Friday, July 3, 2015

Rais Kikwete azindua rasmi Kiwanda cha Viuadudu Wilayani Kibaha

Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Mhe.Dkt.Jakaya Mrisho Kikwete pamoja na Waziri Mkuu wa Ethiopia Mhe.Hailemariam Desalegn wakikata utepe kwenye uzinduzi wa Kiwanda cha kuzalisha Viuadudu vya kuua Viluwiluwi vya Mbu wanaoeneza Malaria kilichopo eneo la viwanda-TAMCO Kibaha Mkoani Pwani. Uzinduzi huo ulifanyika tarehe 02 Julai, 2015. Wanaoshuhudia pembeni ni Waziri Mkuu, Mhe. Mizengo Pinda na Balozi wa Cuba nchini, Mhe. Jorge Tormo.
Rais Kikwete pamoja na Waziri Mkuu wa Ethiopia wakizindua rasmi Kiwanda cha kuzalisha viuadudu vya kuua viluwiluwi vya mbu wanaoeneza ugonjwa wa Malaria.
Mhe. Rais Kikwete akizungumza na wananchi waliohudhuria  uzinduzi wa kiwanda hicho.Wanaomsikiliza ni Mhe. Desalegn, Mhe. Pinda na Mhe. Tormo.
Waziri Mkuu wa Ethiopia, Mhe.Hailemariam Desalegn akihutubia umati wa watu wakati wa uzinduzi wa kiwanda hicho kilichopo Wilayani Kibaha.
Sehemu ya umati wa watu waliohudhuria uzinduzi wa kiwanda hicho,wakimsikiliza kwa makini Mhe. Rais Kikwete (hayupo pichani) 
Mhe. Rais Kikwete kwa pamoja na Mhe. Desalegn, Mhe. Pinda, Mama Salma Kikwete na Waziri wa Viwanda na Biashara, Mhe. Abdallah Kigoda wakifurahia jambo wakati wa hafla ya uzinduzi wa Kiwanda cha kuzalisha Viuadudu vya kuua viluwiluwi vya mbu wanaoeneza malaria kilichopo Wilayani Kibaha
Balozi Joseph Sokoine (wa kwanza mstari wa mbele kulia) akiwa na Mabalozi mbalimbali wanaoziwakilisha nchi zao hapa nchini wakiwa wamesimama wakati wa hafla ya uzinduzi wa kiwanda hicho.
Katibu Mkuu wa Wizara ya Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Kimataifa,  Balozi Liberata Mulamula akifurahia jambo na Mhe. Rais Kikwete pamoja na Waziri Mkuu wa Ethiopia, Mhe. Desalegn wakati wa uzinduzi wa kiwanda hicho.
Rais Kikwete pamoja na Waziri Mkuu wa Ethiopia wakipata maelezo kutoka kwa mmoja wa Wataalam wa kiwanda hicho cha kuzalisha viuadudu vya kuua viluwiluwi vya mbu wanaoeneza Malaria
 Juu na Chini ni baadhi ya mitambo ya kuzalisha Viuadudu hivyo vya kuulia viluwiluwi vya mbu wanaoeneza malaria.

Picha na Reuben Mchome

Thursday, July 2, 2015

Wizar yaidhinisha Michoro ya Makao Makuu

Balozi Hassan Simba Yahya, Naibu Katibu Mkuu wa Wizara ya Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Kimataifa (kulia), na Bibi Li Xi, Mkurugenzi wa Idara ya Nje ya Taasisi ya Michoro ya Majeno na Utafiti ya Citic ya China, wakitia saini makubaliano ya michoro ya Makao Makuu Mapya ya Wizara jijini Dar Es Salaam jana.
Balozi Yahya na Bibi Li wakibadilishana hati za makubaliano waliyosaini.
Balozi Yahya na Bibi Li wakionyesha hati za makubaliano ya michoro ya Makao Makuu mapya ya wizara ya Nje.

Wizara ya Mambo ya Nje kujenga jengo jipya

Naibu Katibu Mkuu wa Wizara ya Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Kimataifa, Balozi Hassan Simba Yahya kulia na Mwakilishi wa Kampuni itakayojenga jengo la Wizara ya Mambo ya Nje wakiweka saini Makubaliano ya mchoro wa jengo hilo.
Balozi Yahya akibadilishana nyaraka za makubaliano ya michoro ya jengo la Wizara na Mwakilishi wa Kampuni itakayojenga jengo hilo.
Wizara ya Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Kimataifa, imeidhinisha michoro ya Jengo jipya la wizara hiyo, litakalojengwa jirani na Ukumbi wa Kimataifa wa Mikutano wa Julius Nyerere, jijini Dar Es Salaam.
Makubaliano kuhusu michoro hiyo ya jengo la ghorofa sita, litakalogharamiwa na Serikali ya Jamhuri ya Watu wa China, yametiwa saini jana baina ya wizara na mwakilishi wa mkandarasi wa ujenzi.
Akiongea baada ya kutia saini makubaliano hayo kwa niaba ya wizara, Naibu Katibu Mkuu, Balozi Hassan Simba Yahya, alisema hatua hiyo inatoa fursa kwa matayarisho ya ujenzi kuanza, na kuwa kazi ya ujenzi inatarajiwa kuanza kabla ya mwisho wa muhula wa Serikali ya Awamu ya Nne.
"Tumekamilisha hatua muhimu katika matayarisho ya ujenzi wa Jengo la Wizara," alisema, na kuongeza kuwa mradi huu ulianzishwa na Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Mhe. Jakaya Kikwete.
Utiaji saini wa makubaliano ya michoro hiyo ulishuhudiwa na wawakilishi wa Wakala wa Majengo (TBA).

Wednesday, July 1, 2015

Press Release


H.E. Jakaya Mrisho Kikwete, President of the United Republic of Tanzania has sent congratulatory message to The Right Honourable Stephen Harper, Prime Minister of Canada on the occasion of the National Day of Canada.

The message reads as follows.

“The Right Honourable Stephen Harper,
  The Prime Minister of Canada,

          Rt. Honourable and Dear colleague,

On behalf of the People and the Government of the United Republic of Tanzania, and indeed on my own behalf, I extend to you and through you to the People of Canada, my sincere congratulations on the occasion of Canada's National Day.

Tanzania and Canada continue to enjoy excellent bilateral relations that date back to the early years of our independence. Throughout the years, our two nations have continued to work together to strengthen our friendship, cooperation and partnership both at the individual and Government levels. As you celebrate your county's National Day, I take this opportunity to reiterate my personal commitment and that of my Government to work closely with you and Your Government in elevating to greater heights, the cordial bilateral relations that happily exist between our two countries and peoples.

I wish you, Rt. Honourable, personal good health and prosperity as you lead the people of Canada.

May I once again congratulate you on your National Day. Please accept, Rt. Honourable Prime Minister, the assurances of my highest consideration.


Issued by the Ministry of Foreign Affairs and International Cooperation. Dar es Salaam, 30th June, 2015
 

Waziri Mkuu wa Ethiopia awasili nchini kwa ziara ya kikazi

Waziri Mkuu wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Mhe. Mizengo Peter Pinda (kulia) akimtambulisha Waziri wa Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Kimataifa, Mhe. Bernard K. Membe (Mb.) kwa Waziri Mkuu wa Ethiopia, Mhe. Hailemariam Desalegn (Katikati) mara baada ya kuwasili katika Uwanja wa ndege wa Kimataifa wa Julius Nyerere Jijini Dar es Salaam. Mhe. Desalegn yupo nchini kwa ziara ya kikazi ya siku mbili ambapo pamoja na mambo mengine atashiriki uzinduzi wa Kiwanda cha Viuadudu vya kuua viluwiluwi vya mbu wanaoeneza malaria.
Waziri Mkuu wa Ethiopia, Mhe. Desalegn akisalimiana na Kaimu Katibu Mkuu wa Wizara ya Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Kimataifa na Mkurugenzi Idara ya Asia na Australasia, Balozi Mbelwa Kairuki mara baada ya kuwasili Uwanja wa Ndege wa Kimataifa wa Julius Nyerere Jijini Dar es Salaam
Waziri Mkuu, Mhe. Pinda akimtambulisha Balozi wa Tanzania nchini Ethiopia, Mhe. Naimi Aziz kwa Waziri Mkuu wa Ethiopia, Mhe. Desalegn.
 Waziri Mkuu wa Ethiopia, Mhe. Desalegn. akisalimiana na Kaimu Mkurugenzi wa Idara ya Afrika katika Wizara ya Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Kimataifa, Bi. Zuhura Bundala
Afisa Mambo ya Nje, Bw. Mudrick Soraga naye akisalimian na Mhe. Desalegn 
Waziri Mkuu wa Ethiopia akikagua Gwaride la Heshima mara baada ya kuwasili huku akisindikizwa na Mhe. Pinda
Waziri Mkuu wa Ethiopia, Mhe. Desalegn kwa pamoja na Mhe. Pinda wakimsikiliza Mhe. Membe wakati wa mazungumzo mafupi mara baada ya Mhe. Desalegn kuwasili.


............Matukio zaidi ya ziara ya Waziri Mkuu wa Ethiopia nchini

Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania,  Dkt. Jakaya Mrisho Kikwete akiwa na Mhe. Desalegn, Mhe. Pinda na Bi. Joyce Phumaphi, Katibu Mtendaji wa Taasisi ya Viongozi wa Afrika walio mstari wa mbele katika  kupambana na Malaria  (ALMA). Mhe. Desalegn ndiye Mwenyekiti wa sasa wa Taasisi hiyo wakati wa hafla ya chakula cha jioni iliyoandaliwa Ikulu kwa heshima ya Mhe. Desalegn.
Balozi wa Cuba (kushoto), Mhe. Jorge Luis Lopez Tormo akiwa pamoja na Mkurugenzi  wa Idara ya Ulaya na Amerika, Balozi Joseph Sokoine (wa pili kushoto), wakimsikiliza Mkurugenzi na Mkuu wa Itifaki, Balozi Juma Maharage wakati wa hafla ya chakula cha jioni kwa heshima ya Waziri Mkuu wa Ethiopia.
Balozi wa Tanzania nchini Ethiopia, Mhe. Naimi Aziz (mwenye kitambaa kichwani) akiwa na Kaimu Mkurugenzi  wa Idara ya  Afrika katika Wizara ya Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Kimataifa,  Bi. Zuhura Bundala pamoja na wageni wengine waalikwa wakati wa hafla ya chakula cha jioni kilichoandaliwa Ikulu kwa heshima ya Waziri Mkuu wa Ethiopia.

Picha na Reginald Philip

Tuesday, June 30, 2015

Press release




H.E. Jakaya Mrisho Kikwete, President of the United Republic of Tanzania has sent a condolences message to H. H. Sheikh Sabah Al Ahmad Al Sabah, Amir of the State of Kuwait following the tragedy death of 27 innocent Kuwait nationals and hundreds who sustained injuries caused by terror attack  which occurred on 26th June, 2015. The message reads as follows;



“His Highness Sheikh Sabah al-Ahmad al-Jabir al-Sabah,

Amir of the State of Kuwait,

Kuwait City.



Your Highness,



I have learnt with deep sorrow and sadness the tragedy unexpected demise of 27 innocent Kuwait nationals and left hundreds who sustained injuries caused by terror attack on a Shia mosque which occurred on 26th June, 2015.



On behalf of the Government and  the People of the United Republic of Tanzania I wish to convey to you, and through you, to the people of the State of Kuwait, particularly the families of the bereaved our heartfelt condolence  and deep sympathies.



The Government of the United Republic of Tanzania condemns in the strongest terms the terror attack which took place at one of Kuwait’s oldest Shia mosques during midday prayers.

 

In this time of grief, our heartfelt and prayers are with the families of the victims and the people of the State of Kuwait in general.



Please accept, Your Highness, the assurance of my highest consideration.





Issued by: Ministry of Foreign Affairs and International Cooperation, Dar es Salaam. 30th June, 2015



BALOZI WA TANZANIA NCHINI KENYA AKUTANA NA RAIS DK.SHEIN LEO

Rais wa Zanzibar na Mwenyekiti wa Baraza la Mapinduzi Dk.Ali Mohamed Shein akisalimiana na Balozi Mteule wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Nchini Kenya Mhe,John Michael Haule alipofika Kujitambulisha Ikulu Mjini Zanzibar leo.
Rais wa Zanzibar na Mwenyekiti wa Baraza la Mapinduzi Dk.Ali Mohamed Shein akizungumza na  Balozi Mteule wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Nchini Kenya Mhe,John Michael Haule alipofika Kujitambulisha Ikulu Mjini Zanzibar leo. 
Rais wa Zanzibar na Mwenyekiti wa Baraza la Mapinduzi Dk.Ali Mohamed Shein akibadilishana mawazo na Balozi Mteule wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Nchini Kenya Mhe,John Michael Haule baada ya mazungumzo yao alipofika Kujitambulisha Ikulu Mjini Zanzibar leo.

Friday, June 26, 2015

Rais Kikwete atumia fursa ya maadhimisho ya Miaka miwili ya Papa Francis kuwa madarakani kuwaaga Maaskofu



Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Dkt. Jakaya Mrisho Kikwete akitoa Hotuba yake kwenye maadhimisho ya Siku ya kitaifa ya Taifa la Vatican pamoja na kuadhimisha miaka miwili ya Baba Mtakatifu, Papa Franci kuwa madaraki kwenye Ubalozi wa Vatican hapa nchini.  Rais Kikwete ameipongeza Vatican kwa kuwa na mahusiano mazuri na Tanzania, pia alitumia nafasi hiyo kuwaaga Maaskofu wote wa Tanzania walio kuwepo kwenye maadhimishi hayo ikiwa ni sherehe yake ya mwisho akiwa madarakani. maadhimisho hayo yalifanyika katika makazi ya Balozi wa Vatican hapa nchini Askofu Padilla tarehe 26.06.2015, na kuhudhuriwa na Waziri wa Mambo ya nje Bernard Membe (Mb.), Kaimu Mufti Mkuu wa Tanzania Sheikh Abubakar Zuber Bin Ally na Muadhama Polycarp Kardinal Pengo, Mabalozi na maaskofu wa kanisa katoliki hapa nchini.  
Rais Kikwete akiendelea kuhutubia huku Waziri Membe na Askofu Padilla (Kushoto) wakifuatilia kwa makini hotuba hiyo.
Balozi wa Vatican Askofu Padilla naye akitoa hotuba yake katika maadhimisho hayo.
Waziri wa Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Kimataifa, Mhe. Bernard Kamilius Membe (Mb.) akitoa salamu za pongezi ya maadhimisho ya miaka miwili ya Baba Mtakatifu, Papa Francis wakati wa maadhimisho hayo katika Ubalozi wa Vatican uliopo hapa nchini  
Viongozi mbalimbali wa Kidini, Mabalozi na Wakuu wa Mashirika ya Kimataifa nchini wakisikiliza kwa makini Hotuba zilizo kuwa zikitolewa na rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Dkt Jakaya Mrisho Kikwete, Mwakilishi wa Baba Mtakatifu nchini Askofu Francisco Montecillo Padilla na Waziri wa Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Kimataifa Mhe. Bernard Membe (Mb.) hawapo pichani
Rais Kikwete(Kulia) akifanya akigonganisha Glasi na Muadhama Polycarp Kardinal Pengo (Wa kwanza kushoto) na Balozi wa Vatican Askofu Montecillo Padilla kama ishara ya kumtakia Baba Mtakatifu Afya njema na miasha marefu wakati wa maadhimisho hayo.

juu na chini: Rais Kikwete akigonganisha Glasi na Rais wa Baraza la Maaskofu Katoliki Tanzania Askofu Tarcisius Ngalalekumtwa nchini na Waziri Membe.
Waziri Membe akimtambulisha Kaimu Mkuu Mufti wa Tanzania Sheikh Ally (Kulia) kwa Balozi wa Vatican nchini Askofu Padilla
Waziri Membe (Katikati) akimtambulisha Kaimu Mufti Mkuu wa Tanzania Sheikh Abubakar Zuber Bin Ally kwa Balozi wa Uingereza nchini Tanzania Mhe. Dianna Melrose 
Rais Kikwete (Wa pili kushoto) akiwa katika picha ya pamoja na Waziri wa Mambo ya nje na Ushirikiano wa Kimataifa Mhe. Bernard Kamilius Membe (Wa kwanza kulia), Balozi wa Vatican nchini Askofu Padilla (Wa kwanza Kushoto) na Kaimu Mkuu Mufti wa Tanzania Sheikh Abubakar Zuber Bin Ally 
Rais Kikwete akiagana na Maaskofu mara baada ya kumalizika kwa maadhimisho hiyo  
Waziri Membe (Kushoto) akizungumza jambo na Balozi Askofu Padilla
Waziri Membe naye akiagana na Maaskofu mara baada ya kumalizika kwa Maadhimisho hayo.

Picha na Reginald Philip