Wednesday, March 18, 2015

Gavana wa Benki Kuu ya Tanzania awasilisha mada kwa Watumishi wa Wizara ya Mambo ya Nje

Gavana wa Benki Kuu ya Tanzania, Prof. Benno Ndulu akiwasilisha mada kuhusu  "Exchange Rate Developments in Tanzania and Implications for the Economy"  kwa Watumishi wa Wizara ya Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Kimataifa wakati wa Semina fupi iliyofanyika katika Ukumbi wa Mikutano wa Kimataifa wa Julius Nyerere (JNICC), Dar es Salaam tarehe 18 Machi, 2015.  Katika mada yake Prof. Ndulu  alielezea pamoja na mambo mengine umuhimu wa Tanzania kuuza zaidi bidhaa zake nje ili kudhibiti mfumuko wa bei na kuipandisha thamani  Sarafu ya Tanzania dhidi ya sarafu nyingine hususan Dola ya Marekani, kuimarisha upatikanaji wa fedha za nje kama dola na kuvutia zaidi wawekezaji nchini.
Waziri wa Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Kimataifa,  Mhe. Bernard K. Membe (Mb.) (katikati) akifuatilia uwasilishwaji wa mada kutoka kwa Prof. Ndulu (hayupo pichani). Kushoto ni Kaimu Katibu Mkuu wa  Wizara ya Mambo ya Nje, Balozi Irene Kasyanju na kulia ni Balozi Mstaafu Elly Mtango.    
Mkurugenzi wa Idara ya Asia na Australasia katika  Wizara ya Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Kimataifa, Balozi Mbelwa Kairuki akiwa na  Katibu wa Waziri Membe, Bw. Thobias Makoba  wakimsikiliza Prof. Ndulu ambaye hayupo nchini.
Waziri Membe akielezea jambo mara baada ya Gavana kumaliza kutoa mada 
 Mkurugenzi Idara ya Ushirikiano wa Kimataifa Balozi Celestine Mushy (katikati), akiwa pamoja na Mkurugenzi Idara ya Ulaya na Amerika,  Balozi Joseph Sokoine na Mkuu wa Kitengo cha Mawasiliano,  Bi Mindi Kasiga wakati wa Semina hiyo.
Sehemu ya Watumishi kutoka Wizara ya Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Kimataifa wakifuatilia Semina iliyokuwa ikiendeshwa na Prof.  Ndulu.
Mkurugenzi wa Chuo cha Diplomasia (CFR), Balozi. Omary Mohamed Maundi akiuliza swali kwa Prof. Ndulu wakati wa semina iliyofanyika katika ukumbi wa JNICC Jijini Dar es Salaam.
Prof. Ndulu akifafanua jambo
Wakurugenzi kutoka Chuo cha Diplomasia wakisikiliza semina iliyokuwa ikitolewa na Prof. Ndulu. Mwenye tai nyeusi ni Dr. Watengere Kitojo  na kulia ni Dr. Bernard Archiula.
Mchumi kutoka Wizara ya Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Kimataifa, Bw. Joseph Mwasota akiomba ufafanuzi wa hoja kutoka  kwa Prof. Ndulu ambaye hayupo pichani.
Prof. Ndulu akiendelea kutoa majibu yaliyokuwa yakiulizwa katika semina hiyo.
Mhasibu Mkuu wa Wizara ya Mambo ya Nje, Bw. Paul Kabale (kushoto) akiwa na Mkaguzi Mkuu wa Ndani,  Bw. Mathias Abisai pamoja na  Mkurugenzi wa Idara ya Ununuzi, Bw. Elias Suka wakati wa semina hiyo.
Sehemu nyingine ya washiriki katika Semina hiyo
Prof. Benno Ndulu akibadilshana mawazo na Mkurugenzi wa Masomo wa Chuo cha Diplomasia Dkt. Watengere Kitojo.  
Waziri Membe akizungumza na  na Waandishi wa Habari 
Picha ya pamoja baada ya kumalizika kwa Semina.

Picha na Reginald Philip na Reuben Mchome

Waziri Membe amwakilisha Rais Kikwete, Lesotho


Waziri wa Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Kimataifa, Mhe. Bernard K. Membe (Mb) wa katikati alipokuwa anaingia kwenye uwanja uliotumika kumwapisha Waziri Mkuu mpya wa Lesotho, Mhe. Pakalitha Mosisili jijini Maseru jana. wengine katika picha, kutoka kulia ni Bibi Talha Mohammed, Afisa kutoka Wizara ya Mambo ya Nje na Mhe. Radhia Msuya, Balozi wa Tanzania nchini Afrika Kusini ambaye pia anawakilisha Lesotho. kutoka kushoto ni Maafisa wa Serikali ya Lesotho.

Waziri Mkuu mpya wa Lesotho, Mhe. Mosisili (kushoto) akikabidhiwa Bendera ya nchi hiyo na Waziri Mkuu wa Zamani, Mhe. Thom Thabane kama ishara ya kukabidhiwa rasmi madaraka ya uwaziri Mkuu.



Waziri Mkuu mpya wa Lesotho, Mhe. Pakalitha Mosisiliakitoa neno la shukrani baada ya kuapishwa.
Viogozi mbalimbali wa Lesotho na kutoka nje ya Lesotho, mwenye kofia nyeupe ni mke wa mfalme wa Lesotho akiwa na mumewe ambaye ni Mfalme wa Lesotho.


Mandhari ya Uwanja livyokuwa wakati wa sherehe za uapisho.



Waziri Membe (katikati) alipokuwa anawasili katika Uwanja wa Ndege wa Maseru kwa ajli ya kushiriki sherehe za uapisho. Mwingine ni Balozi wa Tanzania mchini Afrika Kusini, Mhe. Bibi Radhia Msuya.

Rais wa Afrika Kusini, Mhe. Jacob Zuma akiwasili Lesotho kwa ajili ya kushiriki sherehe za uapisho.

Rais Mteule wa Namibia, Mhe. Hage Geingob naye akiwasili Lesotho kwa ajili ya sherehe za uapisho.

Waziri Membe akihojiwa na Mwandishi wa Habari wa TBC, Bw. Stanley Ganzel mara baada ya sherehe kukamilika.



Na Ally Kondo, Lesotho
Nchi za Afrika zimetakiwa kujifunza kutoka Lesotho, nchi ambayo dunia inashuhudia imekuwa na utaratibu wa kubadilishana madaraka kwa utulivu na amani bila fujo za aina yoyote. Kauli hiyo ilitolewa na Waziri wa Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Kimataifa, Mhe. Bernard K. Membe (Mb) wakati wa sherehe za kumuapisha Waziri Mkuu mpya, Mhe. Pakalitha Mosisili zilizofanyika jijini Maseru siku ya Jumanne tarehe 17 Machi 2014. Waziri Membe alimwakilisha Rais Jakaya Kiwete katika sherehe hizo.

Mhe. Mosisili amerudi madarakani baada ya Chama chake cha Democratic Congress (DC) kuungana na vyama vingine sita vidogo kuunda Serikali ya Mseto. Mhe. Mosisili alikuwa Waziri Mkuu wa Lesotho kwa miaka 15 (1998 – 2012) na amerudi madarakani katika uchaguzi mkuu uliofanyika tarehe 28 Februari 2015. Uchaguzi huo ulifanyika mapema kwa miaka miwili kutokana na matatizo ya kisiasa yaliyosababisha kuvunjika kwa Serikali ya Mseto iliyokuwa inaongozwa na Waziri Mkuu wa Zamani, Mhe. Thom Thabane.

Katika hotuba yake, Mhe. Mosisili alisema kuwa nchi hiyo inakabiliwa na changamoto nyingi, hivyo, aliahidi kutumia uzoefu wake kuhakikisha kuwa nchi inaondokana na migogoro ya kisiasa ili iweze kusonga mbele kiuchumi.

Viongozi wengine waliohudhuria sherehe hizo ni pamoja na Rais wa Afrika Kusini,  Mhe. Jacob Zuma, Rais Mteule wa Namibia, Mhe. Hage Geingob na Katibu Mtendaji wa Jumuiya ya Maendeleo ya Nchi za Kusini mwa Afrka (SADC), Dkt. Stergomena Tax.

Tuesday, March 17, 2015

PRESS RELEASE



Hon. Bernard Membe (left), Minister for Foreign Affairs and International Cooperation in  a photo with Mr. Julius Shirima, winner of the African region and an overall winner amongst 18 finalists for the pan-Commonwealth Youth Awards of 2015



PRESS RELEASE
Tanzanian government has applauded the work of DARECHA, a youth owned micro-venture capital firm that builds capacity of young people in entrepreneurial skills as well as promoting businesses in a shared network. Its founder, Mr. Julius Shirima (26) is a recent winner of Commonwealth Youth Awards 2015 for his commitment in lifting lives of his fellow youth through entrepreneurship.

In his brief meeting with Mr. Shirima, Hon. Bernard Membe, the Minister for Foreign Affairs and International Cooperation and also the current chair of Commonwealth Ministerial Action Group said DARECHA’s business model not only promotes young businesses and assists young people of Tanzania but is also inspirational.

“Your work inspires all of us and I do hope that your fellow youth will emulate such initiative, in different areas. Well done, congratulations” said Minister Membe.

Mr. Shirima emerged winner of the African region and an overall winner amongst 18 finalists for the pan-Commonwealth Youth Awards of 2015. In addition to the decorated awards, Mr. Shirima also received 5,000 pounds to be re-invested into his business. Other winners from other regions received 3,000 pounds each.

Through Mr. Shirima’s DARECHA a network of over 5,000 young people is established which enables young Tanzanian entrepreneurs to transform their business ideas into profitable ventures and eventually provide employment to other young people. DARECHA’s business model has also been adopted in other countries in the region.

“We at the Foreign office are very proud of Mr. Shirima’s accomplishments in the country and now outside, to the Commonwealth. My office and I will provide the necessary support for his endeavor, for Tanzania’s future leaders” concluded Mr. Membe.

Hon. Membe met with Mr. Shirima briefly after adjourning the Commonwealth Ministerial Action Group (CMAG) which he currently chairs. Commonwealth has 53 member states and nine out of these forms CMAG. Other Commonwealth countries also in CMAG are New Zealand (Vice Chair), Gayana, Solomon Island, Pakistan, Cyprus, India, Siera Leone and Sri Lanka.


Issued by:
Government Communication Unit,
Ministry of Foreign Affairs and International Cooperation.
16.03.2015







Waziri Mkuu akutana na Watanzania waishio nchini Japan

Waziri Mkuu, Mizengo Pinda akisalimiana na Bibi wa Kijapan, Midori Uno,machi 17, 2015 kwenye hoteli ya New Otani jijini New York , ambaye aliishi Tanzania miaka ya 60 baada ya Uhuru wa Tanganyika akifanya kazi kwa kujitolea. Hisasa Bibi Uno ni bingwa wa lugha ya kiswahili na amekwishaandika Kamusi ya Kijapan na Kiswahili pamoja na vitabu kadhaa.
Waziri mkuu, Mizengo Pinda na mkewe wakitia saini kitabu cha wageni kwenye ubalozi wa Tanzania uliopo Tokyo nchini Japan baada ya kuwasili ubalozini hapo kuzungumza na Watanzania waishio Japan Machi 17, 2015. Kulia ni Balozi wa Tanzania nchini Japan aliyemaliza muda wake, Salome Sijaona na Wapili kulia ni Waziri wa Nchi Ofisi ya Makamu wa Pili wa Rais wa Zanzibar, Mohamed Abood Mohamed. Kushoto ni Balozi wa Tanzania nchini Japan, Batilda Buriani na wapili kushoto ni Naibu Waziri wa Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Kimataifa. Mahadh Maalim.
Waziri Mkuu, Mizengo Pinda akiwa kwenye picha ya pamoja na baadhi ya Watanzania waishio nchini Japan.

Monday, March 16, 2015

Press Release

H.E Michael D. Higgins, President of Ireland


PRESS RELEASE

H.E. Jakaya Mrisho Kikwete, President of the United Republic of Tanzania has sent a congratulatory message to H.E. Michael D. Higgins, President of Ireland on the occasion of the National Day of Ireland on 17th March 2015.

The message reads as follows;


“H.E. Michael D. Higgins,
President of Ireland
Dublin

IRELAND


Your Excellency and Dear Colleague,

It is my pleasure and privilege to extend to you and through you to the Government and people of Ireland my heartfelt congratulations on the occasion of your country’s National Day.

Tanzania cherishes the good relations and co-operation that happily exist between our two countries.  On this historic day, I take the opportunity to reaffirm my country’s commitment and desire to continue working with you and your Government in strengthening further the existing ties of friendship and co-operation for the mutual benefit of our two countries and peoples.

        Please accept, Your Excellency, my best wishes for your continued good health and prosperity for the people of Ireland”.



Issued by the Ministry of Foreign Affairs and International Cooperation, Dar es Salaam

16th March 2015

WAZIRI MEMBE AKUTANA NA MTANZANIA ALIYESHINDA TUZO ZA COMMONWEALTH MJINI LONDON

Mhe. Bernard Membe (Mb.), Waziri wa Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Kimataifa akiwa na Julius James Shirima, mshindi wa Tuzo ya Vijana wa Nchi za Jumuiya ya Madola upande wa Afrika. Kwenye mazungumzo mafupi, Mhe. Membe alimpongeza Shirima kwa tuzo hizo na aliahidi kumpa ushirikiano kupitia Wizara anayoiongoza ili vijana wengi wa Kitanzania wanufaike na mchango wa Shirima na pia waige mfano wake na kuendelea kupeperusha vema bendera ya Tanzania.

Bw. Julius Shirima, mshindi wa Tuzo za Vijana wa nchi za Jumuiya ya Madola akiwa kwenye picha ya pamoja na Mhe. Bernard Membe, ambaye alifanya naye mazungumzo mara baada ya kumaliza kuendesha kikao cha Mawaziri wa Kikosi Kazi cha Jumuiya ya Madola mjini London hivi karibuni. Wengine kwenye picha ni Mhe. Peter Kallaghe, Balozi wa Tanzania nchini Uingereza, Mhe. Bernard Membe, Julius Shirima, Bi. Mindi Kasiga, Mkuu wa Kitengo cha Mawasiliano ya Serikali na Balozi Celestine Mushy Mkuu wa Idara ya Ushirikiano wa Kimataifa. 

Julius James Shirima akiwa amebeba Siwa ya Jumuiya ya Madola ambapo aliongoza maandamano ya Malkia Elizabeth kwenye sherehe hizo kama mshindi wa Tuzo za Vijana wa Nchi za Jumuiya ya Madola mwaka 2015. 

Malkia Elizabeth wa II, ambaye pia ni Mkuu wa Nchi 16 kati ya nchi 53 wanachama wa Jumuiya ya Madola akiwapongeza washindi Wanne wa Tuzo za Jumuiya ya Madola kutoka Afrika, Asia, Pacific na Karibian & Amerika, kabla ya kuzindua sherehe za Jumuiya hiyo mjini London, Uingereza. Pichani kulia ni Katibu Mkuu wa Jumuiya hiyo Mhe. Kamalesh Sharma ambaye ndiye aliyekabidhi tuzo hizo kwa niaba ya malkia.


Washindi wa Tuzo za Vijana wa Nchi za Jumuiya ya Madola kwenye picha ya pamoja. Kutoka kushoto, majina yao na eneo waliloshindia kwenye mabano ni Bi. Brianna Frueann 16 wa Samoa (Pacific), Bw. Julius Shirima 26 (Afrika), Bi. Gulalai Ismael wa Pakistan (Asia) na Bi. Nolana Lynch wa Trinidad na Tobago (Caribbean & Americas) 


Bw. Julius Shirima akiwa nje ya Jengo la Jumuiya ya Madola Jijini London Uingereza wakati wa sherehe za jumuiya hiyo.

Sunday, March 15, 2015

Ziara ya mafunzo kutoka U.S. Army War Collage ofisi za Uwakilishi wa Kudumu wa Tanzania umoja wa mataifa

Mhe. Balozi akielezea jambo mbele ya  kikundi  cha wanajeshi wanafunzi  ambao wapo katika  mafunzo  katika chuo cha U.S Army War Collage, wanafunzi hao walipata fursa ya kumuuliza Balozi maswali mbalimbali na ambayo yalijibiwa kwa ufasaha na  Mhe. Balozi.
Kiongozi wa Msafara akitoa zawadi yao kwa Mhe. Balozi kama kumbukumbu  na shukrani yao kwa kupokelewa na kwa Balozi kutenga muda wake kukutana nao.
Mhe. Balozi Tuvako  Manongi akiwa katika picha ya pamoja na Wanajeshi kutoka U.S Army War Collage,  miongoni mwa wanafunzi hao ni Mtanzania Luteni Kanali Juma Sipe kutoka JWTZ
Mhe. Balozi Manongi akiteta jambo na Luteni Kanali Juma Sipe  kutoka JWTZ ambayo  yuko mafunzoni U.S Army War Collage hapa Marekani

Mhe. Balozi Tuvako Manongi mwishoni mwa wiki alikutana na ujumbe wa wanawajeshi wanafunzi kutoka chuo cha Kijeshi (U.S. Army War Collage) ambao walikuwa katika ziara ya mafunzo. Miongoni mwa wanafunzi yupo Luteni Kanali Juma Sipe kutoka JWTZ. Ugeni huo ulitumia ziara hiyo kujifunza masuala mbalimbali yanayoihusu Tanzania kitaifa na kimataifa na uwepo wake kama nchi mwanachama wa Umoja wa Mataifa. 

TASWIRA KUTOKA UMOJA WA MATAIFA JIJINI NEW YORK

 Mhe. Waziri   Simba akisalimiana na  First Lady wa Kenya Mama Margaret Kenyatta, First Lady huyu   hukimbia mbio za marathon kama njia moja wapo ya kufatua  raslimali za kuwasaidi akina mama wenzie na watoto walio katika mazingira magumu.
Mkutano huu wa mbao ni wa waki mbili unafanyika sambamba na maadhimisho ya miaka 20 tangu kufanyika kwa mkutano wa kihistoria wa wanawake uliofanyika mwaka 1995 huko Beijing, China.
Pamoja na kuhudhuria mbalimbali inayohusianana Kimesheni   Kuhusu Hadhi ya Wanawake,   Mwakilishi wa Kudumu wa wa Tanzania katika Umoja wa Mataifa,  alipata fursa ya kuwapokea na kuzungumza na wageni mbalimbali waliofika katika Uwakilishi wa Kudumu. Balozi Manongi akiwa na Wabunge wa Bunge la Jamhuri ya Muungano wa Tanzania ambao walikuwa  Jijini  New York  kwa shughuli za Kikazi.  
" Utanzania na uzalendo kwanza" ndivyo anavyoelekea kusema Mhe. Susan Lymo wakati yeye na wabunge wenzie   walipofika katika Uwakilishi wa Kudumu wa Tanzania katika Umoja wa Mataifa.
Mhe. Waziri Sophia Simba  akiwa na  Mbunge wa Kawe Mhe. Halima Mdee,  Katibu Mkuu Anna Maembe, na Balozi  Tuvako Manongi katika moja wa  mikutano ya pembezoni iliyokuwa  inakwenda sambamba na  majadiliano  ya jumla ya Kamisheni ya 59. Mkutano huu  uliandaliwa na  Mke wa Rais wa  Kenya Mama, Margaret Kenyata,  ambapo alitumia fursa hiyo kuelezea shughuli anazozifanya  za kuwasaidia wanawake  na watoto wa nchi mwake hasa wale walio katika mazingira magumu. Kampeni yake inayoitwa Beyond Zero inalenga katika kufikisha huduma za afya


==============================================
Wajumbe wanaohudhuria Mkutano wa 59 wa Kamisheni kuhusu Hadhi ya Wanawake, kwa wiki kuanzia jumatano hadi Ijumaa wameendelea na jukumu kubwa la kujadiliana, kuhabaridha,a kubadilishana uzoefu, kuelimisha na hata kujifunza namna ya kuzikabilia changamato mbalimbali ambazo mwanamke na mtoto wea kike wanaendelea kukabiliana nazo. 

Mkutano huu wa mbao ni wa waki mbili unafanyika sambamba na maadhimisho ya miaka 20 tangu kufanyika kwa mkutano wa kihistoria wa wanawake uliofanyika mwaka 1995 huko Beijing, China. 

 Ujumbe wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania wenye wajumbe kutoka Serikali ya Mapinduzi Zanzibar unaongozwa na Mhe. Sophia Simba ( Mb) Waziri wa Maendeleo ya Jamii, Jinsia na Watoto na umekuwa ukishiriki majadiliano ya jumla na mikutano ya pembezo iliyobeba maudhui mbalimbali lakini yote yakilenga katika usawa wa jinsia na uwezeshwaji wa mwanamke.