of opposition parties who had been in exile in South Africa. Thus, in line with the decisions of the SADC Summit, it is expected that the return of the exiled leaders will contribute to the national reconciliation of the Basotho nation as it prepares to undertake fundamental structural reforms aimed at normalizing the political and security challenges affecting the country since August 2014.

Honorable Ministers,
As for DRC, a direct Ministerial Assessment Mission has continued to maintain a presence there and provides continued support to the Member State. Recently, a technical assessment team comprising of officers from the Secretariat and the United Republic of Tanzania was deployed to the DRC from 13 to 17 February, 2017, to further assess the situation on the ground.
In light of the above, this meeting will give us an opportunity to interrogate these and other matters that continue to affect our Region. It will also give us an opportunity to review relevant policy documents that will enable us to execute this noble mandate in response to increasing contemporary complexities.

Distinguished Delegates,
May I reiterate the importance of our duty to promote and protect democracy, which is a vehicle for unity and economic development in the SADC region. Let us recall that it is only through peaceful co-existence and stability that we can achieve all the goals of the community.

As the chair I am aware that, among other issues, during this meeting we will have an opportunity to set an agreed date on the commemoration of the Southern Africa Liberation day. A day that will signify the liberation struggles of the frontline states which led to the formation of the SADCC organization in 1980.  The celebrations will also uphold and support the founding principles of the SADC Treaty and Protocol on Politics, Defense and Security cooperation which is the guiding book of the organ.

Distinguished Delegates,
As you may all agree, SADC is one of the strongest and longest surviving regional groups in Sub- Saharan Africa. Not only that but it also has strong bonds that tie its members together. This has been highlighted by the requests from other states; the Union of Comoros in 2015 and from the Republic of Burundi in 2016 to join the organization. This meeting has been tasked to assess the eligibility of both states to join SADC.

Together, let us see if both states meet the set criteria for membership of SADC and advise our Heads of States accordingly.

Distinguished Delegates,
With these few remarks and tasks ahead of us, I wish to declare this meeting officially opened.


‘Asanteni sana’
‘Karibuni Tanzania’