Wednesday, August 24, 2016

KONGAMANO LA WATANZANIA WANAOISHI UGHAIBUNI KUANZA LEO ZANZIBAR


Mkuu wa Kitengo cha Mawasiliano ya Serikali na Msemaji wa Wizara ya Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki, Bi. Mindi Kasiga akizungumza na Wanahabari (hawapo pichani) katika Ukumbi wa Mikutano wa Kimataifa wa Julius Nyerere Jijini Dar es Salaam. Katika Mkutano huo na Wanahabari Bi. Mindi Kasiga aliujulisha umma kuhusu kufanyika kwa Kongamano la siku mbili (24 -25 Agosti, 2016) la Watanzania wanaoishi Ughaibuni (Diaspora) linalotajiwa kuanza leo Mjini Unguja, Zanzibar.
Mmoja wa Watanzania anayeishi ughaibuni ambaye pia ni Mdau wa Michezo, Bw. Emmanuel Nasaa akizungumza na Wanahabari. Katika mazungumzo yake, Bw. Emmanuel Nasaa alielezea umuhimu wa Watanzania wanaoishi ughaibuni (Diaspora) kushiriki katika kuchangia jitihada za maendeleo nchini kupitia Sekta mbalimbali

Naibu Waziri wa Mambo ya Nje ahudhuria mkutano wa Mawaziri wa ushirikiano wa Afrika na Singapore

Naibu Waziri wa Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki, Mhe. Dkt. Susan Kolimba (wa pili kutoka kushoto), akifanya mazungumzo na Waziri wa Viwanda na Biashara nchini Singapore, Mhe. Dkt. Koh Poh Koon (wa tatu kutoka kushoto), wa kwanza kushoto ni Afisa Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki Emannuel Luangisa. Dkt. Kolimba yupo nchini Singapore kuhudhuria mkutano wa pili wa "Singapore - Sub Saharan Africa High Level Ministerial Exchange Visit" 
Naibu Waziri wa Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki, Mhe. Dkt. Kolimba akizungumza na Balozi wa Heshima wa Tanzania nchini Singapore, wakati ulipoutembelea ubalozi huo.
Naibu Waziri wa Mambo ya Nje na Ushirikano wa Afrika Mashariki, Dkt. Susan Kolimba (wa nne kutoka kulia) akiwa katika picha ya pamoja na Mawaziri wenzake mara baada ya kumalizika mkutano wa Sub - Sahara Afrika

Rais Magufuli apokea Hati za Utambulisho kutoka kwa Waheshimiwa Mabalozi wa Ireland, Somalia, Italia na Korea Kusini

Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Mhe. Dkt. John Pombe Magufuli akipokea Hati za Utambulisho kutoka kwa Balozi wa Ireland nchini Tanzania, Mhe. Paul Sherlock Ikulu Jijini Dar es Saalam
Balozi wa Ireland nchini Tamzamia, Mhe. Paul Sherlock akisaini Kitabu cha Wageni Ikulu Jijini Dar es Salaam
Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Mhe. Dkt John Pombe Magufuli akiwa katika picha ya pamoja na Balozi wa Ireland nchini, Mhe. Paul Sherlock (wa tatu kushoto). Wengine katika picha, kulia kwa Mhe. Balozi ni Maafisa alioambatana nao na kutoka kulia Balozi Zuhura Bundara, Mshauri wa Rais wa masuala ya Diplomasia na Balozi Joseph Sokoine, Kaimu Katibu Mkuu, Wizara ya Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki.
Balozi Mteule wa Somalia nchini Tanzania, Mhe. Mohammed Hassan Abdi akisaini Kitabu cha Wageni Ikulu Jijini Dar es Saalam kabla ya kuwasilisha Hati za Utambulisho kwa Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Mhe. Dkt. John Pombe Magufuli

Balozi wa Somalia nchini Tanzania, Mhe. Mohammed Hassan Abdi akiwasilisha Hati za Utambulisho kwa Mhe. Dkt. John Pombe Magufuli, Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania
Balozi Mteule wa Somalia nchini Tanzania, Mhe. Mohammed Hassan Abdi (katikati) akitoa heshima wakati Wimbo wa Taifa ulivyokuwa ukipigwa mara baada ya kuwasili Ikulu Jijini Dar es Saalam kuwasilisha Hati za Utambulisho kwa Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Mhe. Dkt. John Pombe Magufuli. Kushoto kwa Mhe. Balozi ni Kaimu Mkuu wa Itifaki, Bw. James Bwana.
Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mhe. Dkt John Pombe Magufuli akiwa katika mazungumzo na Balozi wa Somalia nchini Tanzania, Mhe. Mohammed Hassan Abdi mara baada ya kuwasilisha Hati za utambulisho

Balozi Mteule wa Italia nchini Tanzaia, Mhe.Roberto Mengoni akisaini kitabu cha wageni mara baada ya kuwasili Ikulu, Jijini Dar es Salaam kwa ajili ya kuwasilisha Hati za Utambulisho kwa Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Mhe. Dkt. John Pombe Magufuli.
Balozi wa Italia nchini Tanzania, Mhe. Roberto Mengoni akiwasilisha Hati zUtambulisho kwa Mhe. Dkt. John Pombe Magufuli, Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania

Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mhe. Dkt John Pombe Magufuli akisalimia na Balozi Mteule wa Italia, Mhe. Roberto Mengoni Ikulu Jijini Dar es Salaam
Balozi wa Italia nchini, Mhe. Roberto Mengoni (katikati) akitoa heshima kwa wimbo wa Taifa alipowasili Ikulu kuwasilisha Hati za Utambulisho kwa Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Mhe. Dkt. John Pombe  Magufuli
Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mhe. Dkt. John Pombe Magufuli akiwa katika picha ya pamoja na Viongozi kutoka Ofisi ya Ubalozi wa Italia na Wizarani. Wapili kulia ni Balozi Joseph  Sokoine, Kaimu Katibu Mkuu wa Wizara ya Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki na wa kulia ni Balozi Zuhura Bundala, Mshauri wa Masuala ya Diplomasia wa Rais.




Balozi Mteule wa Jamhuri ya Watu wa Korea nchini Tanzania, Mhe. Kim Yong Su akisaini Kitabu cha Wageni Ikulu Jijini Dar es Salaam kabla ya kuwasilisha Hati za Utambulisho kwa Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Mhe. Dkt. John Pombe Magufuli.
Balozi wa Jamhuri ya Watu wa Korea nchini Tanzania, Mhe. Kim Yong Su akiwasilisha  Hati za Utambulisho kwa Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Mhe. Dkt. John Pombe Magufuli
Mhe. Rais Dkt John Pombe Magufuli akiwa katika mazungumzo na  Balozi wa Jamhuri ya Watu wa Korea Mhe. Kim Yong Su mara baada ya kuwasilisha Hati za Utambulisho




Friday, August 19, 2016

Waziri Mahiga akutana na Mjumbe Maalum wa Waziri Mkuu wa Japan

Waziri wa Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki, Mhe. Dkt. Augustine Mahiga (kulia) akizungumza na Mjumbe Maalum wa Waziri Mkuu wa Japan, Mhe. Balozi Junzo Fijita aliyetembelea katika ofisi za Wizara Jijini Dar es Salaam tarehe 19 Agosti, 2016.
Balozi wa Japan nchini, Mhe. Masaharu Yoshida  (kushoto) pamoja na Afisa aliyefuatana naye wakifuatilia mazungumzo.
Mkurugenzi wa Idara ya Asia na Australasia, Balozi Mbelwa Kairuki (kushoto) pamoja na Afisa Mambo ya Nje, Bi. Bertha Makilagi wakifuatilia mazungumzo.
Mazungumzo yakiendelea
Wakiagana mara baada ya mazungumzo

Wanawake wa Mambo ya Nje wamuaga Balozi Mulamula

Naibu Waziri wa Wizara ya Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki, Dkt. Susan Kolimba akiongea na Wanawake wa Wizara ya Mambo ya Nje walioshiriki katika kikao cha kumuaga Balozi Liberata Mulamula, kilichofanyika katika Ukumbi wa Kimataifa wa Julius Nyerere Jijini Dar es Salaam. Balozi Mulamula ambaye amestaafu utumishi wa umma alikuwa Katibu Mkuu wa kwanza mwanamke kuongoza  Wizara ya Mambo ya Nje pia mlezi wa Umoja wa Wanawake wa Wizara hiyo (Nje Women). Mhe. Naibu Waziri alimshukuru Balozi Mulamula kwa kuimarisha umoja wa wanawake wa Wizara na kuahidi kuendelea kuenzi mchango wake kwenye umoja huo.
Balozi Liberata Mulamula akitoa neno la shukrani kwa Wajumbe (hawapo pichani) ambapo aliwaasa kuendelea kutekeleza majukumu yao ya kila siku kwa bidii huku wakizingatia weledi ili kuwa mfano bora kazini, kwenye familia na taifa kwa ujumla.
Balozi Mulamula akimkabidhi Naibu Waziri, Mhe. Kolimba mwongozo wa Umoja huo baada ya kuchaguliwa kuwa Mlezi mpya.
Sehemu ya Watumishi wanawake wa Wizara ya Mambo ya Nje wakifuatilia kikao.
Sehemu nyingine ya Watumishi hao wakifuatilia kikao
Mkurugenzi Msaidizi wa Idara ya Utawala na Rasilimali Watu ambaye pia ni Mwenyekiti wa Umoja wa Wanawake, Bibi. Amisa Mwakawago akitoa taarifa fupi ya Umoja kwa mama mlezi mteule na kwa Wajumbe wengine walioshiriki kikao. Kulia ni Katibu wake, Bi. AnnaGrace Rwalanda.
Dkt. Kolimba akimkabidhi zawadi Balozi Mulamula. 
Bibi. Mwakawago akimkabidhi Balozi Mulamula zawadi ya picha yake ya kuchorwa.
Mkuu wa Kitengo cha Mawsiliano na Msemaji wa Wizara ya Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki ambaye pia ni mjumbe wa Umoja wa Wanawake (Nje Women) akitoa neno la shukrani kwa Balozi Mulamula.
Kikao kikiendelea
Picha ya Pamoja ya walezi na uongozi wa Nje Women

Picha ya pamoja.


Mkutano wa tano wa Bunge la tatu la Jumuiya ya Afrika Mashariki (EALA) kuanza Arusha

JAMHURI YA MUUNGANO WA TANZANIA
WIZARA YA MAMBO YA NJE NA USHIRIKIANO WA AFRIKA MASHARIKI
 


Simu: 255-22 211906-12, 2126827  

Fax: +255-22 2116600, 2120488/2126651
Barua pepe: gcu@nje.go.tz

Tovuti: www.foreign.go.tz/ www.meac.go.tz


                20 KIVUKONI FRONT,
                           P.O. BOX 9000,
            11466 DAR ES SALAAM, 
                                    Tanzania.

 
TAARIFA KWA VYOMBO VYA HABARI
Mkutano wa tano wa Bunge la tatu la Jumuiya ya Afrika Mashariki (EALA) kuanza  Arusha
Bunge la Jumuiya ya Afrika Mashariki (EALA) linatarajia kuanza vikao vyake mapema wiki ijayo Jijini Arusha, Tanzania, kwa muda wa wiki mbili kuanzia Jumatatu Agosti 22, 2016 hadi Ijumaa Agosti 2, 2016.

Pamoja na mambo mengine Bunge hilo linatarajia kujadili ripoti ya ukaguzi wa hesabu kutoka Kamati ya Fedha kwa mwaka ulioishia Juni 30, 2015. Ripoti hiyo inayozingatia na kuonyesha taarifa za ukaguzi wa hesabu za fedha kwa mwaka ulioishia Juni 30, 2015, inahusisha taasisi na vyombo mbalimbali vilivyopo chini ya Sekretariati ya Jumuiya ya Afrika Mashariki pamoja na Miradi 20 inayotelezwa na kusimamiwa na Sekretariati, kwa mujibu wa kifungu cha sheria namba 134 ya Mkataba wa uanzishwaji wa Jumuiya ya Afrika Mashariki.

Tume ya ukaguzi iliwasilisha ripoti yake kwenye Baraza la Mawaziri na kujadiliwa na Baraza hilo Mei 24, 2016. Ripoti hii ya tume ya ukaguzi inayoonesha kuwa bajeti imetekelezwa kwa 65% inajadiliwa kipindi ambacho Jumuiya inapitia kipindi kigumu cha ukosefu wa fedha.
Pia Bunge linatarajia kujadili ripoti ya Kamati ya Kilimo, Utalii na Maliasili kuhusu uangalizi wa shughuli za Utalii katika Jumuiya. Vilevile Bunge litajadili ripoti nyingine ya kamati ya Kilimo, Utalii na Biashara ambapo itaangazia hali ya ujangili ndani ya JumuiyaKama sehemu ya kudumisha ushirikiano na wadau wengine kwenye kanda, EALA itapokea ripoti kuhusu masuala ya vijana ndani ya Jumuiya kufuatia matokeo ya utafiti uliofanywa na Shirika la Afrika Mashariki (The East African Institute) chini ya uangalizi wa Shirika la Mtandao wa Maendeleo la Aga Khan (Aga Khan Development Network)
Vikao vya EALA vinafanyika kwa utaratibu wa mzunguko miongoni mwa Nchi Wanachama kwa mujibu wa kifungu cha sheria namba 55 ya Mkataba wa Uanzishwaji wa Jumuiya ya Afrika Mashariki. Wakati huohuo Bunge linafanya kazi kwa ukaribu na wadau mbalimbali sambamba na kupokea taarifa kuhusu Bunge hilo. Bunge hilo linatarajiwa kuongozwa na Spika wake Mhe. Daniel Kadega.

Mwisho
Imetolewa na:
Kitengo cha Mawasiliano ya Serikali,
Wizara ya Mambo ya Nje, Ushirikiano wa Afrika Mashariki
Dar es Salaam, 26 Mei 2016.




Thursday, August 18, 2016

Waziri Mahiga akutana na Balozi wa China nchini


Waziri wa Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki, Mhe. Dkt. Augustine Mahiga akizungumza na Balozi wa China nchini, Mhe. Lu Youqing alipomtembelea katika ofisi za Wizara Jijini Dar es Salaam leo tarehe 19 Agosti, 2016. Mazungumzo yao yalijikita katika kujadili masuala ya ushirikiano kati ya Tanzania na China na taratibu zinazoendelea kwa upande Serikali za kuhamia Dodoma. 
Mkurugenzi wa Idara ya Asia na Australasia katika Wizara ya Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki, Balozi, Mbelwa Kairuki pamoja na Mkuu wa Kitengo cha Mawasiliano ya Serikali na Msemaji wa Wizara ya Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki, Bi. Mindi Kasiga na Afisa Mambo ya Nje, Bw. Halmenshi Lunyumbu wakifuatilia mazungumzo. 
Mazungumzo yakiendelea

Wakiwa katika  picha ya pamoja

Waziri Mahiga akutana na Balozi wa Israel nchini


Waziri wa Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki, Mhe. Dkt. Augustine Mahiga akizungumza na Balozi wa Israel nchini Mhe. Yahel Vilan alipomtembelea katika ofisi za Wizara Jijini Dar es Salaam leo tarehe 18 Agosti, 2016. Katika mazumgumzo yao walijadili namna ya kuimarisha ushirikiano baina ya mataifa yao hususan katika sekta za Kilimo, Elimu na Masuala ya kuwawezesha Wanawake katika kufikia maendeleo.
Mhe. Yahel akimweleza Waziri Mahiga namna Serikali ya Israel ilivyofanikiwa katika miradi ya kilimo na umwagiliaji ambayo imesaidia katika kuwahakikishia wananchi wake upatikanaji wa chakula.
Mkurugenzi wa Idara ya Mashariki ya Kati katika Wizara ya Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki, Balozi Abdallah Kilima (wa kwanza kushoto) pamoja na Maafisa  Mambo ya Nje  Bw. Hangi Mgaka (wa pili kushoto) na Bi. Kisa Doris Mwaseba wakifuatilia mazungumzo
Mazungumzo yakiendelea
Wakijadili jambo mara baada ya mazungumzo

Katibu Mkuu wa Mambo ya Nje akutana na Mkurugenzi wa Kampuni ya SMH RAIL ya Malaysia

Katibu Mkuu wa Wizara ya Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki, Balozi, Dkt. Aziz Mlima (kulia) akizungumza na Mkurugenzi wa Masoko wa SMH RAIL Bw. S. Rajamohan ya Malaysia alipomtembelea katika ofisi za Wizara Jijini Dar es Salaam. Katika mazungumzo yao walijadili kuhusu fursa za uwekezaji zilizopo nchini hususan katika miundombinu ya reli.
Bw. S. Rajamohan akielezea namna kampuni ya SMH RAIL inavyofanya shughuli zake na utayari wao wa kuja kuwekeza nchini.
Mazungumzo yakiendelea



Wednesday, August 17, 2016

Waziri Mahiga apokea hati za utambulisho za Mwakilishi mpya wa WFP nchini

Waziri wa Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki, Mhe. Dkt. Augustine Mahiga akipokea Hati za Utambulisho kutoka kwa Mwakilishi mpya wa Shirika la Mpango wa Chakula Duniani (WFP) hapa nchini, Bw. Michael Dunford. Hafla hiyo fupi ilifanyika Wizarani tarehe 17 Agosti, 2016.
Mhe. Waziri Mahiga akizungumza na Bw. Dunford mara baada ya kupokea hati zake za utambulisho
Bw. Dunford nae akimweleza jambo Mhe. Waziri
Mazungumzo kati ya Mhe. Mahiga na Bw. Dunford yakiendelea. Wengine katika picha ni Bi. Eva Ng'itu (kushoto) na Bi. Sekela Mwambegele, Maafisa Mambo ya Nje.