Sunday, March 24, 2013

China’s President makes historical visit to Tanzania






China’s President makes historical visit to

 Tanzania


By TAGIE DAISY MWAKAWAGO

As the climax of the Golden Jubilee celebration of the relations between Tanzania and China nears, President Xi Jinping of the People’s Republic of China later today is expected to make his first State Visit in Tanzania, since he assumed his Presidency earlier this month. 

The visit is forecasted to further cement historical foundation of nearly fifty years' friendship that had existed between the two countries since the era of the Late Founders of both countries, the Late Mwalimu Julius Kambarage Nyerere of then Tanganyika and the Late Mao Zedong of China. 

President Jakaya Mrisho Kikwete, President of the United Republic of Tanzania is expected to receive his counterpart President of China at the Mwalimu Julius Nyerere International Airport in Dar es Salaam today, whereby official talks will follow later in the evening at the State House. 

President Xi Jinping formerly assumed his Presidency on March 13, 2013 by China’s National Legislature, giving him the three titles held by his predecessor, Hu Jintao.  The three titles apart from being President, are that he will also serve as a Head of the Communist Party and a Chairman of China’s military.

Speaking before members of the media, Minister for Foreign Affairs and International Co-operation, Hon. Bernard K. Membe (MP), said that this is an historical visit as China has been a close friend and a good partner of Tanzania for nearly fifty years.  Tanzania and China have been historical friendly allies since their signing of the Treaty of Friendship in February 1965.

“China is ranked as one of the top foreign investors in Tanzania’s national economy, and is expected to enter into further cooperative agreements with Tanzania in the sectors of agriculture, industries, energy and infrastructure,” said Hon. Membe. 

During his State Visit, President Xi Jinping also is expected to make his first international speech aims at highlighting Chinese Foreign Policy, in particular, the Afro-Sino future relations.  The China’s new stand on Afro-Sino relations is anxiously awaited due to recent first speech made by President Jinping’s as China’s new president whereby he promised his citizens to pursue a “great renaissance of the Chinese nation” and to deliver a more equitable society and a more effective, less corrupt government.

Since in the 1960s, China has contributed significant aid towards Tanzania that included the built of Tanzania-Zambia Railway (TAZARA), Friendship Textile Mill, Mubarali Rice Farm, Kiwira Coal Mine and Mahonda Sugar Cane Factory.  Further, Chinese Government has also cooperated with Tanzania in development projects in sectors of trade and agriculture, including the current project-building of the Convention Centre dedicated to the Late Mwalimu Julius Nyerere.  The two Governments have cooperated in many areas that include economy, trade, culture, education, health, and whereby Chinese investors have grown interest to invest in the extraction of natural resources particularly natural gas and oil in Tanzania.

The Tanzania-Chinese relation has grown profoundly for a decade since China established diplomatic relations with Tanganyika and Zanzibar on December 9, 1961 and December 11, 1963 respectively.  The political, economic and cultural relations have grown and prosper throughout the years to effect significant exchange of official visits between the two countries.  Since his Presidency, the Founder of then Tanganyika, the Late Mwalimu Julius Nyerere had visited China five times, including other Leaders such as former President Ali Hassan Mwinyi, former President Benjamin William Mkapa, President Kikwete when he was a Minister for Foreign Affairs and many others.  For Chinese Government, the officials visited Tanzania included Premier Zhou Enlai, Premier Zhao Ziyang, Vice Premier Hui Liangyu last year 2012 and several Foreign Ministers that included Hon. Tang Jiaxuan.

During his two-days State Visit, President Xi Jinping is expected to officiate the formal hand over ceremony of the Julius Nyerere International Convention Centre (JNICC), which was built by the Chinese Government and thereafter he will participate in a lay of a wreath ceremony at the Chinese Experts Cemetery at Majohe Village in Ukonga, Dar es Salaam.  

President Xi Jinping is expected to travel to South Africa on Monday evening 25 March 2013, upon the end of his State Visit here in Tanzania.


End.


Friday, March 22, 2013

TAARIFA KWA VYOMBO VYA HABARI


220px-Coat of arms of Tanzania.svg f1f71
 

TAARIFA KWA VYOMBO VYA HABARI KUHUSU ZIARA YA RAIS WA JAMHURI YA WATU WA CHINA, MHE. XI JINPING NCHINI, TAREHE 24 – 25 MACHI 2013 ILIYOTOLEWA NA WAZIRI WA MAMBO YA NJE NA USHIRIKIANO WA KIMATAIFA, MHE. BERNARD K. MEMBE (MB), TAREHE 22 MACHI 2013
1.0     UTANGULIZI
1.1     Ndugu waandishi, nimewaita leo ili kuwaeleza kuhusu ziara ya kihistoria hapa nchini ya Rais wa Jamhuri ya Watu wa China, Mhe. Xi Jinping ambayo itafanyika hivi karibuni. Najua mtakuwa mmekwishasikia kuwa Rais huyu atafika nchini hivi karibuni.
Sasa niwatangazie rasmi kuwa taarifa hii ni sahihi na ziara hiyo itafanyika tarehe 24 – 25 Machi, 2013. Ziara hii ni ya kwanza kwa Rais Xi barani Afrika mara tu baada ya kuchaguliwa katika nafasi hiyo ya Urais mnamo tarehe 14 Machi, 2013.
1.2     Mahusiano  ya  Tanzania na China yametoka mbali, tangu enzi ya waanzilishi wa mataifa haya mawili, yaani Mwalimu Julius Nyerere wa Tanzania na Mao Zedong  wa China. Ifahamike kuwa, kutokana na mahusiano haya ndipo mmoja ya miradi mikubwa kabisa iliyofanywa na China barani Afrika ulitokea. Mradi huu ni reli ya Tanzania na Zambia (TAZARA). Pamoja na kuwa mradi wa kimaendeleo, reli hii ya TAZARA ilitusaidia katika ukombozi wa bara la Afrika – kama moja ya njia za usafiri, hivyo kuifanya China kuwa rafiki wa kweli. Mradi mwingine mkubwa ni ujenzi wa jengo la Umoja wa Afrika, Addis Ababa, Ethiopia. Haya, kati ya mengineyo, yanafanya ugeni huu kuwa wa kihistoria na heshima kubwa kwetu.
 1.3    Rais Xi anakuja kwa mwaliko wa Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Mhe. Jakaya Mrisho Kikwete na akiwa nchini atafanya mazungumzo na mwenyeji wake Mheshimiwa Rais Kikwete, na Rais wa Zanzibar na Mwenyekiti wa Baraza la Mapinduzi, Mhe. Dkt Ali Mohamed Shein. Mheshimiwa Xi ataambatana na mke wake, pamoja na Maafisa Waandamizi wa Serikali ya China wasiopungua 25.
2.0     RATIBA YA MGENI KWA KIFUPI
2.1     Rais Xi Jinping atawasili nchini siku ya jumapili tarehe 24 Machi, 2013 saa 10:25 jioni katika Uwanja wa Ndege wa Kimataifa wa Mwalimu Julius Nyerere kwa ndege maalumu aina ya Boeing 747 ambapo atalakiwa na Viongozi mbalimbali wa Kitaifa wakiongozwa na Rais Jakaya Kikwete.
2.2     Baadaye Rais Xi pamoja na ujumbe wake watafanya mazungumzo rasmi na Rais Jakaya Kikwete pamoja na Viongozi Waandamizi wa Serikali ya Jamhuri ya Muungano wa Tanzania. Mazungumzo hayo yataanza saa 12:15 jioni na yatafanyikia Ikulu.
2.3     Baada ya mazungumzo rasmi, Rais Xi pamoja na mwenyeji wake Mheshimiwa Rais Jakaya Kikwete watashuhudia utiaji saini wa Makubaliano na Mikataba mbalimbali (kumi na tisa) ya ushirikiano baina ya Serikali ya Jamhuri ya Muungano wa Tanzania/na Serikali ya Mapinduzi ya Zanzibar  kwa upande mmoja na Serikali ya Jamhuri ya Watu wa China kwa upande mwingine. Kwa kifupi mikataba hiyo inahusu kukuza uwekezaji na biashara baina ya nchini za Tanzania na China, kukuza ushirikiano wa kiutamaduni baina ya nchi hizi mbili na watu wake, nk.
2.4     Baada ya tukio hilo, Rais Xi pamoja na ujumbe wake watahudhuria dhifa ya kitaifa itakayoandaliwa  kwa heshima yake na Rais Jakaya Kikwete. Dhifa hiyo itafanyika Ikulu kuanzia saa 1:40 usiku. Hilo ndilo litakuwa tukio la mwisho kwa siku ya kwanza.
2.5     Siku itakayofuata ya tarehe 25 Machi, 2013 saa 3:10 asubuhi Rais Xi atafanya mazungumzo rasmi na Rais wa Zanzibar na Mwenyekiti wa Baraza la Mapinduzi, Mhe. Ali Mohamed Shein pamoja na ujumbe wa Viongozi Waandamizi kutoka Serikali ya Mapinduzi ya Zanzibar.
2.6     Tukio litakalofuata litakuwa ni uzinduzi na makabidhiano rasmi ya kituo cha Mikutano cha Kimataifa cha Mwalimu Julius Kambarage Nyerere kilichojengwa kwa msaada wa Serikali ya China kwa lengo la kumuenzi Mwalimu Nyerere. Baada ya makabidhiano ndipo Rais Xi atatoa hotuba maalumu kwa Tanzania, Afrika na Dunia kwa ujumla. Hotuba hiyo itajikita katika kuelezea Sera ya Serikali mpya ya China kwa bara la Afrika. Watu kutoka kada mbalimbali kama vile Wahadhiri wa Vyuo Vikuu, Wanafunzi, Wabunge, Viongozi na Maafisa Waandamizi wa Serikali, Wafanyabiashara, n.k. wamealikwa kuhudhuria ukumbini hapo.
2.7     Mchana wa tarehe 25 Machi, 2013 Rais Xi Jinping ataelekea katika Makaburi ya Wataalamu wa Kichina ya Majohe yaliyopo katika kijiji cha Majohe – Ukonga ambapo atatoa heshima zake kwa Wachina waliofariki wakati wakijenga Reli ya TAZARA.
2.8     Baada ya hapo Rais Xi ataelekea Uwanja wa Ndege wa Julius K. Nyerere ambapo ataondoka saa 10:40 jioni kuelekea nchini Afrika Kusini kuhudhuria Mkutano wa tano wa Wakuu wa Nchi za BRICS.
 
3.0     FAIDA ILIYOPATA TANZANIA KUTOKANA NA UHUSIANO NA CHINA
3.1     Jambo kubwa Tanzania inalojivunia tangu kuanzisha uhusiano na China ni kukua kwa urafiki wa karibu sana na China;  urafiki wa kuaminiana na kusaidiana katika nyanja mbalimbali za kitaifa, kikanda na kimataifa. Uhusiano huo wa karibu unazidi kukua kila kukicha.
3.2     Kwa upande wa ushirikiano wa kiuchumi Tanzania inajivunia miradi mbalimbali ya kimaendeleo iliyotekelezwa kwa ushirikiano na China. Baadhi ya miradi hiyo ni pamoja na:

            i.    Mradi wa Reli ya TAZARA – kama nilivyoeleza hapo awali Mradi huu umekuwa mhimili na kiungo muhimu sana katika ukuzaji wa uchumi wa Tanzania na nchi jirani za Zambia, DRC, Zimbabwe n.k, hususan  katika sekta ya usafirishaji wa rasilimali ghafi, bidhaa za kibiashara na abiria
 
           ii.    Kiwanda cha nguo cha URAFIKI – (licha ya changamoto kadhaa zinazokikabili) kiwanda hiki kimetoa ajira kwa Watanzania wengi, pamoja na soko kwa pamba inayolimwa hapa nchini.
 
         iii.    Miradi mikubwa ya maji ya Shinyanga, Dar es Salaam na Pwani.
 
          iv.    Viwanja vya kisasa vya michezo – Uwanja wa Taifa (Dar es Salaam) na Karume Stadium (Zanzibar).
 
           v.    Kituo cha maonesho na majaribio ya zana za kilimo cha Mvomero, Morogoro.
 
          vi.    Kituo cha Mikutano cha Kimataifa cha Mwalimu Julius K. Nyerere. Manufaa ya Kituo hiki cha Mikutano ni kama yale yanayopatikana katika Kituo cha Kimataifa cha Mikutano cha Arusha (AICC).
 
        vii.    Mradi wa ujenzi wa mkongo wa Taifa kwa Tanzania bara na Zanzibar – mradi huu ni muhimu sana katika maendeleo ya sekta ya Teknohama (Teknolojia ya Habari na Mawasiliano). Manufaa yake yatapatikana si tu hapa Tanzania lakini pia kwa nchi za jirani kama vile Rwanda, Burundi, n.k, kwani huduma hii itatolewa kibiashara.
 
      viii.    Mradi wa bomba la gesi kutoka Mtwara hadi Dar es Salaam – Mradi huu utakapokamilika hapo mwakani utatupatia uhakika wa umeme, pamoja na kupunguza kwa kiasi kikubwa gharama zake. Pia utapelekea kupungua kwa gharama za maisha kwa ujumla na kukua kwa kipato cha mtu mmoja mmoja kiuchumi.
 
          ix.    Manufaa mengine mengi yanatarajiwa kupatikana mara baada ya ziara.

 
4.0     MATARAJIO YA TANZANIA KUTOKANA NA ZIARA HII
4.1     Katika ziara hii ya kihistoria Tanzania inatarajia kufaidika kwa namna mbalimbali kama ifuatavyo:
 

            i.    Kufungua milango ya uwekezaji katika sekta mbalimbali. Ziara hii inafuatiliwa na kumulikwa na nchi karibu zote duniani; pamoja na makampuni makubwa kila kona ya dunia. Ziara ya Rais wa huyu wa China inatuma ujumbe kwa wawekezaji kote duniani kuhusu mazingira mazuri na fursa za uwekezaji zinazopatikana nchini Tanzania.

 
           ii.     Wakati wa ziara hii mikataba na makubaliano zaidi ya 19 yatatiwa saini kati ya Serikali za Jamhuri ya Muungano wa Tanzania na Serikali ya Mapinduzi ya Zanzibar kwa upande mmoja, na Serikali ya China kwa upande mwingine (tafadhali rejea kiambatisho Na.1 kwa orodha ya Makubaliano na Mikataba iyakayotiwa saini.)
 
Kama ilivyoelezwa hapo awali, Mikataba na makubaliano haya yanagusa sekta za kilimo kibiashara, uwekezaji, uendelezaji wa miundombinu, miradi ya maji na umeme, fursa za kimasomo kwa vijana wa Kitanzania nchini China, nk.
 
5.0     HITIMISHO
5.1     Uhusiano kati ya Tanzania na China ni wa muda mrefu tangu miaka ya 1950 wakati bado Tanzania (Tanganyika kwa wakati huo) ikiwa katika harakati za kupigania Uhuru. Mwaka kesho (2014) nchi zetu mbili zitasherehekea miaka 50 ya uhusiano wa kidiplomasia. Uhusiano huu unatoa picha ya ukaribu uliopo kati ya Serikali za nchi za Tanzania na China pamoja na watu wake.
5.2     Hivyo basi, napenda kuchukua fursa hii kuwaomba Watanzania wote kwa ujumla tujitokeze kwa wingi kumlaki Rais Xi Jinping atakapokuwa anawasili kutoka Uwanja wa Ndege wa Kimataifa wa Julius K. Nyerere mpaka Hoteli ya Serena atakapofikia kwa kupitia Barabara ya Pugu/Julius K. Nyerere.


 

Mhe. Membe azungumza na Waandishi wa Habari kuhusu ziara ya Rais wa China hapa nchini

Waziri wa Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Kimataifa, Mhe. Bernard K. Membe (Mb.) akizungumza na Waandishi wa Habari (hawapo pichani) leo tarehe 22 Machi, 2013 kuhusu ziara ya kitaifa ya siku mbili ya Rais mpya wa Jamhuri ya Watu wa China, Mhe. Xi Jinping atakayoifanya hapa nchini kuanzia tarehe 24 hadi 25 Machi, 2013. Wengine katika picha ni Mhe. Mahadhi Juma Maalim (Mb.) (kulia), Naibu Waziri wa Mambo ya Nje na Bw. John Haule, Katibu Mkuu wa Wizara  wa Wizara ya Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Kimataifa.

Baadhi ya Waandishi kutoka Vyombo mbalimbali vya Habari vya hapa nchini wakimsikiliza Mhe. Membe (hayupo pichani) alipozungumza nao kuhusu ziara ya Rais wa China, Mhe. Xi Jinping hapa nchini.

Kundi jingine la Waandishi wa Habari wakifuatilia kwa makini taarifa ya Mhe. Membe kuhusu ziara ya Rais wa China hapa nchini.


Waandishi kutoka mashirika mbalimbali ya habari ya China pia walikuwepo kwenye mkutano huo.

Naibu Katibu Mkuu wa Wizara ya Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Kimataifa, Balozi Rajab Gamaha (kulia) akiwa na Balozi wa Tanzania nchini China, Mhe. Philip Marmo (katikati) pamoja na Mkurugenzi wa Idara ya Diaspora katika Wizara ya Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Kimataifa, Balozi Bertha Semu-Somi wakimsikiliza Mhe. Membe (hayupo pichani) alipozungumza na waandishi wa habari kuhusu ziara ya Rais wa China hapa nchini

Mmoja wa waandishi wa habari kutoka China akiuliza swali kwa Mhe. Membe (hayupo pichani) wakati wa mkutano kuhusu ziara ya Rais wa China hapa nchini

Mhe. Membe, Mhe. Maalim, Bw. Haule na Balozi Gamaha wakisikiliza swali kutoka kwa Mwandishi wa Habari (hayupo pichani) wakati wa mkutano kuhusu ziara ya Rais wa China, Mhe. Xi Jinping hapa nchini.

Minister Membe holds talks with British Minister Responsible for Africa Affairs


 Hon. Bernard K. Membe (MP), Minister for Foreign Affairs and International Co-operation welcomes Hon. Mark Simmonds, British Minister Responsible for Africa Affairs prior to their meeting held today in the Ministry in Dar es Salaam.


 Hon. Membe in discussion with Hon. Simmonds about the recent Zimbabwe Constitutional Referendum held on 16 March, 2013.  Hon. Membe led a team of observer from SADC -Troika, as Tanzania currently sits as a Chairman of the Organ.  (photo by Tagie Daisy Mwakawago)
 
 The meeting between Hon. Membe and Hon. Simmonds continues, while delegation from both countries listen. (photo by Tagie Daisy Mwakawago)

 Hon. Membe, Hon. Simmonds together with British delegation that consisted of H.E. Dianna Melrose, British High Commissioner to Tanzania, Mr. Alex Patridge (2nd left), Private Secretary to Minister Simmons and Ms. Susie Townend (left), Head of Southern Africa Department, Foreign & Commonwealth Office (FCO).

 Minister Membe (2nd left) and Hon. Simmonds (left), together with Tanzania delegation that included Ambassador Dora Msechu, Director of Europe and Americas in the Ministry of Foreign Affairs, Mr. Nathaniel Kaaya (2nd right), Acting Director of the Department of the Multilateral Cooperation and Ms. Zainab Angovi (right), Foreign Service Officer. 

 Hon. Simmonds (left) signing visitors' book during his meeting with Hon. Membe.

 Hon. Membe saying goodbye to H.E. Dianna Melrose, British High Commissioner to the United Republic of Tanzania.

Hon. Minister Bernard K. Membe (MP), listening to Hon. Mark Simmonds, British Minister of Responsible of African Affairs prior to say goodbye to him. (photo by Tagie Daisy Mwakawago)



Minister Membe holds talks with British Minister Responsible for Africa Affairs 

by Tagie Daisy Mwakawago 


Hon. Minister Bernard K. Membe (MP) of Foreign Affairs and International Co-operation today held talks with Hon. Mark Simmonds, British Minister Responsible for Africa Affairs, discussing various key issues of continuing cooperation between the two countries.  The two met in the Minister's office in Dar es Salaam.  

During their meeting, the Ministers held bilateral talks that also highlighted the UK G-8 Presidency which started January 2013, and the upcoming Summit scheduled for later this June 2013 in Ireland. 

Further to their discussion, the Ministers talked about regional issues that included the recent Constitutional Referendum in Zimbabwe and Madagascar.  Hon. Membe, who led the team of observers from SADC- Organ Troika, said that the team is gearing forward for a free, peaceful and fair election in the coming months. The Members of from the Organ  are Tanzania, Mozambique, Namibia and South Africa.

For his part, Hon. Simmonds praised the leadership of President Jakaya Kikwete in overseeing a positive, peaceful constitutional referendum held in Zimbabwe recently.  He said his country too was looking forward to see a free, peaceful and fair election take place in Zimbabwe.

"The UK and the European Union are ready to assist if there are any challenges, lack of resources and if additional observers were needed to make the election possible", he said.   
On Madagascar part, Hon. Simmonds also hailed President Kikwete for bridging peace talks between President Andry Rajoelina of Madagascar and Marc Ravalomanana, former President of Madagascar.  He said his country was eager to see a positive transition towards democratic government.

This year UK's G-8 Presidency Agenda is Tax, Trade and Transparency whereby Hon. Membe assured his counterpart Minister that the Agenda is also important for Tanzania as it will benefit on improving and imposing on frameworks that are relevant on transparency through trade and taxation. 

In concluding their meeting, both Ministers expressed to continue the friendly and traditional relations  that existed between UK and Tanzania for years.


End.




Wednesday, March 20, 2013

Mkurugenzi wa Kitengo cha Sheria akutana kwa mazungumzo na Mkurugenzi wa Idara ya Sheria ya Denmark

Mkurugenzi wa Kitengo cha Sheria katika Wizara ya Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Kimataifa, Balozi Irene Kasyanju akizungumza na Mkurugenzi wa Idara ya Sheria katika Wizara ya Mambo ya Nje ya Denmark, Balozi Thomas Winkler kuhusu ushirikiano kati ya Tanzania na Denmark katika masuala ya  sheria na mikataba mbalimbali  ya kimataifa ikiwemo masuala ya kupambana na Uharamia. Mazungumzo hayo yalifanyika Wizarani tarehe 20 Machi, 2013.

Balozi Winkler akichangia hoja wakati wa mazungumzo hayo huku Balozi Kasyanju akimsikiliza.


Balozi Kasyanju akimsikiliza Balozi Winkler wakati wa mazungumzo yao. Wengine katika picha ni Bw. Elisha Suku (kulia), Afisa Mambo ya Nje katika Kitengo cha Sheria, Wizara ya Mambo ya Nje, Bi. Mille Sofie Brandrup (kushoto), Afisa kutoka Idara ya Sheria za Kimataifa, Wizara ya Mambo ya Nje ya Denmark na Bw. Lars Bo Kirketerp Lund, Afisa kutoka Ubalozi wa Denmark hapa nchini.

Tuesday, March 19, 2013

Katibu Mkuu na Balozi wa India hapa nchini wasaini Mkataba wa Makubaliano kati ya CFR na ICWA

Katibu Mkuu wa Wizara ya Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Kimataifa, Bw. John Haule (kulia) kwa pamoja na Balozi wa India hapa nchini, Mhe. Debnath Shaw wakisaini Mkataba wa Makubaliano ya Ushirikiano (MoU) kati ya Chuo cha Diplomasia (CFR) cha Tanzania na Taasisi ya Utamaduni ya India (ICWA). Uwekaji saini huo ulifanyika Wizarani leo tarehe 19 Machi, 2013.

Mkurugenzi wa Chuo cha Diplomasia, Balozi Mohammed Maundi (kushoto) pamoja na Mkurugenzi wa Idara ya Asia na Australasia katika Wizara ya Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Kimataifa, Balozi Mbelwa Kairukiwakishuhudia uwekaji saini wa mkataba huo.

Wajumbe wengine waliohudhuria katika tukio hilo la uwekaji saini wa mkataba. Kutoka kushoto ni Afisa kutoka Ubalozi wa India hapa nchini, Bw. Gobal Krisha  na Bw. Ali Ubwa, Afisa Mambo ya Nje kutoka Kitengo cha Sheria.

Bw. Haule akibadilishana Mkataba na Balozi Shaw mara baada ya kusaini.


Katibu Mkuu, Bw. Haule pamoja na Balozi Shaw wakionesha Mkataba huo.

Katibu Mkuu Bw. Haule akizungumza na Balozi Shaw mara baada ya kukamilisha zoezi la uwekaji saini mkataba wa Ushirikiano kati ya Chuo cha Diplomasia cha Tanzania na Taasisi ya Utamaduni ya India.

Mhe. Balozi Shaw akichangia hoja wakati wa mazungumzo na Bw. Haule huku wajumbe wengine wakisikiliza.

Mhe.Naibu Waziri akutana kwa mazungumzo na Katibu Mtendajii wa Kamisheni ya Uchumi ya UN kwa Afrika

Naibu Waziri wa Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Kimataifa, Mhe. Mahadhi Juma Maalim (Mb.) akimkaribisha Katibu Mtendaji wa Kamisheni ya Uchumi ya Umoja wa Mataifa kwa Bara la Afrika, Bw. Carlos Lopes,  Ofisini kwake leo tarehe 19 Machi, 2013 ambapo walizungumzia masuala mbalimbali ya ukuzaji uchumi hapa nchini ikiwemo maendeleo ya viwanda.

Mhe. Maalim akiwa katika mazungumzo na Bw. Lopes.

Mhe. Maalim akimsikiliza kwa makini Bw. Lopes wakati wa mazungumzo yao.

Mhe. Maaalim akifafanua jambo kwa Bw. Lopes wakati wa mazungumzo yao. Mwingine katika picha ni Bw. Antonio Pedro, Mkurugenzi wa Kamisheni hiyo kwa Ukanda wa Afrika Mashariki.

Mhe. Maalim akimweleza jambo Bw. Lopes (hayupo pichani) wakati wa mazungumzo yao. Wengine katika picha ni Bw. Nathaniel Kaaya (wa pili kulia), Kaimu Mkurugenzi wa Idara ya Ushirikiano wa Kimataifa katika Wizara ya Mambo ya Nje, Bw. Ali Mwadini (mwenye tai nyekundu), Msaidizi wa Naibu Waziri na Bw. Macocha Tembele (kulia), Afisa Mambo ya Nje katika Idara ya Ushirikiano wa Kimataifa.


Mhe. Maalim na wajumbe wengine wakimsikiliza Bw. Lopes.


Monday, March 18, 2013

Mhe. Naibu Waziri afungua mkutano kuhusu ushirikiano wa India na Afrika

Naibu Waziri wa Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Kimataifa, Mhe. Mahadhi Juma Maalim (katikati) (Mb.) akifungua mkutano wa siku mbili ulioaandaliwa na Taasisi ya Utafiti wa masuala  ya Kiuchumi na Kijamiii (ESRF) ya hapa nchini kuhusu mahusiano kati ya India na Afrika. Mkutano huo ambao uliwahusisha wasomi kutoka Vyuo Vikuu mbalimbali duniani ulifanyika katika Hoteli ya Protea Courtyard Jijini Dar es Salaam.

Mhe. Maalim (wa nne kutoka kushoto) akiwa katika picha ya pamoja na wajumbe wa mkutano kuhusu ushirikiano kati ya India na Afrika.

Tanzania hosts a three-day Meeting on Prevention of Atrocities


Hon. Mathias Chikawe (MP), Minister for Constitution and Legal Affairs gives his opening remarks during the High Level Working Meeting on Prevention of Atrocities, particularly on genocide prevention and responsibility to protect.  The Meeting is held at Protea Courtyard Hotel in Dar es Salaam.  Listening is H.E. Olvier Chave (left), Ambassador of Switzerland in the United Republic of Tanzania. 

During his opening remarks, Hon. Chikawe said it is not by sheer luck that Dar es Salam is the right venue to host such important meeting.  He said that preventing mass atrocities in our countries requires partnering with citizens, civil societies, media, private sector and important countries such as Switzerland who is funding this meeting.

Hon. Chikawe concluded his remarks saying, that the Meeting will produce substantial deliberations which will "contribute to efforts towards collective responsibility on preventing any future genocide tragedy and raise awareness on responsibility to protect hence creating a peaceful world." 

Several experts from different countries that included Costa Rica, Argentina, Tanzania, Australia, Switzerland, Denmark and civil society organizations listening to the opening remarks by Hon. Chikawe. 

Tanzania delegation in participation during the High Level Working Meeting on Prevention of Atrocities.  Also in the photo is Mr. Nathaniel Kaaya (2nd right), Acting Director of the Department of Multilateral Cooperation. 

Hon. Mathias Chikawe (MP) (2nd left), Minister for Constitution and Legal Affairs continues with his opening remarks during the High Level Working Meeting on Prevention of Atrocities.  Left is H.E. Olvier Chave, Ambassador of Switzerland in the United Republic o Tanzania. 

Hon. Minister Chikawe (center) in a light moment with Ambassador Liberata Mulamula (right), Senior Advisor to President Jakaya Mrisho Kikwete (Diplomatic Affairs) and H.E. Ambassador Olvier Chave (left), Ambassador of Switzerland in the United Republic of Tanzania.


H.E. Ambassador Olvier Chave (left) exchanges views with Mr. Matteo Facchinotti, Deputy Head Section of the Security Council and Political Affairs in Switzerland. 

Mr. Miraji Magai (right), Secretary of the Tanzania National Committee on Prevention of Genocide exchanges views with one of the experts on genocide prevention.

A group photo of Hon. Mathias Chikawe (MP) (seated - center), Minister for Constitution and Legal Affairs together with experts on genocide prevention that included countries from Australia, Argentina, Denmark, Costa Rica, Switzerland, Tanzania and Civil Society Organizations.



All photos courtesy of Protea Courtyard Hotel